KESSY FRANCIS
Member
- Nov 9, 2011
- 42
- 11
" Wenye ushawishi huko juu zingatieni haya, wana-CCM katika Bunge la Jamuhuri ni 75% ya wabunge wote. Ni HALALI yao kuwa hivyo maana walichaguliwa kwa kupigiwa kura mwaka 2010. Wakiungana na Baraza la Wawakilishi Zanzibar bado hawapungui 70%. Kuongeza wajumbe wa bunge la katiba 166 kutoka asasi za kiraia nje ya Bunge ni KUPUNGUZA nguvu ya CCM katika Bunge la katiba . Haina UHALALI wa kidemokrasia isipokuwa kuwafurahisha na kuwaridhia WAPINZANI, ambao wanataka idadi ya wabunge wa Bunge la katiba iongezwe mpaka CCM WASIWE NA WINGI, kisha Raisi aliyeomba kura nchi nzima ASITEUWE wabunge wa Bunge la katiba ila NGO's na asasi zingine za kiraia ndio WATEUWE kwa kuwa eti wao ndio Wawakilishi wa Wananchi. Ajabu hii ni kuwa asasi hizi hatujawai kuwapigia kura ya kuwa Viongozi a Watawala wetu!! Tunashangaa Wawakilishi wa watu waitwao MADIWANI wala hata hawaungumzwi. Tupende tusipende demokrasia yasema ni KIKWETE na wabunge wa CCM ndio walipata kura nyingi, na ndio wanahaki kuliko yeyote KUTUAMULIA mambo. Kama tunaona kura za 2010 ni za zamani mo, basi tufanye UCHAGUZI wa Bunge lote la katiba . Hiyo itakuwa ni demokrasia ya moja kwa moja. Lakini Hilo Lina gharama kubwa, basi TUKUBALI kuwa utawala wa CCM umependelea asasi zisizo za kiserikali, vyama pinzani kwa KUJIPUNGUZIA nguvu ya UWAKILISHI na kuongeza wajumbe 166 wa Bunge la katiba nje ya UWAKILISHI. Raisi wetu ni msikivu na mpenda amani, asililize sauti ya Wawakilishi wa kweli wa Wananchi na siyo wanaojipagingia, wanaojiapisha kuwa ni Wawakilishi wa wananchi pasipo kuchaguliwa." Profesa DAUDI MUKANGARA UDSM