Nkobe
JF-Expert Member
- Feb 17, 2013
- 2,162
- 3,162
Ukifuatilia mjadala unaoendelea TBC juu ya chanjo ya COVID-19 na maswala ya uzalendo utangundua kuwa bado tuko na matatizo makubwa Africa.
Ukiutizama mjadala umejikita juu ya kuuponda ukoloni ambapo ni jambo jema ingawa ni mada ya kizamani. Ukiwasikiliza wasomi wanaochangia hizo mada, wamejikita kuwaponda wazungu badala ya kuwaambia Watanzania kuwa wao wamefanya nini.
Unamsikiliza Prof Mgaya akieleza huchukua takribani miaka 7 hadi 10 kupata chanjo rasmi, anasema hii chanjo inayotolewa iko katika majaribio, kwamba ufanisi wake ni kwa asilimia kidogo, je hizi dawa za miti shamba tunazoambiwa zinatibu Corona, Covidol, NIMRCRAF na ile iliyofuatwa kwa ndege ya umma Madagascar ilifanyiwa majaribio miaka mingapi? . Hapa unajiuliza, kama kwa siku nchi inaweza kupoteza maelfu ya watu, je inabidi usubiri miaka 10 ndipo uzuie vifo? Lakini je ni kweli kwa technolojia ya sasa karne ya 21 ni lazima usubiri miaka 7 au 10 ndipo ujue chanjo inafanya kazi au la? Haya ni maswali ya kujiuliza.
Jambo la mwisho, wasomi hawa wanaoendesha mjadala, hawasemi kabisa kuwa serikali imefanya nini hadi sasa kuwekeza kwenye uvumbuzi wa chanjo yetu binafsi ya Corona, inakuwaje wewe hata kujaribu hufanyi halafu unainua mdomo wako kuponda chanjo zinazotoka nje ya nchi?. Je kwanini Tanzania hatuandai chanjo zetu? kama tunaweza kutumia mabilioni ya pesa kujenga miundombinu ambayo haina manufaa kwa wananchi, inakuwaje tushindwe kutumia mabilioni kuwekeza kwenye chanjo zetu badala ya kulalama na habari ya chanjo ya tunaowaita mabeberu?
Ukiutizama mjadala umejikita juu ya kuuponda ukoloni ambapo ni jambo jema ingawa ni mada ya kizamani. Ukiwasikiliza wasomi wanaochangia hizo mada, wamejikita kuwaponda wazungu badala ya kuwaambia Watanzania kuwa wao wamefanya nini.
Unamsikiliza Prof Mgaya akieleza huchukua takribani miaka 7 hadi 10 kupata chanjo rasmi, anasema hii chanjo inayotolewa iko katika majaribio, kwamba ufanisi wake ni kwa asilimia kidogo, je hizi dawa za miti shamba tunazoambiwa zinatibu Corona, Covidol, NIMRCRAF na ile iliyofuatwa kwa ndege ya umma Madagascar ilifanyiwa majaribio miaka mingapi? . Hapa unajiuliza, kama kwa siku nchi inaweza kupoteza maelfu ya watu, je inabidi usubiri miaka 10 ndipo uzuie vifo? Lakini je ni kweli kwa technolojia ya sasa karne ya 21 ni lazima usubiri miaka 7 au 10 ndipo ujue chanjo inafanya kazi au la? Haya ni maswali ya kujiuliza.
Jambo la mwisho, wasomi hawa wanaoendesha mjadala, hawasemi kabisa kuwa serikali imefanya nini hadi sasa kuwekeza kwenye uvumbuzi wa chanjo yetu binafsi ya Corona, inakuwaje wewe hata kujaribu hufanyi halafu unainua mdomo wako kuponda chanjo zinazotoka nje ya nchi?. Je kwanini Tanzania hatuandai chanjo zetu? kama tunaweza kutumia mabilioni ya pesa kujenga miundombinu ambayo haina manufaa kwa wananchi, inakuwaje tushindwe kutumia mabilioni kuwekeza kwenye chanjo zetu badala ya kulalama na habari ya chanjo ya tunaowaita mabeberu?