Ninavyojua ni kwamba nchi yetu, TANZANIA ni nchi iliyotokana na muungano kati ya TANGANYIKA na ZANZIBAR na kuzaliwa kwa TANZANZANIA. Hivyo basi, serikali ya Tanzania ni serikali ya muungano na serikali ya muungano huwa ni moja na si mbili wala tatu. Kwa mtazamo wangu, kama wabunge wetu watapitisha serikali mbili au tatu jua kwa nchi yetu ni ya SHIRIKISHO na siyo MUUNGANO. Hivyo marekebisho inabidi yawepo hivi; JAMUHURI YA SHIRIKISHO YA TANZANIA na hii JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA haifai hapa bali nafasi yake ni kwenye dola moja tu si vinginevyo. Au wasemaje wataalamu wenzangu?