Ukipendwa, pendeka

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,709
Reaction score
35,701
Hamna mtu anaependa kuwa Single. Kuwa single sio kwamba mtu hujui kupenda. Sababu kubwa ni kuchoka kujitoa kwa mtu halafu mwishoni unapata maumivu.
.
Inachoka kuamini na kupenda sana mtu na mwishoe inaishia kusalitiwa na kuumizwa moyo.
.
Inachosha na inaumiza sana kujali, kuheshimu na kuonesha uaminifu lakini unaambulia kudanganywa na kupigwa danadana !
.
Inachosha kuwa na mipango mingi ya mbali na mtu ambaye lengo lake ni la muda mfupi!
.
Hivyo, kabla hujamjaji mtu, ukamwita majina mabaya na kumlaumu katika msimamo wake wa maisha, hebu fikiria kwanza ni nini kimemfanya awe hivyo.
.
Vaa viatu vyao na uone maumivu waliyopitia. Wamepitia mengi ya kuumiza na kukatisha tamaa katika mahusiano. Hofu hiyo bado imewajaa mioyoni mwao. Hawana uhakika na yupi atakayefaa kupewa tena nafasi mioyoni mwao.
.
Ndio, wanayo mapenzi ya dhati, lakini uhakika wa nani apewe ndio haupo. Kama mtu akikupenda, jaribu kumuelewa, jaribu kumjali, jaribu kumuonesha kwamba, wewe sio kama wale wengine.
.
"The best and most beautiful things in this world cannot be seen or even heard, but must be felt with the heart. Keep love in your heart."
 
Nshawahi mkuu, hapa namaanisha mpenzi wako, huyo anayekupenda na wewe humpendi maana yake nyie sio wapenzi.
Kumuelewa na kumjali mwanamke ambae humpendi ni kujidanganya aiseeh; yeye atafikiri unafanya hivyo kwa sababu umeshaanza kumpenda kumbe wewe unafanya hivyo ili usimuumize!! hapo ndo unazidi kulikoroga kwa sababu some days utachoka kumfanyia ivo kwa sababu humuelewi yani ile siku ukichoka kumfanyia ivo thats where the troublesome begin....
Mkuu; Kumcare mtu ambae sina malengo nae yoyote just for the purpose ya kutokumuumiza, i did it once na siku nilipochoka (kwa sababu lazima uchoke tu si haumpendi!!) you know what i found?? It was chaotic, catastrophic!! Kama nisingenotice mapema kama ameshakunywa sumu na kumuwaisha hospitali maanake today ingekua different story.
MY TAKE: Ukipendwa na mwanamke ambae humpendi cha kwanza umwambie tena iwe MAPEMA sana then usimjali kiivo kwa sabu atafikiria possibly umeshachange your mind na kuanza kumuelewa which is not.
 
Bro kama hukumpenda kwann ulianzisha mahusiano nae??

Ukiona mtu anakuonyesha dalili za kukupenda unamwambia vile unafeel right from the beggining

Mapenzi ni mutual feeling for both sides
 
Bro kama hukumpenda kwann ulianzisha mahusiano nae??

Ukiona mtu anakuonyeaha dalili za kukupenda unamwambia vile unafeel right from the beggining

Mapenzi ni mutual feeling for both sides
Nilichokitumia kipindi kile ni hiyo heading yako Mkuu ya "ukipendwa, pendeka" which actually it doesn't work kwa wanaume wengi. Ulichokizungumza hapa ndio nimekitoa kwenye My take pale chini.
 
Poa mkuu
Nilichokitumia kipindi kile ni hiyo heading yako Mkuu ya "ukipendwa, pendeka" which actually it doesn't work kwa wanaume wengi. Ulichokizungumza hapa ndio nimekitoa kwenye My take pale chini.
 
Inahitaji uvumilivu wa juu,hata awe billionea kama humpendi hutoishi kwa furaha katu
 
Inaumiza sana kwa kweli , unajitoa kama n maji yanachemka 100c halaf yeye wa baridiiii kama barafu inaudhi kimahaba.
 
Inauzi nini sasa. ..kwani Kuna ulazima kwa yule unaempenda nae kukupenda hivyo hivyo ---

Ni ubinafsi mkubwa sana -pale unapotaka hisia zako za upendo dhidi ya mtu fulani na yeye hisia zake ziweze kufanana na wewe. ..wakati Nyie ni watu wawili wenye hisia na matakwa tofauti. .....

Ukiona unaempenda mtu halafu umemuonyesha hisia zote na jinsi unavyo mjali halafu bado ikawa hakupendi basi achana nae. ..Huenda ikawa mawazo yake yapo kwa mtu mwingine ambaye ni tofauti ki-vigezo vya upendo na wewe
Inaumiza sana kwa kweli , unajitoa kama n maji yanachemka 100c halaf yeye wa baridiiii kama barafu inaudhi kimahaba.
 
Umeongea vzr mkuu, ila mm sijamaanisha kulaumu bali "inauma" kujiona hupendwi wakati ndo chaguo lako! I know real love is fair play.
 
Wengine ni kunguru hawaelewi maana ya kupendwa lazima warudi majalalani wakachakure chakure. Ukigundua hivyo usipoteze muda wako au utaumiza moyo wako bure.

Kunguru hafugiki. Hayo si maneno ya BAK bali ya wahenga.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…