Ulimpataje mwenza/mchumba/mpenzi wako?

Ulimpataje mwenza/mchumba/mpenzi wako?

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,427
Reaction score
10,749
Wadau,
"Ka jioni hivi, nipo kando ya mto nachunga mbuzi 16 wa home kando ya mto. Sasa pale mtoni kuna sehemu ya wasichana na sehemu ya wavulana. Ktk mbuzi wale nakumbuka kuna beberu moja sumbufu likakurupuka toka kundini nikaanza kulifukuza. Katika makona kona likatokezea upande waogao akina dada, hapo ndipo nilipagawa! Niliwakuta wadada watatu wanaoga mmoja mkubwa wa rika langu wengine vitoto tu. Basi yule mkubwa akakimbilia nguo fasta, akajifunga kanga. Nilimuomba samahani sana japo alinitusi kwa hasira. Mi niliendelea kumfukuza mbuzi huku image ya yule dada ikijirudia kichwani mpaka usiku sikulala vzr!
Baada ya mwezi nilikutana nae sokoni, looh si alinikumbuka! Kuanzia hapo ndo nikaanza kufukuzia kwa bidii maana hakika moyo wangu uligala gala kabisaaa kwake....! Mpaka naandika, sasa ni mama watoto wangu.

Mwana JF hasa hapa MMU, tushirikishane namna tulivyowapa wapenzi wetu. Karibuni....

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Nilikutana nae porini nina ukame balaa nlikuwa jela miaka 8...nkampiga ngwala akapiga kelele kabla sijampa mambo watu wakajaa nikafungishwa ya mkeka.
 
Dah wangu nilimpata chuo alikuwa 1st year me nikiwa 2nd .Duh long story wakubwa
 
Nilienda benki kulipa ada ya nusu muhura wakati huo nikiwa chuo mwaka wa nne,pesa yote niliiweka kweny kibegi changu cha vitabu,kumbe wakati navuka barabara ilidondoka yote.Niliingia ndani kutaka kujaza form ya kuweka nakuta sina kitu.Nilichanganikiwa.Nilitoka nje ili nianze kutafuta.Ile naigia barabarani niliona binti mwupe, mwembaba alievalia sare sa shule akinifuata na kunambia 'Kaka ulidondosha hela yako' huku akinikabidhi pesa yangu ikiwa vilevile.Sikuamini nilifurahi sana.Kipindi hicho alikua form 4.Leo ni mke Wangu mama wa mtoto mmoja na mapacha wawili nampenda sana.
 
Nilienda benki kulipa ada ya nusu muhura wakati huo nikiwa chuo mwaka wa nne,pesa yote niliiweka kweny kibegi changu cha vitabu,kumbe wakati navuka barabara ilidondoka yote.Niliingia ndani kutaka kujaza form ya kuweka nakuta sina kitu.Nilichanganikiwa.Nilitoka nje ili nianze kutafuta.Ile naigia barabarani niliona binti mwupe, mwembaba alievalia sare sa shule akinifuata na kunambia 'Kaka ulidondosha hela yako' huku akinikabidhi pesa yangu ikiwa vilevile.Sikuamini nilifurahi sana.Kipindi hicho alikua form 4.Leo ni mke Wangu mama wa mtoto mmoja na mapacha wawili nampenda sana.

Naamini mnaishi maisha ya uaminifu na furaha. Hongera sana best! Real interesting!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Dah wangu nilimpata chuo alikuwa 1st year me nikiwa 2nd .Duh long story wakubwa

Weka ka ufupisho basi tujifunze kaka!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Nilienda benki kulipa ada ya nusu muhura wakati huo nikiwa chuo mwaka wa nne,pesa yote niliiweka kweny kibegi changu cha vitabu,kumbe wakati navuka barabara ilidondoka yote.Niliingia ndani kutaka kujaza form ya kuweka nakuta sina kitu.Nilichanganikiwa.Nilitoka nje ili nianze kutafuta.Ile naigia barabarani niliona binti mwupe, mwembaba alievalia sare sa shule akinifuata na kunambia 'Kaka ulidondosha hela yako' huku akinikabidhi pesa yangu ikiwa vilevile.Sikuamini nilifurahi sana.Kipindi hicho alikua form 4.Leo ni mke Wangu mama wa mtoto mmoja na mapacha wawili nampenda sana.
mwaka wa nne chuo na form four? hukuona mabango ya Haki Elimu? ila mkuu hongera sana ulifanya vyema mwishoni, happy ending story.
 
Wangu nilimpata hiv,nilikua na girlfriend ambae hanizimii kwa kua nilimwambia mimi msukuma mikokoteni.oneday akaja na shost wake wakati anaenda kumnunulia soda akaniacha nae,kamanda nokaomba namba fasta,nikaingiza cd,ikasoma,nikafanya cool revolution.
Picha limeisha.
 
Wakati nipo form 4 nilitokea kumpenda binti wa form 2 jangwani ambae tulikuwa tunasoma tuisheni moja alikuwa mrembo haswa na alikuwa anajisikia sana.basi kidume nikakomaa kumfuatilia lakini nilikuwa napewa majibu ya shombo kwamba Mimi sio level yake.sasa alikuwa na Rafiki yake aliyekuwa anasoma zanaki ikabidi nibadilishe mbinu nimuombe huyu wa zanaki anisaidie na yeye akakubali kuongea na wa jangwani.binti wa zanaki aliimbisha lakini wapi mwishoni nikakata tamaa na nikampotezea.basi yule wa zanaki akawa ananifariji sana na tukaendelea kuwa na mawasiliano.kuifanya story iwe fupi yule binti wa zanaki ndie mke wangu kwa sasa
 
wakati tuko sec alinizidi kidato alinitamani na kila anionapo pande za skuli hapiti bila kunipa hi ila hakuniambia kama amekufa kwangu ila macho yalionyesha. Nilipokua mwaka wa kwanza chuo flan dom pale me shoga angu tukasogea pande za nyerere square kupata lunch, ile tunaingia tu kabla cjavuta kiti nikaangalia pembeni kheeeeeee c nikamwona mshikaji kumbe nae kaja dom kwenye intavyuu. Nikaenda alipokaa nikamsalimia kisha nkaenda kwa rafiki angu tukala kabla cjaondoka pale nkaenda kumuaga, tukapeana namba za simu akanipa pesa i seeee kama alijua vile kunikeshia maana nlifulia vby., kwa hyo safar yake ya dom ilikua ya mafanikio kwan alibahatika kupata ajira na kupata msichana ambae kwa sasa ni mke wake ambae ni mimi hapa., luv u ma bebyiii
 
Mi nilikuwa Tabora pale CRDB kama bank officer na nilikuwa nakaimu nafasi ya MPB so hamna mtu atapata tembocard bila kupitia kwangu. Mwaka huo 2006 tunaenda saba akatokea mmasai binti mrembo balaa daah. Kaja kwangu kupiga picha ya tembocard nikapagawa. Wiki mbili baadae kadi zikaja take nikaificha so nikamwambia anipe namba ya cm I'll nikiipat basi nimpigie aje chukka. Haaa nikaanza msg za mapenzi kawa ananitukana balaa.

Basi nikaone yote heri. Nikampigia day moja, mama eehh kadi imekuja njoo uchukue. Ile kaja nikampa kadi yake lakini password paper nikampa ya mtu mwingine. Akashindwa kuaccess account through ATM. Kaja alalamika huyo kidume namuwinda tuuu. Nikampiga picha ingine, mama eehh hoi kadi imekosewa namba ntakupigia kila baada ya muda kukupa update. Kaniona msamaria kumbe nawinda. Sasa si wawajua wasichana wa pale uhaziri tabora wale warembo hupenda kuheshimiwa na ukubwa ilhali account zao ziko hoi.

Basi kawa aona aibu kuja counter kuchukua pesa na kama akija antaka mie tu. Siku alobugi kaja kutoa elfu hamsini kaandika vocha mie kanipa nikaona muda huuhuu. Nikatoa wallet nkampa pesa hiyo mama nenda siku ingine utanilipa Niko bize ati. Kaona kanpata kumbe hajui. Basi nikawa nunda mama eehh nope hela yangu Nate huyu mwanafunzi hana basi ikawa tarehe baada ya tarehe.

Kaja kustuka msg za luvluv kibao azijibu mara kaamkia nyumbani kwangu shaharibu hivyo. Leo ndo mke wangu Ana mtoto 6 yes na mwingine yuko tumboni aja ila roho yaniuma mie hajanilipa hata leo.
 
Back
Top Bottom