TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,868
- 5,753
Habari za Jumatatu wapendwa.
Itakumbukwa kwamba Oktoba 26, 2014 , vyama vinne ; Chadema , NCCR Mageuzi , CUF NLD vilifikia makubaliano SABA ya Muungano wao ambao ni pamoja na:
1. Kuhusisha sera zao na kuchukua yote yanayofanana ili viwe na kauli Zinazolingana na kufanana kwa Watanzania.
2. Kusimamisha wagombea wa pamoja kwenye chaguzi zote kuanzia serikali za mitaa, udiwani, ubunge, uwakilishi wa urais kwa jamhuri ya Muungano na Zanzibar.
3. Kuweka utaratibu wa namna gani vyama hivyo vingeshirikiana kwenye uchaguzi wa mitaa uliofanyika Desemba 2014 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
4. Kushirikiana kuelimisha umma kupiga kura ya Hapana katika mchakato wa kura ya maoni ya Katiba inayopendekezwa iliyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
5. Kujenga ushirikiano wa dhati kwa mambo yote na hoja zote za msingi zenye maslahi kwa Taifa.
6. Kuulinda Muungano bila ya kuwa na migongano ya kimaslahi kama ilivyojitokeza kwenye Katiba inayopendekezwa.
7. Kuhimiza na kusimamia ushirikiano wa pmoja baina yao na asasi zingine.
Mytake: Mpaka sasa UKAWA yapi mmetekeleza kati ya hayo saba? Tumeshuhudia kwenye uchaguzi wa sm uliomalizika hivi karibuni baadhi ya vyama washirika vikiambulia patupu kabisa na kutosikika kabisa kana kwamba hawako UKAWA na maeneo mengine mfano mkoa wa pwani vyama washirika kutupiana lawama za kuhujumiana kwa maana ya kukiuka masharti ya kuachiana maeneo ya kugombea.
Kule Mtwara tumeshuhudia kiongozi wa chama kinachounda UKAWA akikiuka makubaliano kwa akimpandisha jukwaani mwanachama aliyekataliwa na chama chake. Tayari kuna vyama vimeshatangaza wawakilishi wao kwenye kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Aidha ajenda ya kumpata mgombea mmoja wa urais kuwakilisha UKAWA ambayo ilisemekana nayo ingekuwa moja ya agenda za kikao cha kesho inaonekana kuyeyuka. Yapi mmeshatekeleza kati ya hayo Saba?
Itakumbukwa kwamba Oktoba 26, 2014 , vyama vinne ; Chadema , NCCR Mageuzi , CUF NLD vilifikia makubaliano SABA ya Muungano wao ambao ni pamoja na:
1. Kuhusisha sera zao na kuchukua yote yanayofanana ili viwe na kauli Zinazolingana na kufanana kwa Watanzania.
2. Kusimamisha wagombea wa pamoja kwenye chaguzi zote kuanzia serikali za mitaa, udiwani, ubunge, uwakilishi wa urais kwa jamhuri ya Muungano na Zanzibar.
3. Kuweka utaratibu wa namna gani vyama hivyo vingeshirikiana kwenye uchaguzi wa mitaa uliofanyika Desemba 2014 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
4. Kushirikiana kuelimisha umma kupiga kura ya Hapana katika mchakato wa kura ya maoni ya Katiba inayopendekezwa iliyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
5. Kujenga ushirikiano wa dhati kwa mambo yote na hoja zote za msingi zenye maslahi kwa Taifa.
6. Kuulinda Muungano bila ya kuwa na migongano ya kimaslahi kama ilivyojitokeza kwenye Katiba inayopendekezwa.
7. Kuhimiza na kusimamia ushirikiano wa pmoja baina yao na asasi zingine.
Mytake: Mpaka sasa UKAWA yapi mmetekeleza kati ya hayo saba? Tumeshuhudia kwenye uchaguzi wa sm uliomalizika hivi karibuni baadhi ya vyama washirika vikiambulia patupu kabisa na kutosikika kabisa kana kwamba hawako UKAWA na maeneo mengine mfano mkoa wa pwani vyama washirika kutupiana lawama za kuhujumiana kwa maana ya kukiuka masharti ya kuachiana maeneo ya kugombea.
Kule Mtwara tumeshuhudia kiongozi wa chama kinachounda UKAWA akikiuka makubaliano kwa akimpandisha jukwaani mwanachama aliyekataliwa na chama chake. Tayari kuna vyama vimeshatangaza wawakilishi wao kwenye kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Aidha ajenda ya kumpata mgombea mmoja wa urais kuwakilisha UKAWA ambayo ilisemekana nayo ingekuwa moja ya agenda za kikao cha kesho inaonekana kuyeyuka. Yapi mmeshatekeleza kati ya hayo Saba?