Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,555
- 41,064
Kwa namna Tanzania ilivyo na jinsi Watanzania tulivyo, lazima uwe na akili ndogo sana au uwe huna kabisa, ndiyo unaweza kuamini kuwa nchi hii kuna siku itakuja kuendelea kwa kutegemea jinsi tunavyoenda.
Karibia wakati wote, kwa kiasi fulani ukiondoa kipindi cha awamu ya kwanza, wakati mwingine wote, Watanzania wamekuwa katika laana ya kuongozwa na watu majizi, wazembe wasio na huruma kwa wananchi na Taifa kwa ujumla. Ofisi nyingi za umma zimejaa majizi, wafuja pesa, wazembe na uwezo duni wa kiutendaji.
Kila mwaka report ya CAG inakuja na madudu yale yale, wakati wote ni mabilioni na matrilioni yaliyopotea. Safari hii mpaka mamia ya magari yaliyonunuliwa hayaeleweki yameenda wapi.
Ndiyo maana haya majitu hata wakati wa uchaguzi yapo tayari kuiba kura, kuhonga, kupora ushindi wa waliochaguliwa na wananchi ili wapate nafasi ya kwenda kukomba mabilioni wa Watanzania makondoo na wajinga.
Hakuna mtu anayeweza kuiba kura na kuhonga wapiga kura kwa sababu ana uchungu wa kutaka kwenda kuwahudumia wananchi. Wanaiba kura, wanapora ushindi, wengine wanaenda mpaka kuwanga, ili tu wapate mwanya utakaowapeleka kwenda kuiba pesa ya umma.
Uchafu unaotendwa na watendaji wa Serikali kila mwaka, ingekuwa ni nchi ya watu wenye akili timamu wanaojitambua, hakika lazima kuna kitu kingetendeka dhidi ya Serikali.
Ndugu zangu, hata ukianzisha mradi wowote, mafanikio huwa yanategemea zaidi maeneo mawili:
Moja, ni uzalishaji. Hii ndiyo itakayoamua mapato (revenue) utakayoyapa.
Sehemu ya pili ni matumizi.
Mradi wako unaweza kufanikiwa kwa kuhakikisha unaongeza uzalishaji, matumizi yakabakia constant. Au unaweza kubakiza uzalishaji ule ule lakini ukapunguza matumizi.
Ukitaka kufanikiwa zaidi, unaweza kuongeza uzalishaji na pia ukapunguza matumizi wakati mmoja.
Ukweli ni kwamɓa hata ukizalisha kiasi gani, na mapato yakaongezeka, lakini matumizi yakawa nayo yanapaa, mradi wako hauwezi kufanikiwa, na wewe utabakia maskini daima.
Kwa Tanzania, hatuwezi kupata mafanikio yoyote kwa sababu wakati tunahangaika kuongeza mapato, tena kwa kuwakamua hasa wananchi maskini, haya majizi yaliyomo kwenye ofisi za Serikali, yenyewe yanajitahidi kuongeza kufuja na kuiba pesa za umma maradufu.
Lakini haya yote yanatokea kwa sababu ya ujinga wa sisi wananchi. Yanaiba kura, sisi tupo kimya, yanaiba pesa, tupo kimya. Kwa nini yasiongeze kuiba!!
Hivi kama tumeshindwa japo kuandamana kudai tuoneshwe kwa majina, hayo majizi ili tukayakokote kuyaondoa ofisini, kwa nini hata tusigome wote kwa pamoja kulipa kodi mpaka tutakapokuwa na uhakika kodi zetu zinatumika vizuri?
Kwa hali ya wizi, rushwa na uzembe wa watendaji wa Serikali ya Tanzania, kwa kweli si halali kabisa kulipa kodi. Wajibu hauwezi kukaa upande mmoja. Yaani mwananchi alipe kodi, lakini mkusanyaji atapanye kodi kwa anasa na wizi. Hii haikubaliki. Kama anayekusanya hana uwezo wa kuitunza hela inayokusanywa ikawa salama, basi asikusanye mpaka siku atakapokuwa na uwezo wa kuilinda na kuitumia vizuri na kwa umakini kwa manufaa ya walipa kodi.
Kama tusingekuwa na majitu majizi kwenye ofisi za Serikali na taasisi zake, ingewezekana vipi shirika kama TANESCO, lisilo na mshindani, linalopewa mpaka na ruzuku na Serikali, lingeweza kupata hasara?
Ni mradi gani wa Serikali au CCM uliwahi kufanikiwa? TBL walifeli, TANESCO wamefeli, viwanda vya bidhaa mbalimbali walifeli, SUKITA ya CCM ilifeli, Shule za wazazi za CCM zilifeli, maduka ya TRC yalifeli, ATCL wamefeli, TTCL wamefeli, kila kitu wamefeli. Hata reli watafeli tu. Kwa sababu hawa watu hakuna wanachofikiria zaidi ya kuiba
Ukweli ni kwamba kila inapowezekana kukwepa kulipa kodi ni aheri kufanya hivyo. Maana hata ukilipa, kuna majitu yanaenda kuichezea pesa yako wakati wewe umejibana, umeiacha familia yako ikijibana na kuteseka, lakini huko kuna mijitu inaenda kuichezea pesa yako kama haina mwenyewe.
Karibia wakati wote, kwa kiasi fulani ukiondoa kipindi cha awamu ya kwanza, wakati mwingine wote, Watanzania wamekuwa katika laana ya kuongozwa na watu majizi, wazembe wasio na huruma kwa wananchi na Taifa kwa ujumla. Ofisi nyingi za umma zimejaa majizi, wafuja pesa, wazembe na uwezo duni wa kiutendaji.
Kila mwaka report ya CAG inakuja na madudu yale yale, wakati wote ni mabilioni na matrilioni yaliyopotea. Safari hii mpaka mamia ya magari yaliyonunuliwa hayaeleweki yameenda wapi.
Ndiyo maana haya majitu hata wakati wa uchaguzi yapo tayari kuiba kura, kuhonga, kupora ushindi wa waliochaguliwa na wananchi ili wapate nafasi ya kwenda kukomba mabilioni wa Watanzania makondoo na wajinga.
Hakuna mtu anayeweza kuiba kura na kuhonga wapiga kura kwa sababu ana uchungu wa kutaka kwenda kuwahudumia wananchi. Wanaiba kura, wanapora ushindi, wengine wanaenda mpaka kuwanga, ili tu wapate mwanya utakaowapeleka kwenda kuiba pesa ya umma.
Uchafu unaotendwa na watendaji wa Serikali kila mwaka, ingekuwa ni nchi ya watu wenye akili timamu wanaojitambua, hakika lazima kuna kitu kingetendeka dhidi ya Serikali.
Ndugu zangu, hata ukianzisha mradi wowote, mafanikio huwa yanategemea zaidi maeneo mawili:
Moja, ni uzalishaji. Hii ndiyo itakayoamua mapato (revenue) utakayoyapa.
Sehemu ya pili ni matumizi.
Mradi wako unaweza kufanikiwa kwa kuhakikisha unaongeza uzalishaji, matumizi yakabakia constant. Au unaweza kubakiza uzalishaji ule ule lakini ukapunguza matumizi.
Ukitaka kufanikiwa zaidi, unaweza kuongeza uzalishaji na pia ukapunguza matumizi wakati mmoja.
Ukweli ni kwamɓa hata ukizalisha kiasi gani, na mapato yakaongezeka, lakini matumizi yakawa nayo yanapaa, mradi wako hauwezi kufanikiwa, na wewe utabakia maskini daima.
Kwa Tanzania, hatuwezi kupata mafanikio yoyote kwa sababu wakati tunahangaika kuongeza mapato, tena kwa kuwakamua hasa wananchi maskini, haya majizi yaliyomo kwenye ofisi za Serikali, yenyewe yanajitahidi kuongeza kufuja na kuiba pesa za umma maradufu.
Lakini haya yote yanatokea kwa sababu ya ujinga wa sisi wananchi. Yanaiba kura, sisi tupo kimya, yanaiba pesa, tupo kimya. Kwa nini yasiongeze kuiba!!
Hivi kama tumeshindwa japo kuandamana kudai tuoneshwe kwa majina, hayo majizi ili tukayakokote kuyaondoa ofisini, kwa nini hata tusigome wote kwa pamoja kulipa kodi mpaka tutakapokuwa na uhakika kodi zetu zinatumika vizuri?
Kwa hali ya wizi, rushwa na uzembe wa watendaji wa Serikali ya Tanzania, kwa kweli si halali kabisa kulipa kodi. Wajibu hauwezi kukaa upande mmoja. Yaani mwananchi alipe kodi, lakini mkusanyaji atapanye kodi kwa anasa na wizi. Hii haikubaliki. Kama anayekusanya hana uwezo wa kuitunza hela inayokusanywa ikawa salama, basi asikusanye mpaka siku atakapokuwa na uwezo wa kuilinda na kuitumia vizuri na kwa umakini kwa manufaa ya walipa kodi.
Kama tusingekuwa na majitu majizi kwenye ofisi za Serikali na taasisi zake, ingewezekana vipi shirika kama TANESCO, lisilo na mshindani, linalopewa mpaka na ruzuku na Serikali, lingeweza kupata hasara?
Ni mradi gani wa Serikali au CCM uliwahi kufanikiwa? TBL walifeli, TANESCO wamefeli, viwanda vya bidhaa mbalimbali walifeli, SUKITA ya CCM ilifeli, Shule za wazazi za CCM zilifeli, maduka ya TRC yalifeli, ATCL wamefeli, TTCL wamefeli, kila kitu wamefeli. Hata reli watafeli tu. Kwa sababu hawa watu hakuna wanachofikiria zaidi ya kuiba
Ukweli ni kwamba kila inapowezekana kukwepa kulipa kodi ni aheri kufanya hivyo. Maana hata ukilipa, kuna majitu yanaenda kuichezea pesa yako wakati wewe umejibana, umeiacha familia yako ikijibana na kuteseka, lakini huko kuna mijitu inaenda kuichezea pesa yako kama haina mwenyewe.