Mtu mbalimbali
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 315
- 413
Habari za muda huu waungwana, wanachama na wapenzi wa Jamiiforum,
Ikiwa leo ni zaidi ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa Jamiiforums, mtandao huu umekuwa kwa kasi sana miongoni mwa Watanzania na wanajamii ya East Africa kwa kuwa Mtandao wa huru na wa haki.
Binafsi naweza sema ni Mtandao wangu pendwa kuliko yote, kwani imekuwa kama kilevi kila nikiwa na bando lazima nichungulie Jamiiforums kuna nini.
Licha ya Mtandao huu kuwa mkubwa hadi kufikia kuwa na watumiaji takribani 632,335 (kwa taarifa za saa 14:20 06/04/2023), bado sio maarufu miongoni mwa Watanzania wengi na hivyo kuwa kama Mtandao fulani wa kisiri ama usiokuwa na wafuatuliaji wengi (unaweza thibitisha hili kwa kuangalia watu wanaokuzunguka na ufahamu wao juu ya Jamiiforum).
Lakini pia miongoni mwetu tunao members waliokuwa bega kwa bega toka miaka ya 2008 na wamesimama na Jamiiforums kwa kipindi chote, huku kila mmoja anahistoria yake ya namna alivyoijua Jamiiforums na hadi kufikia kuwa member kindakindaki.
Uzi huu ni maalum kwaajili ya kuchangia ni kwa namna gani tulikutana na Jamiiforums na hadi sasa tunanufaika vipi, je tunajivunia?
Nianze na mimi Rashmane;
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2017 nikiwa na simu yangu ya kibatani, sina bando, nimeboeka nikaingia freebasics bana walau nipate kuijua dunia.
Wakati naperuzi huku na huku nikakutana kwa mara ya kwanza na JamiiForums na zaidi nilivutiwa na nyuzi za Jamii Intelligence na Educational Forums.
Mwaka 2018 nikafungua account hadi sasa tuko pamoja kuisapoti JF paka iwafikie Watanzania wote kwa ujumla, kwani huu ni Mtandao super hapa Tanzania.
Karibuni kwa maoni na mchango wenu.
Uliijuaje JamiiForums?🎤
NB:
Kama kuna member unatamani kufahamu alifikaje JF waweza kumtag
Mshana Jr
Ikiwa leo ni zaidi ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa Jamiiforums, mtandao huu umekuwa kwa kasi sana miongoni mwa Watanzania na wanajamii ya East Africa kwa kuwa Mtandao wa huru na wa haki.
Binafsi naweza sema ni Mtandao wangu pendwa kuliko yote, kwani imekuwa kama kilevi kila nikiwa na bando lazima nichungulie Jamiiforums kuna nini.
Licha ya Mtandao huu kuwa mkubwa hadi kufikia kuwa na watumiaji takribani 632,335 (kwa taarifa za saa 14:20 06/04/2023), bado sio maarufu miongoni mwa Watanzania wengi na hivyo kuwa kama Mtandao fulani wa kisiri ama usiokuwa na wafuatuliaji wengi (unaweza thibitisha hili kwa kuangalia watu wanaokuzunguka na ufahamu wao juu ya Jamiiforum).
Lakini pia miongoni mwetu tunao members waliokuwa bega kwa bega toka miaka ya 2008 na wamesimama na Jamiiforums kwa kipindi chote, huku kila mmoja anahistoria yake ya namna alivyoijua Jamiiforums na hadi kufikia kuwa member kindakindaki.
Uzi huu ni maalum kwaajili ya kuchangia ni kwa namna gani tulikutana na Jamiiforums na hadi sasa tunanufaika vipi, je tunajivunia?
Nianze na mimi Rashmane;
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2017 nikiwa na simu yangu ya kibatani, sina bando, nimeboeka nikaingia freebasics bana walau nipate kuijua dunia.
Wakati naperuzi huku na huku nikakutana kwa mara ya kwanza na JamiiForums na zaidi nilivutiwa na nyuzi za Jamii Intelligence na Educational Forums.
Mwaka 2018 nikafungua account hadi sasa tuko pamoja kuisapoti JF paka iwafikie Watanzania wote kwa ujumla, kwani huu ni Mtandao super hapa Tanzania.
Karibuni kwa maoni na mchango wenu.
Uliijuaje JamiiForums?🎤
NB:
Kama kuna member unatamani kufahamu alifikaje JF waweza kumtag
Mshana Jr