Ukweli kuhusu unga airport.

Ukweli kuhusu unga airport.

Kwa hiyo hizo kilo 150 wanazodai zimekamatwa S.A hapo JNIA hamkuziona?????!!! Are you kidding me??!!!


Je kuna uhakika kuwa hayo madawa yalipita hapo airport..????? au kwa vile mhusika anatoka Tanzania. je kama dili lilianzia nchi zingine yeye Masogange ni mtekelezaji wa hayo madawa huko S.A
 
hujamsoma, kasema wanawajibika kuripoti ikiwa wataona mzigo kama huo. Sasa hapa swali ni je hawakuziona zile 150k??!! Soma vizuri hapa

hayo mengineyo kama madawa,pembe za ndovu,utoroshaji wa fedha etc ni ya ziada na hushughulikiwa endapo watayaona na kama hawatayaona basi hawapaswi kuhukumiwa.


hicho ndicho alichoandika huyo bwana. Kwa hiyo swali langu liko pale pale hizo 150k hawakuziona???!!!

mbona ukumalizia kunukuu?nilisema endapo itabainika pasi na shaka kuwa maafisa hao wanatiwa hatiani endapo ikithibitika pasi na shaka kuwa;
1.walikuwa na taarifa kuhusu contraband
2.waliziona na kuziacha kwa makusudi
3.walisaidia kuzipitisha.
Sehemu gani ambayo hukuelewa au ni kimbelembele tu cha kubwabwaja?
 
je kuna uhakika kuwa hayo madawa yalipita hapo airport..????? Au kwa vile mhusika anatoka tanzania. Je kama dili lilianzia nchi zingine yeye masogange ni mtekelezaji wa hayo madawa huko s.a

nisaidie kumuelimisha mkuu,watu wengine badala ya kufikiri huwa wanakalia kulaumu.kwani nani amethibitisha kuwa mzigo huo ulipitia jnia?je kama masogange alikutana nao o.tambo airport ndio akawa anautoa je?
 
Suala hapa si idara ya uhamiaji bali ni ukweli kuwa kipo kitengo kinachohusika name ukaguzi. wa mizigo ya abiria. Mfano mdogo tu, ni kwa vipi basi isiwezekane kupita na mafuta ya kupakaa unapo board ndege?
 
vyovyote uelezeavyo hapo airport lazima mlaumiwe maana hao askari maalum si wapo hapo tena na mbwa? Au hao mbwa wanakuwa washalewa madawa ya kulevya washindwe kunusa mizigo??
Btw, hiyo hatua namba 2 kweli hamuwezi kujiuliza ni mzigo wa aina gani mwingi hivyo?? Au kuna staff alipita nao pembeni kama wa kwake kwa kucheza dili na kuepuka utaratibu wa security screening?

mfano,afisa uhamiaji akimruhusu mtu asiyekuwa na viza kuingia nchini utaenda kumlaumu mu wa tra?au mtu akikwepa kulipia ushuru wa bidhaa zake utaenda kumlaumu uhamiaji?nina maana kila mtu awajibike kwa misingi ya kazi yake.airport wapo wafanyakazi wengi sana lakini sio wote wanaofanya kazi ya aina moja.kila mtu anasimamia ya kwake.uhamiaji atafanya ya uhamiaji tu,tra hivyo hivyo,polisi hivyo hivyo etc etc....usimbebeshe mtu lawama zisizo mstahili.
 
Ili kukatisha hadithi

1. Maelezo ya utaratibu yanakaribia sana na taratibu ila hujajikita kwenye maudhui.

2. Misingi ya hizo taratibu ni usalama kama ulivyosema. Swali la kuanzia hoja ni je madawa miminika na unga hayakatazwi? Jibu viwanja vingi serious vinadhibiti. Kwa nini vipitie kiwanja chetu na kuingia kwenye ndege? Jibu ni kuwa kuna udhibiti mbovu tena kwa makusudi.

3. Inakuwaje viwanja vingine vinakamata madawa haya km SA, Hong Kong? Wao pia wanatumia Annex ya ICAO hiyo hiyo. Ina maana ndogo tu; tafisiri ya hiyo Annex inafanywa na mburula au kuna msukumo wa kimaslahi.

4. Kurukia "hukumu" unayoilalamikia ni utetezi wa kitoto. "Facts on the ground" ni kuwa madawa yamepitia hapo kiwanjani yamekamatwa kwenye kiwanja kingine kinachoongozwa na sheria na kanuni zile zile. Lazimja kuna mapungufu ya udhibhiti na hususan kuna mtu au watu hawakutimiza majukumu yao au kwa uzembe/udhaifu au kwa makusudi. Nachelea kuamini wewe ni mmoja wapo.

5. Uongozi/utawala wa viwanja vyetu wameshindwa wamekuwa dhaifu wa kusimamia "usalama" hadi kadhia hii inajitokeza. Na hili linakwenda mbali zaidi kitaifa kwa .maana UDHIBITI ni kitu hakitakiwi na serikali dhaifu kwa malengo ya kuendelea kufanya maovu yao. Hapa namaanisha kutoka juu hadi chini (Kwa kujificha kwenye kumlaumu mnyonge).

6. Kama taifa tumekuwa "tainted" vibaya na mwenendo na kadhia hii na unajua inawezekana hujali kama watawala wako. Lakini ile hulka ya kutokujali na kujipendekeza tunajishushia heshima kimataifa kana kwamba tunajitosheleeza na tunaweza kuishi bila wengine. "Victims" ni sisi wengine innocent wenye shughuli zetu zinazotuunganisha na mataifa mengine. HAIKUBALI8KI.
 
................................................................NASISITIZA TENA,MAJUKUMU YA MSINGI YA HAWA WAKAGUZI WA AIRPORT NDIYO HAYO NILIYOYATAJA NA HAYO MENGINEYO KAMA MADAWA,PEMBE ZA NDOVU,UTOROSHAJI WA FEDHA ETC NI YA ZIADA NA HUSHUGHULIKIWA ENDAPO WATAYAONA NA KAMA HAWATAYAONA BASI HAWAPASWI KUHUKUMIWA.MAAFISA HAWA WATAHUKUMIWA ENDAPO ITATHIBITIKA PASI NA SHAKA KUWA WALIKUWA NA TAARIFA KUHUSU CONTRABAND HIZO AU WALIZIONA WAKAZIACHA AU WALISAIDIA KUZIPITISHA KWA MAKUSUD
........................................................................................................



Join Date : 4th August 2013
Posts : 4
Rep Power : 0
Likes Received: 2
Likes Given: 0
 
ni kweli lakini 15kg ...hukuziona kwa kuwa sio shughuli yako...kweli !?

mnatakiwa wote mrejeshwe JKT mkafunzwe Uzalendo
 
International Drug Dealers, hata wakiwa "well organized " wanaweza wasifanikiwe kutekeleza Malengo yao endapo tu, watumishi wa Idara, taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi, wanaofanya kazi Airport na kwingineko, watakuwa na uhusiano na ushirikiano mzuri, ikiwemo na nia ya dhati ya kukomesha biashara hiyo haramu!
 
Ushauri wangu:
Turejee kwenye maadili mema kama watanzania, Tuwe wazalendo na nchi yetu na jamii ya mtanzania, tuepuke tamaa za utajiri wa haraka usiokuwa na misingi bora, tuepukane na ubinafsi wakutojali maslahi ya jamii including kuukemea ubinafsi hatari kabisa dhidi ya afya ya kizazi cha mtanzania..
halafu baada ya hapo tu invest katika Skills and Professionalism kwa watendaji wetu hususan katika public sectors (that is with direct access to the general public and public resources) kisha tufanye investment katika teknolojia na vifaa vya kisasa vinavyoweza kutupa taarifa sahihi zenye muunganiko wa matukio kwa wakati.. na mwisho tuboreshe maslahi ya watumishi hao wa umma kama additional incentive...
Kwa pamoja muunganiko wa nilivyoviainisha hapo juu vitajenga taifa lenye watu wenye kujali, kuheshimu na kuupenda Utaifa wao, pia Taifa litakuwa limejitengenezea hazina na watu waliopevuka kimaadili mema, wasiokuwa na tamaa mbaya na wenye kukemea mambo au maisha ya hovyo hovyo yenye kujenga maadili maovu.. with that being in place hatimaye Taifa litaweza kupiga na kushinda vita dhidi ya Madawa ya kulevya.. (it needs to be dealt from the root cause, & that is from the moral of the society at large...) i am just trying to think loudly...
 
Ha ha ha! Wakomeshe madawa? Msijidanganye! Mitandao yao hao jamaa aisee! Bora ninyamaze nisijekupotezwa
 
Maelezo mazuri hayo mdau binafsi nimekuelewa but kuna mazingira mzigo ukiwa mkubwa sana kiukweli hata kama hujabobea kwenye hayo mambo ikitokea umepita huo mzigo unahitaji kuhojiwa. Procedure zote ulizozieleza ni sawa lakini bado wale maofisa wa usalama wanaokaa kwenye scanner hata kama kuna baadhi ya vitu hawahusiki navyo but kwa uzoefu wanaweza wakaona kitu ambacho si cha kawaida kipo kwenye mzigo wa abiria especially kilo zote hizo na ndio maana ukishakaguliwa na afisa usalama wa kwanza pale nje ukiingia tu pale kwenye scanner kwa pembeni huwa kuna meza hivyo pindi anapoona kuna kitu ambacho hakielewi elewi anakuambia weka begi pembeni tena unalifungua mwenyewe na kuanza kukuonyesha sehemu ambayo amekiona hicho kitu kwenye scanner na kukikagua na kukuruhusu. Sasa sembe yote ile hata kama jamaa hawahusiki isionekane kiurahisi wakati kuna vitu kama mkasi, box labda la camera umeamua kuliweka kwenye sanduku linaonekana, kilo chache sawa maana hata huko wanakokamata sio kwamba wao ni wataalamu sana kinachofanyika wakati mwingine kufanya sampling na kufanya ukaguzi wa kina na si kwamba hakuna wasiopita na madawa
 
Inabidi JNAI

1.Walete scanner mpya za kisasa kama wanazotumia wenzetu ughaibuni.

2.Vinywaji moto kama kahawa/chai vilazimishwe kutumika kama sehemu ya
uchunguzi wa awali.

3.Kama itawezekana kitaalamu pawepo na scanner maalum itakayo-detect
na kuonesha upande wa pili kilichoko ndani ya mwili wa binadamu.

Hii itasaidia sana kwani baadhi ya scanner uwa zina detect vitu venye
asili ya chuma kuliko vitu kama plastic,mbao n.k

Anyway sio mtaalamu sana wa mambo haya,ila najaribu kuwakilisha kile ninachofikiri
kama suluhisho.
 
mbona ukumalizia kunukuu?nilisema endapo itabainika pasi na shaka kuwa maafisa hao wanatiwa hatiani endapo ikithibitika pasi na shaka kuwa;
1.walikuwa na taarifa kuhusu contraband
2.waliziona na kuziacha kwa makusudi
3.walisaidia kuzipitisha.
Sehemu gani ambayo hukuelewa au ni kimbelembele tu cha kubwabwaja?

Kuwa na adabu wewe kilaza, unadhani hatujui uozo ulioko hapo JNIA? Kwa taarifa yako tuna taarifa za uozo unaoendelea hapo na tunawafanyia kazi, kama umetumwa kuja kujisafisha humu, kazi bado unayo. Usione hatusemi ukadhani tu wajinga sana ebo!
 
Hii biashara ni chain ndefu sana, bahati nzuri mara nyingi nimmekuwa naenda Airport za TZ hasa nyakati za usiku. Huwa najiuliza maswali mengi sana bila majibu, maana mazingira yalivyo ni rahisi sana mtu apite na mzigo wa aina yoyote ambao ni haramu. Uhamiaji na wenyewe wanahusika kuruhusu uingiaji wa ''dealers'' wa madawa kutoka nje, hawa wanafanya kazi ya kurekebisha pass zao faster hasa kwenye swala la uraia.

Anyway,umejitahidi kuelezea ila naona kama umekataa kusema uhamiaji wanahusika.
sirari namanga
 
Back
Top Bottom