singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,538
MUUNGANIKO vya vyama vinne vya siasa unaojulikana kwa jina la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umeanza kumhofia Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, baada ya kumuweka mizengwe kuruhusu chama chake kujiunga katika umoja huo, TAIFA IMARA linaripoti.
Kwa sasa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho ni chama kishiriki katika UKAWA, kimelazimika kuanza ziara mikoani kujaribu kuondoa sumu iliyosambazwa na kiongozi huyo wa ACT kwenye mikoa mbalimbali.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, alilazimika kuwataka wafuasi wa chama hicho kupuuza hoja zinazotolewa na Zitto juu ya kuyumba kwa CHADEMA.
Kauli hiyo ya Lema aliyoitoa kwenye moja ya Mikutano ya hadhara iliyofanyika mjini Shinyanga hivi karibuni ni muendelezo wa matamshi ya John Mnyika aliyelazimika kuwataka wafuasi wa mageuzi kupuuza mikutano ya ACT bila mafanikio.
Pamoja na vizingiti vya kupuuzwa na viongozi waandamizi wa CHADEMA, Zitto ameandika barua ya kuomba kuunganishwa katika UKAWA. Katika kulitazama kwa kina jambo hilo, endelea na makala hii ya uchambuzi wa kisiasa juu ya nini kinachoendelea.
Wahenga walinena, "Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu," na msemo mwingine, "kidole kimoja hakiui chawa," misemo hii inahamasisha umoja katika kutenda jambo ili kuleta manufaa. Kauli kama hizi ndizo zilizosababisha vyama vya upinzani kuungana kujenga nguvu ya pamoja itakayowasaidia kupambana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichosheheni mizizi katika kila ngazi.
Cha kushangaza umoja huu unasitasita kukikubali chama kipya cha ACT- Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Zuberi Kabwe mwenye cheo cha Kiongozi Mkuu ingawa chama kina Mwenyekiti, Katibu na viongozi wengine kadha wa kadha waandamizi. Hata hivyo, muundo wa kuwa na Kiongozi Mkuu wa Chama hutumiwa na vyama vya kikomonisti.
Swali ni kwanini UKAWA (UKAWA ni kifupisho cha maneno Umoja wa Katiba ya Wananchi) wanamuogopa Zitto na chama chake cha ACT Wazalendo?
Zitto Kabwe ni miongoni mwa wanasiasa vijana machachari waliowahi kuleta ladha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mtu pekee aliyemuibua mwanasiasa huyu ni mzee wa kasi na viwango Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta katika Bunge la Tisa wakati alipokuwa Spika wa Bunge.
Sitta aliwapa wapinzani uhuru mkubwa wa kuwakilisha mawazo yao na kuwaunga mkono wapinzani wenye hoja zenye kutetea maslahi ya wananchi. Zitto alikuwa miongoni mwa wabunge wa CHADEMA walioweza kujijengea sifa na kuaminika kwa wananchi kama wawakilishi wazuri wa upande wa upinzani wanaoweza kuwashtua baadhi ya mawaziri ili wawajibike ipasavyo katika wizara zao wanazozisimamia.
Kwa upande wa UKAWA ni muunganiko wa vyama vya kambi ya upinzani ambao waliungana wakati wa mchakato wa rasimu ya Katiba kwa kigezo cha kuwawakilisha wananchi. Umoja huo unaendeleza jina hilo ukiwa na nia ya kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais kwa tiketi ya vyama vya upinzani.
CHADEMA ilimvua uanachama aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto kwa madai ya kukiuka Katiba ya chama hicho. CHADEMA ipo ndani ya UKAWA na Zitto alionekana mtu asiyefaa kwenye chama. Hizi ni baadhi ya sababu za UKAWA kumuogopa Zitto na chama chake cha ACT wazalendo.
Chanzo: TAIFA IMARA
Kwa sasa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho ni chama kishiriki katika UKAWA, kimelazimika kuanza ziara mikoani kujaribu kuondoa sumu iliyosambazwa na kiongozi huyo wa ACT kwenye mikoa mbalimbali.
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, alilazimika kuwataka wafuasi wa chama hicho kupuuza hoja zinazotolewa na Zitto juu ya kuyumba kwa CHADEMA.
Kauli hiyo ya Lema aliyoitoa kwenye moja ya Mikutano ya hadhara iliyofanyika mjini Shinyanga hivi karibuni ni muendelezo wa matamshi ya John Mnyika aliyelazimika kuwataka wafuasi wa mageuzi kupuuza mikutano ya ACT bila mafanikio.
Pamoja na vizingiti vya kupuuzwa na viongozi waandamizi wa CHADEMA, Zitto ameandika barua ya kuomba kuunganishwa katika UKAWA. Katika kulitazama kwa kina jambo hilo, endelea na makala hii ya uchambuzi wa kisiasa juu ya nini kinachoendelea.
Wahenga walinena, "Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu," na msemo mwingine, "kidole kimoja hakiui chawa," misemo hii inahamasisha umoja katika kutenda jambo ili kuleta manufaa. Kauli kama hizi ndizo zilizosababisha vyama vya upinzani kuungana kujenga nguvu ya pamoja itakayowasaidia kupambana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichosheheni mizizi katika kila ngazi.
Cha kushangaza umoja huu unasitasita kukikubali chama kipya cha ACT- Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Zuberi Kabwe mwenye cheo cha Kiongozi Mkuu ingawa chama kina Mwenyekiti, Katibu na viongozi wengine kadha wa kadha waandamizi. Hata hivyo, muundo wa kuwa na Kiongozi Mkuu wa Chama hutumiwa na vyama vya kikomonisti.
Swali ni kwanini UKAWA (UKAWA ni kifupisho cha maneno Umoja wa Katiba ya Wananchi) wanamuogopa Zitto na chama chake cha ACT Wazalendo?
Zitto Kabwe ni miongoni mwa wanasiasa vijana machachari waliowahi kuleta ladha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mtu pekee aliyemuibua mwanasiasa huyu ni mzee wa kasi na viwango Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta katika Bunge la Tisa wakati alipokuwa Spika wa Bunge.
Sitta aliwapa wapinzani uhuru mkubwa wa kuwakilisha mawazo yao na kuwaunga mkono wapinzani wenye hoja zenye kutetea maslahi ya wananchi. Zitto alikuwa miongoni mwa wabunge wa CHADEMA walioweza kujijengea sifa na kuaminika kwa wananchi kama wawakilishi wazuri wa upande wa upinzani wanaoweza kuwashtua baadhi ya mawaziri ili wawajibike ipasavyo katika wizara zao wanazozisimamia.
Kwa upande wa UKAWA ni muunganiko wa vyama vya kambi ya upinzani ambao waliungana wakati wa mchakato wa rasimu ya Katiba kwa kigezo cha kuwawakilisha wananchi. Umoja huo unaendeleza jina hilo ukiwa na nia ya kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais kwa tiketi ya vyama vya upinzani.
CHADEMA ilimvua uanachama aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto kwa madai ya kukiuka Katiba ya chama hicho. CHADEMA ipo ndani ya UKAWA na Zitto alionekana mtu asiyefaa kwenye chama. Hizi ni baadhi ya sababu za UKAWA kumuogopa Zitto na chama chake cha ACT wazalendo.
Chanzo: TAIFA IMARA