Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 3,288
- 5,762
Hapa sina nia yoyote ya kumsema mtu ila ni kuelimishana tu
Naamini mtu akikaa mwenyewe (peke yake) akatafakari anaweza kujua mahusiano yake na Mungu yakoje namaanisha anaweza kujua kama amefaulu au kuna cha kujirekebisha
Sasa kwa kuwa nafasi bado tunayo; kwa nini tusichukue hii fursa kujirekebisha kwani hatujui muda wala saa?
Mambo matatu makuu yanayotuweka mbali na Mungu ni
1. Harakati za kutafuta mali
2. Tamaa ya kujilimbikizia mali na Ardhi
3. Wivu na husuda
“Kumbuka Mungu hadanganyiki kwani anaona yale ya waziwazi na yale ya sirini”
Muhimu ni kukumbushana ila uamuzi ni wa kwako!
Naamini mtu akikaa mwenyewe (peke yake) akatafakari anaweza kujua mahusiano yake na Mungu yakoje namaanisha anaweza kujua kama amefaulu au kuna cha kujirekebisha
Sasa kwa kuwa nafasi bado tunayo; kwa nini tusichukue hii fursa kujirekebisha kwani hatujui muda wala saa?
Mambo matatu makuu yanayotuweka mbali na Mungu ni
1. Harakati za kutafuta mali
2. Tamaa ya kujilimbikizia mali na Ardhi
3. Wivu na husuda
- Angalia njia yako ya kujipatia kipato kuona kama inampendeza Mungu; kwa kawaida kisicho mpendeza Mungu hakiwapendezi hawa wanadamu wanaotegemea huduma yako. Mfano: Kupunja kwenye Mizani, Kuchakachua bidhaa, wanasheria wanaopindisha sheria, Wizi nk Mungu hapendi kabisa
- Kumiliki mali ni jambo jema sana ila angalia upatikanaji wake; kama unaona umilikaji wako mali unatokana na kunyima watu wengine haki yao ya kupata huduma; jua Mungu hapendi kabisa na siku unaondoka pengine zinaweza kusambaratika zote na bado unahoja unatakiwa ukajibu kwa Mungu
- Watu wengine huchukia watu kwa Wivu tu na kuwafanyia figisu figisu ili wafukuzwe kazini/kwenye ndoa zao na kuharibu Maisha yao kabisa; Hii huambatana pia na Uchawi/ushirikina wa kutesa watu wengine bila sababu; Kama unafanya haya, jua Mungu anahasira na wewe; jirekebishe
- Kuendekeza Zina ama pengine kutumia zinaa kama kigezo cha kumpatia mtu favor nk Mungu hapendi
“Kumbuka Mungu hadanganyiki kwani anaona yale ya waziwazi na yale ya sirini”
Muhimu ni kukumbushana ila uamuzi ni wa kwako!