DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,131
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mkuranga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega, amesema ujenzi wa viwanda unaoendelea wilayani Mkuranga tangu Rais Samia Suluhu Hassan aingie madarakani umeiongezea thamani na kwamba mambo matatu yakifanyika itapaa zaidi.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mgombea mwenza wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Ulega alisema sasa idadi ya wananchi wa Mkuranga imekuwa kubwa kwa sababu ya fursa zilizopo na hivyo wanaomba ipandishwe hadhi kuwa manispaa.
Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Wilaya ya Mkuranga ina jumla ya wakazi 533,033 – ikiwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu mkoani Pwani na ya kumi kitaifa.
“ Mheshimiwa mgombea mwenza, hapa Mkuranga baada ya mambo yaliyofanywa na serikali, fursa zimeongezeka na watu wamekuwa wengi. Tuna watu zaidi ya laki tano hapa na kama chama chetu kikipata ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu, tutaomba sana Mkuranga iwe Manispaa kamili,” alisema Ulega.
Ulega ambaye sasa anawania nafasi hiyo ya ubunge kwa muhula wa tatu, alisema wananchi wa Mkuranga watapiga kura za ndiyo kwa wingi kwa mgombea urais wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu ya mambo makubwa aliyowafanyia katika awamu yake ya kwanza ya uongozi iliyoanza Machi 2021.
Alisema Mkuranga sasa ina vituo vya afya na hospitali nyingi zaidi, ina shule nyingi zaidi za msingi na sekondari na ndiyo wilaya inayoongoza kwa kuwa na viwanda vingi kuliko wilaya nyingine yoyote nchini – huku vingine vikiwa vinapatikana Tanzania tu miongoni mwa nchi za ukanda huu wa Afrika.
Ulega alitumia pia nafasi hiyo kutoa shukrani kwa serikali kukubali upanuzi wa Barabara ya Kilwa kutoka Mbagala - Kongowe hadi Mkuranga – na akamwomba Nchimbi kuwa kama itawezekana, iwe ya njia nne ili kupunguza kero ya foleni katika barabara hiyo.
Na kwa sababu barabara hiyo pia ndiyo lango kuu la kuingia na kutoka mikoa ya Kusini, Ulega alimwambia Nchimbi kwamba Mkuranga wametoa eneo ambako serikali inaweza kujenga stendi kubwa kwa ajili yam abasi yanayoenda na kutoka Kusini.
“Mheshimiwa mgombea mwenza, barabara ya Kilwa ndiyo lango la kuingia na kutoka katika mikoa ya Kusini.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mgombea mwenza wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Ulega alisema sasa idadi ya wananchi wa Mkuranga imekuwa kubwa kwa sababu ya fursa zilizopo na hivyo wanaomba ipandishwe hadhi kuwa manispaa.
Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Wilaya ya Mkuranga ina jumla ya wakazi 533,033 – ikiwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu mkoani Pwani na ya kumi kitaifa.
“ Mheshimiwa mgombea mwenza, hapa Mkuranga baada ya mambo yaliyofanywa na serikali, fursa zimeongezeka na watu wamekuwa wengi. Tuna watu zaidi ya laki tano hapa na kama chama chetu kikipata ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka huu, tutaomba sana Mkuranga iwe Manispaa kamili,” alisema Ulega.
Ulega ambaye sasa anawania nafasi hiyo ya ubunge kwa muhula wa tatu, alisema wananchi wa Mkuranga watapiga kura za ndiyo kwa wingi kwa mgombea urais wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu ya mambo makubwa aliyowafanyia katika awamu yake ya kwanza ya uongozi iliyoanza Machi 2021.
Alisema Mkuranga sasa ina vituo vya afya na hospitali nyingi zaidi, ina shule nyingi zaidi za msingi na sekondari na ndiyo wilaya inayoongoza kwa kuwa na viwanda vingi kuliko wilaya nyingine yoyote nchini – huku vingine vikiwa vinapatikana Tanzania tu miongoni mwa nchi za ukanda huu wa Afrika.
Ulega alitumia pia nafasi hiyo kutoa shukrani kwa serikali kukubali upanuzi wa Barabara ya Kilwa kutoka Mbagala - Kongowe hadi Mkuranga – na akamwomba Nchimbi kuwa kama itawezekana, iwe ya njia nne ili kupunguza kero ya foleni katika barabara hiyo.
Na kwa sababu barabara hiyo pia ndiyo lango kuu la kuingia na kutoka mikoa ya Kusini, Ulega alimwambia Nchimbi kwamba Mkuranga wametoa eneo ambako serikali inaweza kujenga stendi kubwa kwa ajili yam abasi yanayoenda na kutoka Kusini.
“Mheshimiwa mgombea mwenza, barabara ya Kilwa ndiyo lango la kuingia na kutoka katika mikoa ya Kusini.