Ulishawahi kupanda daladala ya madereva wanaokimbizana?

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,679
Reaction score
5,165
Kuna muda ni vyema kuyakubali mabadiliko ili kileta tija na ushindani katika sekta zetu za maisha,wakati mwengine akili ya binadamu ipo based on benefits bila ya kucompare athari ya hatua anazozichukua.

Jana nimepanda daladala ya kutoka mbezi - Karikoo mida flani ya saa 7, kulikuwa na gari 2 aina ya costal zinakimbizana sijui changamoto hua ni aboria au kuwahi kituoni.

Mpaka nafika to my destination kichwa na kiuno vilikua kwenye maumivu makubwa,nashindwa kufahamu hawa jamaa wanawaza nini hasa wawapo barabarani.

Nimejikuta nakumbuka akili mnemba naona ni ahueni waingie kwenye soko la daladala ili kudhibigi ujinga huu wa akili za kibinadamu.

walamsiki
 
Pole sana,nunua hata Ist!
 
Nakumbuka niliomba kushuka wakasema mimi mshamba wa vijijini, nikalazimisha nikashuka, kilometer kama moja hivi, nilikuta wamechafuka vumbi na damu, na dereva kondakta hawapo. Nilimshukuru Mungu Sana.
 
Duuh maswala ya daladala kukimbizana sio poa.
Almanusura tuvamie gari la taka, mfpyuuuuu zake anataka kutuletea mushkeli asubuhi asubuhi hata chai hatujanywa.
ni changamoto kwa madereva wetu
 
Mimi sio daladala tu lakini hata mabasi ya mikoani masafa marefu.
Siko tayari mhuni ambae hana cha kupoteza kuhatarisha maisha yangu.
Sheria zinewekwa tuzifuate.
La sivyo naku report ukifika mahala unaambiwa Mwambie boss wako alete dereva mwingine au atrapę wa onto kali .
Mara nyingi ukiwaonya huwa wanasikia na kuanza kunyata makusudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…