UKAWA wakubali kuchemka

UKAWA wakubali kuchemka

Reuters

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2015
Posts
375
Reaction score
160
Zimebaki siku chache za kampeni. Mgombea wa‪ CCM, ‎Dr Magufuli ameonyesha uimara wake kila siku tofauti na mgombea wa UKAWA - ambaye anaonekana amechoka, yuko hoi balaa.

CCM kupitia Magufuli imekamilisha kampeni zake zaidi ya- Mikoa 21 na Wilaya 120, ukiachia mbali stop-overs za kumwaga huko njiani. Magufuli amekuwa akitoa hotuba zenye kuleta matumaini mapya ya‪ Tanzania tuitakayo tofauti na Lowasa ambaye amehahaa tu na hata majimbo yote anakopita- hamalizi kutokana na afya yake.

Kwenye kampeni hakuna kitu cha maana zaidi ya wapiga kura kujihisi wanakusikia wewe mwenyewe ukiwapa ahadi za kuboresha hali zao za maisha. Personal connection is very important kwenye kampeni. Ukifanya mikutano michache, ama usipofanya, kwa kiasi kikubwa unajipunguzia kura zako mwenyewe tu.

UKAWA hawafanyi kampeni, kazi yao kutoa vitisho na kutia wananchi shaka ya kuwa wataibiwa kura, hivi nani atahangaika kuwaibia kura ambazo hawana tofauti na kulalamika kila kukicha?

Hivi kweli chama kina wagombea ubunge 138, kina migogoro na wagombea wa CUF kwenye majimbo zaidi ya 50, kitashindaje sasa? Wabunge wote mashuhuri wa vyama vyao hawana muda na kumuuza mgombea Urais, wanakomaa na kampeni zao majimboni japo pia wameshikwa vibaya na wagombea mahili wa CCM, hali si shwari kabisa.

Lowassa anahaha mtaani na-‪ makapi-toka CCM. Makapi yenyewe hayana mvuto wowote kwa jamii basi tu ilimradi wanamtia moyo kamanda wao anayetoa hotuba za dakika 5 tu.

Sasa watashindaje? Hawa kwa hakika wamejihakikishia kushindwa tu, hakuna namna nyingine!
 
Hawa ukiwa wamejua wamepigwa vibaya, sasa babu kizee kama yule kumbukumbu hana unategemea ushindi,poleni sana
 
Aiseeeee Tarehe 25 na ije mapema
 
nyie pengine hamjui mlitendalo hivi mko sawasawa kweli? pili niulize mnaishi nchi gani isiyo na vyombo vya habar?
 
Kweli wameshakubali kushindwa Maana hata babu duni hajichoshi kuzunguka

ratiba inaonyesha leo babu duni angekuwa ruaha jimbo la mikumi lakin hadi sasa hajatokea Wananchi wamekasirika sana Anawaponza wagombea wao wa ukawa wa huku

Naomba nichukue fursa hii kumtangaza mhe dkt john pombe magufuli Kuwa rais wa awamu ya tano
 
Ukiwaambia ukweli hivi wahuni wao humu ndani wanaanza matusi, waache wataisoma namba ..mzee ilani hana eti anawaambia wakasome kwenye tovuti, wamekwishaaaa!
 
Tuachie ukawa tunajua tunachokifanya, acha umbea fanya ya sisiem.
 
Tulia upate dawa vizuri.

Zimebaki cku 20 tu c nyingi, natoa tu angalizo, kuwa pamoja ushabiki tulionao bado tujue kuwa watz ndio watakaoamua raic, mbunge na diwan. ck zilizobaki ni 20 tu. busara itumike kupunguza kujihic vby baada y kile ulichokipigia debe kushindwa. ccm mnaongea sana, mwaka huu kura zinahesabiwa vituon na malofa na wapumbavu tuliojiandikisha n wengi
 
Mnajifanya kujaribu propaganda lakini mnapost ujinga usioenda shule, hata mnachoandika ni ujinga na hamueleweki! Ukweli wa UKAWA hata wewe unaujua ndio maana unashinda kupost upuuzi, Yaani tar 25 mtalia na hamtakaa msahau! Maana mpaka hapa rais anajulikana wazi, CCM mwaka huu sijui mtapewa kura na Nani!Mnati huruma.
 
Reuters

Wewe na wenzio mna stress za Kingunge
 
Last edited by a moderator:
Mimi naipa kura ccm na ubunge ni act.

Hapa kazi tu ushindi niwetu
 
Ukiwaambia ukweli hivi wahuni wao humu ndani wanaanza matusi, waache wataisoma namba ..mzee ilani hana eti anawaambia wakasome kwenye tovuti, wamekwishaaaa!

Hahahaha
Ilan hawana wahun hawa

Kama unabisha waambie wakutumie picha ya front page ya ilan yao ukawa
natoa laki tatu
 
Nilicho jifunza siasa za tz. Watu wa nafuata mtu. Kinguge kaamua kumfuata aliye kuwa anamsapoti el na sio sera za chama.
 
Mmmh wana CCM wenzangu tumekamatwa pabaya tuseme kweli ya moyo wetu. Nina kadi yangu CCM na chama changu kina sera nzuri but kwa this time tusahau nchi inaenda kwa upinzani. Ni vizuri kukipigania chama ila sio vizuri kukifia ilihali ni wazi kwamba utendaji wake umezorota kwa kiasi kikubwa hata wananchi wamechoka.

Hivi haiwaingii akilini wazee tuliokula kiapo cha TANU na kulelewa ktk misingi imara ya TANU na CCM ya 1980s leo hii wanatandika daruga na kuondoka au kusema kuwa kadi situpi na kwenye chama siondoki ila kura yangu ni kwa upinzani. Naipenda CCM na sera zake ILA SIKO TAYARI KUENDELEA KUIUZA NCHI YANGU NA KUENDELEA KUONA MNYONGE ANAENDELEA KUNYONGWA KILA SIKU - UKIENDA HOSPITALINI WATU WANALALA CHINI ILA VIONGOZI WA JUU HAWANA HABARI KILA SIKU KWAO NI KAMA SIKUKUU, KARAMU HAZIISHI TENA KARAMU NZITO NA NONO AT EXPENSE OF TAX PAYERS

WHY SHOULD I?

KUWA MWANACHAMA WA CHAMA FULANI HAKUKUZUI KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KWA WAKATI SAHIHI.
 
Back
Top Bottom