Ukipandisha bei ya mafuta ya kula itakula kwetu

Ukipandisha bei ya mafuta ya kula itakula kwetu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,255
Reaction score
16,185
Lazima tufanye tathimini ya kina kujua kama ndani ya Tanzania kuna uzalishaji wa mafuta ya kula yakutosha kutosheleza mahitaji yetu ya mafuta ya kupikia kabla hatujatoza kodi ya mafuta yanayoagizwa, viginevyo zigo looote litawaangukia wananchi wenye kipato cha chini ambao LAZIMA wakanunue mafuta dukani ndio wale chakula.

Lazima waziri wa kilimo na chakula aje na takwimu halisi zinazoonyesha:
1. Mahitaji ya mafuta nchini kwa siku/week/mwezi/mwaka
2. Kiasi cha mafuta kinachozalishwa nchini
3. Kiasi cha mafuta kinachoagizwa nje ya nchi (imported)
4. Kiasi cha mafuta kinachosafirishwa nje ya nchi (exported)

Wananchi wetu hawa tunaweza kuwakuta wote wakiwa wamechanganyikiwa na wasijue cha na la kufanya. Ubepari, kodi nyingi na mifumo imara ya ulinzi kule Marekani vinasababisha wananchi wengi wasijue nini cha kukufanya, wamechanganyikiwa kiasi cha kumudu kusema na kufanya chochote kizuri sana au kibaya sana.
 
Mahitaji mkuu ni tan 450000 kwa mwaka viwanda vya ndani vina uwezo wa kuzalisha 130000 kwa mwaka Sawa na asilimia 30 Hapo tutegemee maumivu kwa ile kauli ya mkuu ya Jana ya sukari soon yanakuja ktk maFuta
 
Mahitaji mkuu ni tan 450000 kwa mwaka viwanda vya ndani vina uwezo wa kuzalisha 130000 kwa mwaka Sawa na asilimia 30 Hapo tutegemee maumivu kwa ile kauli ya mkuu ya Jana ya sukari soon yanakuja ktk maFuta
Ila uzalishaji huu mdogo ulikuwa unasababishwa na uagizaji wa mafuta ya poor quality ya bei nafuu kutoka nje, hivyo kwa kuyapiga kodi basi wazalishaji wa ndani watapata nguvu ya kuongeza uzalishaji na ushindani
 
Jamani limeni Alizeti kwa wingi ili tupate mafuta ya kutosha
Lazima ulime kwanza kabla ya kufunga milango. Zamani tulikuwa na sabuni ya gardenia tu tukafungia rexona, life boy n.k tukakiona cha moto.
 
watu wengi hawalimi kwakua bei ya alizeti haipandi. Yafungiwe kabisa ili mikoa inayolima alizeti iendelee.kumekuwepo tabia ya kuchanganyiwa mafuta ya alizeti na korie Lisa korie ni bei poa.
 
watu wengi hawalimi kwakua bei ya alizeti haipandi. Yafungiwe kabisa ili mikoa inayolima alizeti iendelee.kumekuwepo tabia ya kuchanganyiwa mafuta ya alizeti na korie Lisa korie ni bei poa.
Utategemeaje kilimo cha kutegemea mvua na jembe la mkono kikupatie mafuta ya kutosha nchi nzima? Tusidanganyane!!
 
Back
Top Bottom