Ukweli ni upi baada ya kuoa au kuolewa

Ukweli ni upi baada ya kuoa au kuolewa

Bwana Mwiba. Maisha ni safari ndefu, maisha ya ndoa yana milima na mabonde, lazima utapanda na kushuka. Maisha ya uchumba kwa wengi wetu huwa yamejaa bashasha nyingi mno, hufanya watu wakafikiria kwa nini walichelewa kupata mchumba au rafiki wa jinsia tofauti. Kipindi cha uchumba kila mmoja huficha kabisa makucha yake ili yasije yakaharibu mahusiano. Ngoja mfunge ndoa na baada ya muda kupita, tabia halisi huanza kujitokeza. Mwanaume mlevi anaanza kuchelewa kurudi nyumbani tofauti na awali. Mnaanza kuonana wa kawaida tofauti na zamani, aliyeko nje unamuona mzuri kuliko mke wako au mume wako. Mungu aliyaona hayo akasema USITAMANI KITU CHA JIRANI YAKO, HATA MKE WAKE NA MTUMISHI WAKE, NA CHOCHOTE ALICHONACHO JIRANI YAKO. Baada ya mwaka mmoja mke amejifungua mtoto, asilimia 80 ya mapenzi ya mama yanahamishiwa kwa mtoto, wewe unabaki mpweke, unapomhitaji mkeo awe karibu na wewe, yeye anakuwa bize na mtoto. Ndio mwanzo wa kuanza kwenda chobizi. Mapenzi yanakwisha inabaki mazoea. Ndoa zina mambo mengi sana ila inategemeana na umahiri wenu, mume na mke mtakavyoweza kulinda ndoa yenu pasipo kutetereka. Usiogopeshwe na maneno ya wana jf. Ingia kwenye ndoa pasipo woga.
 
mambo ya kufunguliana milango kwenye gari huwa naona kwenye movie za wazungu kumbe bongo wapo wanaume wanaofungulia wanawake milango, hongera kaka, usifuatishe maneno ya huyo njemba alikuwa anakuonea wivu.
 
Fanya jambo ambalo unaweza kulifanikisha siku zote na si jambo la egoli. Ila kama ulimfungulia mlango basi huo mlango mbovu
 
Gari ni zima BMW 325i ,milango yote ni mizima na hayo maisha ya tamthilia ndio yepi mbona ni msemo mpya kwangu ?

Ni yale ya kuiga tunayoona wengine wanafanya yaani hatumaanishi kutoka moyoni wala hatujui umuhimu wala maana ya kufanya hivyo
 
Una uhakika ,maana alikuwa mmoja halafu nilimjibu mtu ! labda wanojua lugha hii ya kigeni watusaidie hapa naona kuna mvutano wa luga !

huo ni msemo.....unamwambia mwanamke/wanawake kuonyesha unajali au wewe ni gentleman....NI LADIES FIRST SIO LADY IS FIRST
 
Sometimes might be more than that if you get a right partner; na kama unajua unachokifanya hiyo itakuwa ni kawaida yako but kama unaiga utaacha soon baada ya kuoa, tusifanye vitu kwa kuiga;ikitoka moyoni inapendeza zaidi!
 
Bwana Mwiba. Maisha ni safari ndefu, maisha ya ndoa yana milima na mabonde, lazima utapanda na kushuka. Maisha ya uchumba kwa wengi wetu huwa yamejaa bashasha nyingi mno, hufanya watu wakafikiria kwa nini walichelewa kupata mchumba au rafiki wa jinsia tofauti. Kipindi cha uchumba kila mmoja huficha kabisa makucha yake ili yasije yakaharibu mahusiano. Ngoja mfunge ndoa na baada ya muda kupita, tabia halisi huanza kujitokeza. Mwanaume mlevi anaanza kuchelewa kurudi nyumbani tofauti na awali. Mnaanza kuonana wa kawaida tofauti na zamani, aliyeko nje unamuona mzuri kuliko mke wako au mume wako. Mungu aliyaona hayo akasema USITAMANI KITU CHA JIRANI YAKO, HATA MKE WAKE NA MTUMISHI WAKE, NA CHOCHOTE ALICHONACHO JIRANI YAKO. Baada ya mwaka mmoja mke amejifungua mtoto, asilimia 80 ya mapenzi ya mama yanahamishiwa kwa mtoto, wewe unabaki mpweke, unapomhitaji mkeo awe karibu na wewe, yeye anakuwa bize na mtoto. Ndio mwanzo wa kuanza kwenda chobizi. Mapenzi yanakwisha inabaki mazoea. Ndoa zina mambo mengi sana ila inategemeana na umahiri wenu, mume na mke mtakavyoweza kulinda ndoa yenu pasipo kutetereka. Usiogopeshwe na maneno ya wana jf. Ingia kwenye ndoa pasipo woga.

haswaaaaaaa; wewe ni mjanja.
 
ukweli mwingine ni ngumu kuuelewa kwa kuelezwa ila experince ndio itakupa majibu kwa iyo we oa tu!! swali lako nalifananisha na wale wanouliza eti nackia ukioa lazima itafika kipindi inabidi uwe na nyumba ndogo au u cheat! jibu la swali kama hilo utajijibu mwenyewe baada ya mda ukishaoa!!!
 
unataka kuwa msafi bila kuoga. Oga kwanza ndo ujue ladha ya usafi.
Utayajua ukishaingia ndoani mkuu.
Kwa sasa dont believe the hype
 
Back
Top Bottom