Ukweli ni Tanzania ni Mojawapo ya Nchi Zenye Sheria na Jeshi la Polisi Lenye Uonevu Sana Duniani

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
12,636
22,488
Ni kitu ambacho watu wengi hawakifikirii kwa makini, lakini ukweli ni wazi kwamba Tanzania ni mojawapo ya nchi zenye sheria na jeshi la Polisi lenye uonevu kwa raia zake duniani.

Hii ni kwa sababu, hapa Tanzania Polisi wanaweza kukutia ndani (arrest) kwa kosa ambalo halipo au la uzushi, au hata kubambikiwa na polisi, na kukupeleka makamani kisha wamwambie hakimu upelelezi bado unaendelea, na hakimu akakubaliana na Polisi. Matokeo ni kwamba unaweza kurudishwa rumande, na kukaa sana huko, wakati polisi wakiendelea na "upelelezi" - ili kupata uhakika (ushahidi) kama kweli ulitenda kosa.

Sasa matokeo ya upelelezi yanaweza kuwa hukutenda kosa, labda hata polisi wakagundua umesingiziwa, au hakimu akaitupilia kesi yako mbali kwa kuwa "haina mshiko" wakati ulishasota sana rumande. Huu ni uonevu wa hali ya juu.

Katika haki za msingi za binadamu, polisi hawapaswi kumkamata mtuhumiwa na huyo mtuhumiwa kunyimwa dhamana ikiwa upelelezi haujakamilika. Kwa hiyo ikiwa polisi watamwambia hakimu tunaomba kesi iahirishwe kwa kuwa upelelezi haujakamilika, basi hiyo inapaswa iwe sababu ya kumpa mtuhumiwa dhamana. Kwa nini umkamate (arrest) mtu bila kwanza kufanya upelelezi kama kweli ana kosa? Tuna sheria zinaruhusu Polisi wakamate (arrest) watu kwanza kwa kuhisi kisha ndio watafute kosa? Na kama hujakamilisha upelelezi mwachie kwa dhamana.

Lakini sijui kama wabunge, wanasheria, majaji na mahakimu wetu na hata Raisi wetu Magufuli analiona hili - au wanaliona lakini hawajali.
 
Jeshi letu la police ni mapokeo ya jeshi la askari wa kikoloni.

Huwezi kuwalaumu sana maana ni watu waliofunzwa kusema ndiyo Mzee hata kama hakuna sababu ya msingi.

Utawala kandamizi wa kikoloni ulichagua wazawa wasio na fikra nzuri kuwa askari ili wasije geuza interests zao.
 
Hilo linawezekana tu kwenye nchi zilizo endelea, ambapo wana investigation resources za higher technology ambapo pia raia wako proud and fearless kwenye kutoa taarifa za uharifu.

Lakini pia ita tegemea na mazingira wakati wa arrest au kabla ya arrest... mfano muhalifu au mshukiwa anaweza kutoroka, au ukubwa wa shitaka kama mauaji, ubakaji, uhaini, ujambazi wa kutumia siraha, madawa ya kulevya na makosa ya kisiasa. Vyote hivi huamua ni wakati gani arrest and dentetion ichukue mkondo.
Ina maana umemkamata mtu bila hata kuwa na huo ushahidi unaohisi utavurugwa. Ndio maana tunasema basi kusanya ushahidi wote kabla hujamkamata mtu.
 
Jeshi letu la police ni mapokeo ya jeshi la askari wa kikoloni.

Huwezi kuwalaumu sana maana ni watu waliofunzwa kusema ndiyo Mzee hata kama hakuna sababu ya msingi.

Utawala kandamizi wa kikoloni ulichagua wazawa wasio na fikra nzuri kuwa askari ili wasije geuza interests zao.

Kweli Mkuu. Nimeona wanahangaika kufungua matairi ya pikipiki na magari yaliyokamatwa eti Raisi alisema tufungue matairi. Nikajiuliza, sasa kama magari na pikipiki vimekamatwa na viko yadi ya polisi wakati wenye navyo wamefunguliwa kesi na ziko mahakamani, kwa nini mnapoteza muda kufungua matairi? Kwani wahitakiwa wakilishalipa faini si watarudishiwa vyombo vyao? Kwa nini kujipa kazi za ziada zisizo na pua wala mdomo - kufungua, kutunza matairi, kuwarudishia matairi wenye vyombo watakapolipa faini, kuhangaika kutafuta tairi za gari au pikipiki fulani, eeh! Au hayo matairi polisi watayauza ili kuongeza mapato ya serikali? Watayauza kwa kutumia sheria gani ikiwa tayari kesi iko mahakamani - adhabu mara mbili kwa kosa moja, moja ya polisi na myingine ya mahakama?

Yaani polisi wao wanakimbia kutekeleza tu bila kufikiri!
 
Hilo linawezekana tu kwenye nchi zilizo endelea, ambapo wana investigation resources za higher technology ambapo pia raia wako proud and fearless kwenye kutoa taarifa za uharifu.

Mkuu, yaani unasema ni sawa kwetu kukiuka haki za msingi za binadamu kwa kuwa hatujaendelea?
 
Kweli Mkuu. Nimeona wanahangaika kufungua matairi ya pikipiki na magari yaliyokamatwa eti Raisi alisema tufungue matairi. Nikajiuliza, sasa kama magari na pikipiki vimekamatwa na viko yadi ya polisi wakati wenye navyo wamefunguliwa kesi na ziko mahakamani, kwa nini mnapoteza muda kufungua matairi? Kwani wahitakiwa wakilishalipa faini si watarudishiwa vyombo vyao? Kwa nini kujipa kazi za ziada zisizo na pua wala mdomo - kufungua, kutunza matairi, kuwarudishia matairi wenye vyombo watakapolipa faini, kuhangaika kutafuta tairi za gari au pikipiki fulani, eeh! Au hayo matairi polisi watayauza ili kuongeza mapato ya serikali? Watayauza kwa kutumia sheria gani ikiwa tayari kesi iko mahakamani - adhabu mara mbili kwa kosa moja, moja ya polisi na myingine ya mahakama?

Yaani polisi wao wanakimbia kutekeleza tu bila kufikiri!
''Wanakimbilia kutekeleza bila kufikiri' umehitimisha vyema.

Polisi hawajiongezi kuchunguza sheria inasemaje juu ya kosa fulani. Matokeo yake ni kutekeleza kauli hata kama hazina maana.

Ni wakati polisi kuacha kuwa kama maroboti yanayopelekeshwa kwa remoti[matamko].
 
''Wanakimbilia kutekeleza bila kufikiri' umehitimisha vyema.

Polisi hawajiongezi kuchunguza sheria inasemaje juu ya kosa fulani. Matokeo yake ni kutekeleza kauli hata kama hazina maana.

Ni wakati polisi kuacha kuwa kama maroboti yanayopelekeshwa kwa remoti[matamko].

Mara nyingine nadhani maroboti ni nafuu kuliko askari wetu. Angalau yale maroboti ya kike ya Japan hayawezi kukuua kimakusudi badala ya kukuhudumia!
 
SHERIA LAZIMA ICHUKUE MKONDO WAKE KWA WAHALIFU. SHERIA NI MSUMENO
wewe utakuwa ni polisi........... ila polisi wetu hawa wanapenda rushwa wanashirikiana na majambazi na usipoangalia haki yako inaibwa pale mshtakiwa anapotoa pesa kisha anageuka mshtaki.............. kiukweli jeshi letu linatia kinyaa........
 
Kuna kamsemo ukipewa dhamana utaenda vuruga ushahidi.


Mkuu wangu kwa nchi za wenzetu mpaka unafika hata ya kukamatwa basi jua ushahidi wote umeshakamilika

Ila hapo kwetu mtuhumiwa anaweza kaa selo week nzima askari wakisema bado wanaendelea na uchunguzi..na Mwisho wa siku anaweza achiwa huru au inaweza pelekwa rumande akasota miaka kadhaa Mwisho ukasikia baada ya jalada kufika kwa DPP imeonekana hakuna ushaidi wa kumtia hatiani kwa hyo anaachiwa huru

Sasa kuna sababu gani ya kumkamata mtu na kumuweka sell wakati ushaidi haupo
 
Chadema ilishasema italivunja jeshi la polisi na kuliunda upya , vuteni subira .
 
Back
Top Bottom