Uliona wapi?

Uliona wapi?

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,758
Reaction score
9,589
HABARINI MABESTITO:

Nimekuja kivingine kabisa kwa wale walionizoea watashaangaa kuona ladyf leo vipi kaja na kaswali ndani yake
watashangaa kulikoni leo mswahiba wetu kaingia spidi haina gavana kwa kututandika kaswaili ,

mabestito wangu wala msihofu kuna wakati tunakuja kwa kuwatia moyo, kuna wakati tunakuja kwa kuwakandamiza
wale wote wasioweza kujirekebisha tabia zao hususani WANAUME na kuna wakati mwingine tunakuja kuchemsha bongo pia. Leo Mfundaji wenu nimekuja na kitu ambacho nimekiweka kama swali ila kimenikera sasa naona nije kuwaelemisha
na kuwafunda wale ambao wanatabia hii waiache mara moja kwani haipendezi kwa jamii

ULIONA WAPI?

Bestito uliona wapi Mwanaume mzima umekuwa tegemezi kwa mkeo,? wewe kila kukicha huna pa kueleweka
kikazi, kibiashara wala kishughuli yoyote unakinga mkono hutadhani wale tunaowasaidia ambao hawana
uwezo wa kujisaidia? Hunashindwa hata kufanya biashara ndogondogo familia yako ikapata kitu toka kwako
Je uliomuolea nini binti wa watu mpaka unamchosha kwa kwa kuwa tegemeizi , Mwanamke huyohuyo atafuta
pesa, huyohuyo aijali familia, huyohuyo tena awalee watoto uliompa, huyohuyo tena awaangalie wazazi wa pande
zote mbili, huyohuyo tena akupe mahitaji yote ya kifamilia. Jamani si unamchosha mtoto wa watu na unamzeesha
bure kabla ya wakati wake. Kwanini usijitume nawe ili familia yenu iwe bora na yenye kustawi?

Upande wapili nao tena

Uliona wapi Mwanamke mwenzangu nawe unakaa tu unasubiri eti baba alete maakuli ndipo ukinge kwenye bakuli
uanze kula, Baba achakarike huko kwa kila hali nawe umekaa huna chochote cha kukuingizia kipato jamani mwanamke
mwenzangu kwanini wakati kuna shughuli nyingi za kufanya kuna kusuka mikeka, kushona, kufanya kile kitu halali cha
kukuingizia kipato kwanini unakaa tu unasubiri jioni mzee akija akurushie alichopata huko hujui kuwa amefanyaje mpaka
akapata hayo manoti, au vitu . Mwanamke mwenzangu usiniangushe wanawake tunaweza muombe mumeo hela ya
kuanzisha biashara kama huna kitu cha kufanya mshirikishe, muombe kwa kumbembeleza sana ili akupe msingi nawe
usiwe golikipa uweze kuiwezesha familia yako.

MABESITO NAWAASA NA KUWAFUNDA

Kwa nguvu na umoja wa pande zote mbili utasababisha familia kuendelea na hakutakuwa na huhitaji labda ule wa lazima kama familia , Mabestito wangu msimu ndo ushazimika wa mwaka huu 2014 tujitume kwa biidii zetu tusiwe watu wa kumfanya mwenzio hahuzunike kwa wewe kutokufanya kitu cha kuleta maendeleo ndani ya ndoa yenu
Kwa nguvu zote tunaweza kuleta mabadiliko ndani ya ndoa na ndoa zetu zikapona na watoto wakaiga mfano wa wazazi wao

namalizia kwa kwa swali langu pale juu ULIONA WAPI mtama ukakua na kuchanua na kuleta utofauti ndani ya ndoa?

Wasaalamu,

Ladyf

cc: Mamndenyi, Kongosho, @Mtambuzi Asprin, KakaKiiza, Jiwe Linaloishi, Kipaji Halisi, Paloma, mwallu, Chocs, Erickb52, Arushaone, Lady doctor, Passion Lady, charminglady, utafiti, Husninyo, watu8, @Mentor, Asnam, amu, Ntuzu, muuza ubuyu, Excel, @Ben Mugashe, Filipo, Chachu Ombara, sister, Heaven on Earth, Kokutona na marafiki zangu wote karibuni
 
ladyfurahia a.k.a............ Hiyo ya pili inaweza kuwepo na haikeri kiviiiiile, inategemea mnaishije ila hiyo ya kwanza inakuaje kuaje mwanaume awe anapewa huduma kama mwanamke?? Hii haiingii akilini
 
Last edited by a moderator:
Kwa mwanume, sio jambo zuri for sure.. Men are meant to sweat and provide for their women...
For women, I cant say much about that, because wengi hukatazwa kufanya kazi na waume zao.. This evident, kama sio kwenu, basi kwa jirani yenu. And this is the case in the Arab world.
 
Kwa nn hujawashauri wanawake wenye waume tegemezi wawape mitaji waume zao!? Naona habari yako ni km bado unakumbatia mfumo dume badala ya 50/50. Me nimesema tu lkn ingawa hujanitagg. Ngoja waje wenyewe.
 
Yf anasema mii mchumi, madada wanaonizengea wanasema mii bahili!
 
Aiseee bora ntafute Mwanamke nimuowe anihudumie....! Kuhudumiwa raha jamani...!
 
:suspicious::suspicious::suspicious::suspicious: hawa ndo walewale wanaouzungumiziwa tegemezi (jokes)
Aiseee bora ntafute Mwanamke nimuowe anihudumie....! Kuhudumiwa raha jamani...!
 
asante kwa kunisaidia kwa hili barikiwa wameona nao watafanya
Kwa nn hujawashauri wanawake wenye waume tegemezi wawape mitaji waume zao!? Naona habari yako ni km bado unakumbatia mfumo dume badala ya 50/50. Me nimesema tu lkn ingawa hujanitagg. Ngoja waje wenyewe.
 
kumbe heeeeeee sijawahi ona hii ila nilisikia kule zenji wengi wa wanawake wanakatazwa kufanya chochote wao ni kusubiri mzee alete kila kitu nao huingia majikoni na kutayarisha mambo

ila kwa upande wa mwafrika jambo hili si busara wote mchakarike na jioni mkabidhiane yale mlioyachakarikia mchana kutwa ndo mpango mzima huo
Kwa mwanume, sio jambo zuri for sure.. Men are meant to sweat and provide for their women...
For women, I cant say much about that, because wengi hukatazwa kufanya kazi na waume zao.. This evident, kama sio kwenu, basi kwa jirani yenu. And this is the case in the Arab world.
 
Back
Top Bottom