Heinrich Himmler
Member
- May 20, 2013
- 71
- 151
Ndugu zangu watanzania, Baba wa Taifa hili mwalimu Nyerere alipoamua rasilimali za taifa hili zisichimbwe mpaka pale watanzania tutakapokuwa na weledi na uwezo wa kutosha katika kusimamia zoezi zima la exploitation ya natural resourses kuanzia uchimbaji, process za uongezaji wa thamani hadi kwenye masoko alijua kuwa hapo ndio tutaweza kunufaika. Kama baba wa taifa angekuwa na uchu wa kujinufaisha yeye na waliomzunguka, angeweza kufanya hivyo tena bila hata ya kelele za mtu yeyote maaan hata uelewa wetu ulikuwa mdogo sana, Tena wakati huo vitu vingi vilikuwa vinatolewa bure (siyo rushwa). Mwalimu angeweza hata kuamuru watu waunganishiwe umeme bure majumbani na isingeonekana kama ni rushwa ukilinganisha na ile rushwa waliyopewa watu wa Lindi na mtwara ya kuwaunganishia umeme kwa elfu 90.
Watanzania wenzangu na wana Lindi na mtwara, tusidanganyane, hakuna kufaidika na rasilimali za nchi kama wananchi hawatashiriki katika zoezi zima la uchimbaji. Nisiwafiche mimi nimefanyakazi mgodi wa north mara wa Barrick, Hakuna wananchi wanaozunguka mgodi wanaofaidika na ile dhahabu inayochimbwa pale, kwa sababu hakuna wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wanaoweza kuajirika katika migodi zaidi ya kazi ya ulinzi ambayo hata hiyo nayo makaburu wanaenda kuwachukua makaburu wenzao kutoka A/kusini. Kuna wakati mgodi wa North mara ulikuwa na makaburu walioajiriwa katika maeneo mbalimbali mgodini waliofikia zaidi ya mia tatu (300+). Mpaka walipokuja wakanada wenyewe ndio wakaamuru makaburu wapunguzwe.
Hii nchi ilipofikia saa hizi, bila resistance ya kutosha kama tunayoiona mtwara, rasilimali zote za nchi hii zitaisha bila kuwanufaisha majority ya wananchi wa Tanzania. Kwa hali ya watawala wetu walipofikia saa hizi, hawajali tena watanzania walio wengi katika kunufaika na rasilimali za nchi, wanachojali ni hizo kamisheni wanazozipata na kuzificha uswisi halafu wanawaacha wananchi waliowengi wakiwa kwenye lindi la umasikini. Mipango waliyopanga kuhusiana na gesi ya mnazibay hawajatekeleza wanarukia gesi ya mtwara. Kwa jinsi watawala wetu wanavyoamini katika rushwa wanafikia hadi kuwahonga wananchi wa Lindi na mtwara kwa kuwaunganishia umeme kwa punguzo la bei, wanawachukua wototo wawili watatu na kujifanya wanawasomesha ili wawalaghai wasilete upinzani. Mwisho wa siku kwenye hayo makampuni mtakuta wamejaa makaburu na watu kutoka nje ilivyo kwenye migodi (ambaye haamini hili atafute mtu yeyote aliyeko kwenye migodi ya barrik). Serikali ikilalamikiwa inasema watu wa immigration ndio wanaozembea (kwani immigration iko serikali ya Kenya?)
Kwa mtu yeyote ambaye hajatoka nje ya Tanzania kutembelea nchi nyingine za Afrika zenye mazingira sawa na yetu, anaweza asiamini kuwa tunaweza kufaidika . Mfano mzuri nenda Zambia, Zambia wamejiwekea sheria kuwa hakuna kampuni kutoka nje inayoenda kuwekeza bila kuwa na ubia na kampuni ya ndani. Na katika management lazima wazambia wawepo katika top management. Zambia ni sehemu ngumu sana kwa wageni kufanyakazi, matokeo yake ni kwamba wananchi ndio wanafaika wakubwa kuanzia mwananchi mmoja mmoja kwa ajira, kampuni za ndani katika kusupply bidhaa kwenye migodi, kampuni za ndani katika kupata tenda za migodini, kampuni za kuchimba za wazawa na serikali kupata mapato. Yaani ukienda Zambia ile multiplier effect ya migodi unaiona kwenye miji inayozunguka migodi. Kuna wakati Ndola ikifika mwisho wa mwezi migodini wamelipwa hela zao wafanyakazi na makampuni yanayosupply, ukienda kwenye maduka ya kubadilishia fedha, unaambiwa kwacha hakuna mpaka uende Lusaka. Ile dola ya migodini unaiona inafanyakitu kwenye miji yote inayozunguka migodi.
Bara bara zinazounganisha mikoa ni dual carriage way au sisi tunaita barabara mbili. Hapa Tanzania barabara kubwa kama morogoro road inayocollect magari yote ya mikoani na nchi za nje kuingia na kutoka dares salaam eti bado ni single lane, ndio maana inaongoza kwa ajari. Serikali inajua sababu za ajali ni kwamba madereva wanaovateki kwenye blackspot na sababu ni kwamba The whole segment of morogoro road is an accident blackspot, traffic volume ni kubwa kuwa handled na single lane. Morogoro road, gari moja bovubovu linaweza kuwapa mnyororo kuanzia kimara mpaka mizani ya kibaha, halafu effect ya jam ika-induce hadi barabara nyingine. Ila kwa sababu za kisiasa serikali inachofanya ni kujaza matraffic police kwaajili ya kuchukua rushwa na kuacha kudeal na core problem. Nimekaa Zambia karibu miezi 8 sijaona ajali za kijinga kama za bongo.
Turudi kwenye mada, Ukweli ni kuwa wananchi wa Lindi na Mtwara hawawezi kufaidika bila kwanza kujengewa shule ili watoto wao wengi waende shule, otherwise watakaofaidika na ajira ni watu wa mikoa mingine ambao walishaenda shule kabla yao. Pili wajasilia mali wazawa wa Lindi na Mtwara wawezeshwe kwa mitaji na utaalamu ili waweze ku-supply mahitaji ya uwekezaji kwa full capacity. Bila hivyo TUSIDANGANYANE mengine yatakuwa ni rushwa au kile alichokiita Tundu lisu ni kutongozea kura 2015. Na maandalizi hayo yanahitaji si chini ya miaka 10 at the very least. Kwa hiyo kama wanamtwara na lindi wameamua kupambana kutoka moyoni basi bottom line ni kwamba hiyo gesi isifanyiwe chochote hadi wao wapelekwe shule na maandalizi mengine ya kuwawezesha yafanyike, lakini kusema viwanda vijengwe huko mtwara siyo hoja maana vitajengwa na watabaki watazamaji tu sana sana vitawaharibia mazingira. Watakaoajiriwa ni makaburu na watu wachache kutoka sehemu nyingine za Tanzania. NAOMBA KUWASILISHA
Watanzania wenzangu na wana Lindi na mtwara, tusidanganyane, hakuna kufaidika na rasilimali za nchi kama wananchi hawatashiriki katika zoezi zima la uchimbaji. Nisiwafiche mimi nimefanyakazi mgodi wa north mara wa Barrick, Hakuna wananchi wanaozunguka mgodi wanaofaidika na ile dhahabu inayochimbwa pale, kwa sababu hakuna wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wanaoweza kuajirika katika migodi zaidi ya kazi ya ulinzi ambayo hata hiyo nayo makaburu wanaenda kuwachukua makaburu wenzao kutoka A/kusini. Kuna wakati mgodi wa North mara ulikuwa na makaburu walioajiriwa katika maeneo mbalimbali mgodini waliofikia zaidi ya mia tatu (300+). Mpaka walipokuja wakanada wenyewe ndio wakaamuru makaburu wapunguzwe.
Hii nchi ilipofikia saa hizi, bila resistance ya kutosha kama tunayoiona mtwara, rasilimali zote za nchi hii zitaisha bila kuwanufaisha majority ya wananchi wa Tanzania. Kwa hali ya watawala wetu walipofikia saa hizi, hawajali tena watanzania walio wengi katika kunufaika na rasilimali za nchi, wanachojali ni hizo kamisheni wanazozipata na kuzificha uswisi halafu wanawaacha wananchi waliowengi wakiwa kwenye lindi la umasikini. Mipango waliyopanga kuhusiana na gesi ya mnazibay hawajatekeleza wanarukia gesi ya mtwara. Kwa jinsi watawala wetu wanavyoamini katika rushwa wanafikia hadi kuwahonga wananchi wa Lindi na mtwara kwa kuwaunganishia umeme kwa punguzo la bei, wanawachukua wototo wawili watatu na kujifanya wanawasomesha ili wawalaghai wasilete upinzani. Mwisho wa siku kwenye hayo makampuni mtakuta wamejaa makaburu na watu kutoka nje ilivyo kwenye migodi (ambaye haamini hili atafute mtu yeyote aliyeko kwenye migodi ya barrik). Serikali ikilalamikiwa inasema watu wa immigration ndio wanaozembea (kwani immigration iko serikali ya Kenya?)
Kwa mtu yeyote ambaye hajatoka nje ya Tanzania kutembelea nchi nyingine za Afrika zenye mazingira sawa na yetu, anaweza asiamini kuwa tunaweza kufaidika . Mfano mzuri nenda Zambia, Zambia wamejiwekea sheria kuwa hakuna kampuni kutoka nje inayoenda kuwekeza bila kuwa na ubia na kampuni ya ndani. Na katika management lazima wazambia wawepo katika top management. Zambia ni sehemu ngumu sana kwa wageni kufanyakazi, matokeo yake ni kwamba wananchi ndio wanafaika wakubwa kuanzia mwananchi mmoja mmoja kwa ajira, kampuni za ndani katika kusupply bidhaa kwenye migodi, kampuni za ndani katika kupata tenda za migodini, kampuni za kuchimba za wazawa na serikali kupata mapato. Yaani ukienda Zambia ile multiplier effect ya migodi unaiona kwenye miji inayozunguka migodi. Kuna wakati Ndola ikifika mwisho wa mwezi migodini wamelipwa hela zao wafanyakazi na makampuni yanayosupply, ukienda kwenye maduka ya kubadilishia fedha, unaambiwa kwacha hakuna mpaka uende Lusaka. Ile dola ya migodini unaiona inafanyakitu kwenye miji yote inayozunguka migodi.
Bara bara zinazounganisha mikoa ni dual carriage way au sisi tunaita barabara mbili. Hapa Tanzania barabara kubwa kama morogoro road inayocollect magari yote ya mikoani na nchi za nje kuingia na kutoka dares salaam eti bado ni single lane, ndio maana inaongoza kwa ajari. Serikali inajua sababu za ajali ni kwamba madereva wanaovateki kwenye blackspot na sababu ni kwamba The whole segment of morogoro road is an accident blackspot, traffic volume ni kubwa kuwa handled na single lane. Morogoro road, gari moja bovubovu linaweza kuwapa mnyororo kuanzia kimara mpaka mizani ya kibaha, halafu effect ya jam ika-induce hadi barabara nyingine. Ila kwa sababu za kisiasa serikali inachofanya ni kujaza matraffic police kwaajili ya kuchukua rushwa na kuacha kudeal na core problem. Nimekaa Zambia karibu miezi 8 sijaona ajali za kijinga kama za bongo.
Turudi kwenye mada, Ukweli ni kuwa wananchi wa Lindi na Mtwara hawawezi kufaidika bila kwanza kujengewa shule ili watoto wao wengi waende shule, otherwise watakaofaidika na ajira ni watu wa mikoa mingine ambao walishaenda shule kabla yao. Pili wajasilia mali wazawa wa Lindi na Mtwara wawezeshwe kwa mitaji na utaalamu ili waweze ku-supply mahitaji ya uwekezaji kwa full capacity. Bila hivyo TUSIDANGANYANE mengine yatakuwa ni rushwa au kile alichokiita Tundu lisu ni kutongozea kura 2015. Na maandalizi hayo yanahitaji si chini ya miaka 10 at the very least. Kwa hiyo kama wanamtwara na lindi wameamua kupambana kutoka moyoni basi bottom line ni kwamba hiyo gesi isifanyiwe chochote hadi wao wapelekwe shule na maandalizi mengine ya kuwawezesha yafanyike, lakini kusema viwanda vijengwe huko mtwara siyo hoja maana vitajengwa na watabaki watazamaji tu sana sana vitawaharibia mazingira. Watakaoajiriwa ni makaburu na watu wachache kutoka sehemu nyingine za Tanzania. NAOMBA KUWASILISHA