Ertugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 13,375
- 26,873
Mheshimiwa Rais wangu.
Pole na majukumu ya kazi yako ya uraisi,na pole Kwa lawama ambazo zinaelekezwa kwako hata pale ambapo makosa hayo yamefanywa na wasaidizi wako.
Mheshimiwa Rais natamani Ile kauli yako ya "ukinizingua nitakuzingua" iendelee kusikika tena na tena kwani watanzania Bila kuzinguliwa huwa hawafanyi kazi,Bila kuonyesha ukali huwa hawajitumi,Bila kufokewa wanaleta mazoea.
Mheshimiwa Rais mara baada ya kuchukua madaraka ya uraisi wasaidizi wako walikuwa bado na Ile hofu ya mtangulizi wako na Ile kauli yako kazi iendelee ikiambatana na "ukinizingua nitakuzingua" iliwafanya watendaji wako wakuogope na kuwajibika kwasababu walijua kabisa huna mswalie Mtume. Na wengine walienda mbali kabisa na kusema "mama hatabiriki" Kwa maana lolote linaweza kutokea. Hayo na mengine mengi yalifanya uonekane ni Raisi ambaye upo tayar kuchukua maamuzi magumu na hutaki kumuangalia mtu machoni,na hayo ndio mambo ambayo yanawafanya watanzania wawajibike ipasavyo.
Mheshimiwa Rais wewe umesomea Uongozi,na katika Uongozi wakati mwingine unatakiwa uwe mkali kama chui na wakati mwingine uwe mpole,lakini hayo yote yatategemeana na utashi wa wale unao waongoza,Kwa mazingira ya Tanzania kuwa mkali ndio best choice kwakuwa ndio tunavyopenda hivyo kwani Bila kushurutishwa huwa tunafanya mambo kimazoea.
Katika Uongozi pia kuna theories mbali mbali lakini moja wapo ni theory X na theory y
Theory X inazungumzia wale watu ambao wanajituma kufanya majukumu yako Bila kusimamiwa ,hawa hawahitaji kusimamiwa au kuambiwa nini cha kufanya,mara zote huwa ni wachapakazi hodari Sana,na watu hawa ukiwasimamia unashusha morali Yao ya kazi,watu hawa wanahitaji motisha kidogo na kazi inaendelea Kwa asilimia Mia mbili, lakini bahati mbaya Sana hawa watu wapo wachache sana ukilinganisha na watu wa theory y.
Watu wa theory y ni watu ambao hawajitumi,wanapenda kusimamiwa na kushurutishwa,hawa kama boss akiondoka Tu ofisini nao wanawacha kuwajibika na kutegea kufanya kazi,hawa wanahitaji uwe mkali zaidi ndio utaenda nao Sawa,hawa hawahitaji kuambiwa kauli kama " kila mtu ale na urefu WA kamba yake" kwani Kwa kufanya hivyo ndio unakuwa umewapa tiketi ya kufanya ubadhirifu na ufisadi WA kiwango cha mwendo Kasi.
Hawa si watu wa kuwaambia "alikuwepo Simba wa Yuda ambaye kila mtu alimuogopa". Hawa ni watu ambao wanatakiwa waone kauli yako na matendo yako yanasadifu malengo yako na matakwa yako ili inchi yetu isonge mbele.
Nina mengi ya kusema lakini kwa Leo naomba niishie hapa najua Una majukumu mengi ya kitaifa, panapo majaliwa nitateta na wewe tena.
Kwa heshima na taadhima naomba kuwasilisha.
Ni hayo tu.
Pole na majukumu ya kazi yako ya uraisi,na pole Kwa lawama ambazo zinaelekezwa kwako hata pale ambapo makosa hayo yamefanywa na wasaidizi wako.
Mheshimiwa Rais natamani Ile kauli yako ya "ukinizingua nitakuzingua" iendelee kusikika tena na tena kwani watanzania Bila kuzinguliwa huwa hawafanyi kazi,Bila kuonyesha ukali huwa hawajitumi,Bila kufokewa wanaleta mazoea.
Mheshimiwa Rais mara baada ya kuchukua madaraka ya uraisi wasaidizi wako walikuwa bado na Ile hofu ya mtangulizi wako na Ile kauli yako kazi iendelee ikiambatana na "ukinizingua nitakuzingua" iliwafanya watendaji wako wakuogope na kuwajibika kwasababu walijua kabisa huna mswalie Mtume. Na wengine walienda mbali kabisa na kusema "mama hatabiriki" Kwa maana lolote linaweza kutokea. Hayo na mengine mengi yalifanya uonekane ni Raisi ambaye upo tayar kuchukua maamuzi magumu na hutaki kumuangalia mtu machoni,na hayo ndio mambo ambayo yanawafanya watanzania wawajibike ipasavyo.
Mheshimiwa Rais wewe umesomea Uongozi,na katika Uongozi wakati mwingine unatakiwa uwe mkali kama chui na wakati mwingine uwe mpole,lakini hayo yote yatategemeana na utashi wa wale unao waongoza,Kwa mazingira ya Tanzania kuwa mkali ndio best choice kwakuwa ndio tunavyopenda hivyo kwani Bila kushurutishwa huwa tunafanya mambo kimazoea.
Katika Uongozi pia kuna theories mbali mbali lakini moja wapo ni theory X na theory y
Theory X inazungumzia wale watu ambao wanajituma kufanya majukumu yako Bila kusimamiwa ,hawa hawahitaji kusimamiwa au kuambiwa nini cha kufanya,mara zote huwa ni wachapakazi hodari Sana,na watu hawa ukiwasimamia unashusha morali Yao ya kazi,watu hawa wanahitaji motisha kidogo na kazi inaendelea Kwa asilimia Mia mbili, lakini bahati mbaya Sana hawa watu wapo wachache sana ukilinganisha na watu wa theory y.
Watu wa theory y ni watu ambao hawajitumi,wanapenda kusimamiwa na kushurutishwa,hawa kama boss akiondoka Tu ofisini nao wanawacha kuwajibika na kutegea kufanya kazi,hawa wanahitaji uwe mkali zaidi ndio utaenda nao Sawa,hawa hawahitaji kuambiwa kauli kama " kila mtu ale na urefu WA kamba yake" kwani Kwa kufanya hivyo ndio unakuwa umewapa tiketi ya kufanya ubadhirifu na ufisadi WA kiwango cha mwendo Kasi.
Hawa si watu wa kuwaambia "alikuwepo Simba wa Yuda ambaye kila mtu alimuogopa". Hawa ni watu ambao wanatakiwa waone kauli yako na matendo yako yanasadifu malengo yako na matakwa yako ili inchi yetu isonge mbele.
Nina mengi ya kusema lakini kwa Leo naomba niishie hapa najua Una majukumu mengi ya kitaifa, panapo majaliwa nitateta na wewe tena.
Kwa heshima na taadhima naomba kuwasilisha.
Ni hayo tu.