Ukilala, usilale kimasikini

Apr 14, 2016
6
18
Kuna wakati ni ngumu kukumbatia maumivu ukitabasamu.
Kuna wakati usingizi huja baada ya machozi.

Wakati ambapo kila ladha ni Chungu na kila tendo ni vivu.
Huo wakati ambao hujielewi wewe ni nani ukihisi umepungukiwa akili ,nafsi mpaka roho.

Huo wakati unaopitia ni kila mtu anapitia kwa namna yake kwa kipindi cha maisha fulani,Yapasa ujue.

Jua la mchana likikuchoma ,usilichukie bali cheka nalo ukilitania.
Na Giza la usiku likiingia zungumza nalo kitajiri kuhusu Mwanga.
Lala na Tumaini ,usilale na majonzi.

Hivyo Basi ukilala ,utakuwa umelala kitajiri.
 
Kuishia kuwaza waza matumaini yasiyo na uhalisia, mawazo hayo huitwa ni "ndoto"!

Kuishia kuburudishwa na ndoto hizo na kupelekea kucheka cheka tu kwa furaha bila ya kuzigeuza ndoto hizo kuwa kweli, ni umasikini wa kiwango cha changarawe!
 
Huna ajira
Unadaiwa kodi
Hujala
Unga kilo 1800
Nyama ushawaachia matajiri
Mchele mpaka kwenye misiba au sherehe
Kwanini usialale kimaskini
Na ukiwa ktk mateso/msoto,njaa uukuzoea sana.Hapa kati nimekula sahani mbili kubwa za wali usiku wakati huo mchana nilikuwa nimekula ugal mkubwa na bakuli la maharage.Umasikin mbaya sana hadi kila kitu kinakuchukulia poa!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom