Jaya ni mateso makubwa sasa tunayopitia Watanzania! Tunaishi utadhani tupo kuzimu?
Ndugu Watanzania ninayo mengi sana kifuani kuwahusu wizara hii ya Nishati na uongozi wa awamu hii inayoshindwa kila kukicha, Nashindwa kuyaandika,
Kila nikiandika nafuta , nimeona niulize swali kwa Wizara! Ule umeme wa kabla ya Bwawa la Magufuli nao umekwenda wapi?
Inamaana hili Bwawa lisimgekuwa limeanza kuzalisha umeme sasa, nchi ingekuwa giza?
Juzi wazuri Wa Nishati alitwambia, mtambo uliokuwa umewashwa kwenye bwawa la Rufiji ulizimwa baada ya sjui maji hayakufunguliwa kwa wakati, na umeme ukaacha kuwaka utadhani kabla ya hapo hakukuwa na vyanzo vingine!
Ndiyo maana Magufuli alikuwa akiwatimua mbio wote wazembe! Mama anangoja nini kufukuza na kuteua upya tena?