Ukweli kuhusu laana (Curse)

mkuu vitu vingine sio vya hadithi za sungura na fisi.hii kitu acha kbsa ndugu na iogope.usitegemee ukiwa na laana unajijua sahau hyo watu ndo wanajua ww umelaanika
 
subir ulaaniwe ndio utajua laana ipo.na uzr ukipata laana ww km ww huwezi kujijua ila wengine.hii ipo kiimani na nikwl ipo
Mkuu achana na hiyo imani, itakutesa sana. Ndiyo hii "fear of the unknown". Utatambika sana kwenye makabuli ya mababu zako kwa lengo hili la kuondoa "laana". Na kila utakapofeli kimkakati akili yako itakuelekeza kwenye "laana". Umeshindwa kulipa deni wanataka kuuza nyumba akili itakutuma kutambika kwenye kaburi la baba, mjomba, shangazi, mama, bibi, nk. Ili laana itoke wasiuze nyumba yako! Achana na hiyo dhana.!
 
mkuu vitu vingine sio vya hadithi za sungura na fisi.hii kitu acha kbsa ndugu na iogope.usitegemee ukiwa na laana unajijua sahau hyo watu ndo wanajua ww umelaanika
Wao wanajuaje kama nimepata laanawanakipimo cha laana?
ulimwona mtu kalaniwa?
je iyo laana uwa inampataje muhusika kutoka kwa mtoa laana na anayelaniwa?
je unajua kutoa laana?
Ulimpa laana nani?
Maneno yapi unatumia kutoa laana?
Inachukua siku ngapi laana kumpata muhusika?
Naomba leo unipe laana nitoe ushuhuda jf.

Sipendagi ujinga mimi...
 
umeanza kufafanua vizuri ila mwishoni umeharibu kwa sababu umejitungia swali lako na kujijibu, maana yake uko nje ya maada! sijasema popote pale kwenye huu uzi kwamba ati sayansi ni dini wala dhehebu, leta mchango mkuu
 
tehetehe
taratibu mkuu
 
watu wakishiba ugali wana matatizo sana, eti hakuna laana! nyie mnaishi jamii ipi? acheni kujifanya hamjui haya mambo, tumieni akili ya kawaida sio sigara bwege
Punguza jaziba ili busara zipate nafasi! Hebu tusaidie: umewahi kukutana na mtu aliyealaaniwa? Yukoje? Au nini kilikutuma kuona kuwa huyu ni mtu aliyelaaniwa?! Si kweli kwamba mpaka mtu anayemfahamu alipokwambia kuwa huyo unayemuona amelaaniwa ndipo nawewe akili yako ikaelekea huko?
 
Laana na Baraka zipo na sio suala la kufikirika kama wengine wanavyosema humu. Hebu tuanzie na vitabu vitakatifu tuone namna Baraka na laana zilivyo.
  1. Someni ktk biblia kitabu cha mwanzo laana aliyotoa Mungu kwa 'nyoka', Hawa na Adamu baada ya uovu wa kwanza.
  2. Someni pia kitabu hicho hicho laana ya Mungu kwa Kaini baada ya kumuua nduguye Abeli
  3. Someni Baraka kwa watoto wa Ibrahim Isihaka na Ishmael.
  4. Someni Baraka na laana za Nuhu (kama sikosei) kwa wanae kwa aliyemcheka na wale waliomfunika akiwa amelewa.
  5. Someni Baraka za Israel (Yakobo) kwa wanawe
Ni Mengi ya kusoma ila LAANA na BARAKA zipo, mfano hai zaidi ni Amri ya 4 Ya Mungu ;waheshimu baba na mama upate heri na miaka mingi duniani. hebu angalieni wale ambao waliheshimu wazazi DHIDI ya wale waliowadharau upate mifano.
 
Hakuna kitu kama hicho.Ni suala la kisaikolojia tu. Linamuathiri yule anayeliamini.
Laana ipo mzee kama unabisha jaribu uone.Laana ni adhabu apeyo mtu baada ya kudhulumu nafsi ya mwenzie yaani kumfanyia ubaya au kumkosea Allah.

Kuna laana itokayo moja kwa moja kwa Allah kama vile laana aliyopewa ibilisi na kuna laana ambayo unakuta mja fulani amemdhulumu mja mwenzake,sasa yule aliyedhulumiwa akamshitakia Mola na kumkabidhi Mola amfanye lolote yule aliyedhulumu.

Na sio laana atakayoomba binadamu imfikie mtu fulani itamfikia lazima iwe ya kweli na huyo awe kweli amedhulumu(amekufanyia jambo baya) la sivyo inakurudia mwenyewe.

Kutokana na uwepo wa jambo hilo yaani laana na jinsi lilivyokuwa zito tumehimizwa sana tujizuie kupeana laana.

Dawa ya laana ni mtu kufanya toba na kukiri makosa yake na anatakiwa kwanza kurudi kwa yule aliyemkosea kama anamjua kisha amtake Mola msamaha na Mola ni mwingi wa kusamehe.

Halafu tuwe na desturi ya kuuliza kama kitu hukijui mzee.
 
Nani amekwambia laana inatoka kwa baba na mama au watu wa karibu tu ?
 
Kiongozi umewahi kukutana barabarani au mtaani na mtu aliyelaaniwa?! Ulimtambuaje?!
 
Hakuna kitu kama hicho ni Upuuzi uliopitiliza.Laana ndio nini huyo aliokulaani yeye hajakosea watu
 
Kiongozi umewahi kukutana barabarani au mtaani na mtu aliyelaaniwa?! Ulimtambuaje?!
Sasa mbona unachanganya mada mzee ? Suala ni uwepo wa laana au mpaka nimuone ? Kwa akili ya kawaida mwenyewe jijibu mzee.Sasa utamtambuaje ? Kwa macho huwezi kumtambua suali ni sawa sawa na kuuliza je unaweza kumjua mwanamke aliyeachika kwa kumtazama ? Jibu ni huwezi.

Haya,unataka kusema nini baada ya hapo ?
 
Niliwahi kushuhudia....tukio la kijana akimtwanga mangumi mama yake mzazi...na kumdhalilisha vibaya sana......mbele ya kadamnasi....

Yule mama kuna maneno aliyoyaongea ambayo sikuwa nayatilia maanani lakini baada ya muda tukaja kuona maana yake na madhara yake.....

Namnukuu...

" Wewe Charles( sio jina halisi) kama hujawahi kunyonya ziwa hili ( huku akionyesha ziwa lake) na kama hujakaa tumboni hapa( huku akionyesha tumbo lake)..........tutaona yatakayo kupata......

Baada ya muda kidogo
yule bwana maisha yake yalibadilika haraka sana.......aliacha kazi yeye mwenyewe kwa hiyari yake.....akaanza kuvaa nguo za mkewe....na matukio mengine yakiyotuwacha mdomo wazi......

Mpaka ninavyoandika hapa yule jamaa ni kichaa kabisaa....tena huwa namuonaga hata pale maeneo ya jangwani.....hata tukipishana hanifahamu tena.......

Haya mambo sio ya mchezo....kabisa.....
 
Maana yangu ni kwamba ili umuone mtu kuwa kalaaniwa, ni lazima watu waseme ndipo nawewe akili yako ielekee huko. Kwani nikilaaniwa napatwa na nini specifically?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…