UKAWA sasa tuna kazi moja ya kumuandaa mgombea urais wa 2020

ibesa mau

JF-Expert Member
Sep 17, 2015
2,109
1,692
Vita ni maandalizi na watalaamu wa vita wanasema wakati mzuri wa kujiandaa na vita ni wakati wa amani. Huwezi kushinda kama unategemea wakati wa mapambano ndio uandae silaha. Sasa ni wakati wa kufanya maandalizi ya kutafuta mtu sahihi atakayepeperusha bendera ya ukawa. Ni mtu mjinga anayefikiria muungano wa Ukawa unaweza kuvunjika lakinj ukawa hauwezi kuvunjika kwa sababu vyama vikubwa vyote cuf na chadema wamenufaika mno na umoja huo . Nccr wanaonekana kupoteza kwa sababu ya mazingira yaliyopo kwamba walijiimarisha zaidi mkoa mmoja wa kigoma na ACT nao walikuwa na njama ya kuona nccr inakufa mkoani humo lakini mbili ccm walishaonyesha kwa namna yoyote ile lazima majimbo yote ya kigoma yarudi ccm . Kwa hiyo hata hivyo kama si ukawa hata hilo jimbo moja wasingelipata. Naimani cuf na chadema hawawezi kuuwa umoja wao .

Kwa upande wangu Lowasa alikuwa bado ni asset kubwa ndani ya ukawa tatizo ni umri tu hadi 2020 atakuwa na miaka 67, lakini vinginevyo bado angefaa . Intelligensia ya ukawa waanze kutafiti kimya kimya watu sahihi wanao weza kuvaa viatu 2020. huyu mtu awe ambaye amewahi kushika Nyadhifa za juu serikalini na alikuwa mwadilifu, atoke maeneo ambayo yana wapiga kura wengi kama kanda ya ziwa au kaskazini hii itasaidia sana .
 
Nafikiri kwa tulichokiona kwenye uchaguzi huu hata tungemweka mtume au Yesu Kristo wasingeshinda.

Tulikuwa hatutafuti mshindi kwenye uchaguzi huu,tulikuwa tunakamilisha taratibu za tume
 
Endela naye Lowassa mbona Mugabe anadunda, unasingizia umri ongelea afya yake!
 
Bila katiba ya wananchi yenye time huru ya chaguzi na kusimamia maofisa wa serikali kutojihusisha na siasa za vyama cheo cha raisi na utawala ni mali ya CCM
 
Nafikiri kwa tulichokiona kwenye uchaguzi huu hata tungemweka mtume au Yesu Kristo wasingeshinda.

Tulikuwa hatutafuti mshindi kwenye uchaguzi huu,tulikuwa tunakamilisha taratibu za tume

Ni kweli mkuu ila hakuna marefu yasiyo na ncha na kila hila mbaya ina mwisho wake.
 
Vita ni maandalizi na watalaamu wa vita wanasema wakati mzuri wa kujiandaa na vita ni wakati wa amani. Huwezi kushinda kama unategemea wakati wa mapambano ndio uandae silaha. Sasa ni wakati wa kufanya maandalizi ya kutafuta mtu sahihi atakayepeperusha bendera ya ukawa. Ni mtu mjinga anayefikiria muungano wa Ukawa unaweza kuvunjika lakinj ukawa hauwezi kuvunjika kwa sababu vyama vikubwa vyote cuf na chadema wamenufaika mno na umoja huo . Nccr wanaonekana kupoteza kwa sababu ya mazingira yaliyopo kwamba walijiimarisha zaidi mkoa mmoja wa kigoma na ACT nao walikuwa na njama ya kuona nccr inakufa mkoani humo lakini mbili ccm walishaonyesha kwa namna yoyote ile lazima majimbo yote ya kigoma yarudi ccm . Kwa hiyo hata hivyo kama si ukawa hata hilo jimbo moja wasingelipata. Naimani cuf na chadema hawawezi kuuwa umoja wao .

Kwa upande wangu Lowasa alikuwa bado ni asset kubwa ndani ya ukawa tatizo ni umri tu hadi 2020 atakuwa na miaka 67, lakini vinginevyo bado angefaa . Intelligensia ya ukawa waanze kutafiti kimya kimya watu sahihi wanao weza kuvaa viatu 2020. huyu mtu awe ambaye amewahi kushika Nyadhifa za juu serikalini na alikuwa mwadilifu, atoke maeneo ambayo yana wapiga kura wengi kama kanda ya ziwa au kaskazini hii itasaidia sana .
Fanya kazi ulishe familia ysko.
Usiwaze uchaguzi muda wote, inaelekea nyie ndo mnaishi kwa ruzuku na kodi za wabanchi bila kujishughulisha na kujipatia kipato halali.
 
2020 azimeni Kingwangala au Lusinde.
maana mmezoea kuokota wagombea.
 
Ukawa tusishiriki uchaguzi mwingine bila katiba mpya. Kwa katiba iliyopo tutaambulia wabunge wachache ili serikali iwadanganye wafadhili nchi ina demokrasia.
 
Muandaeni huyohuyo mamvi labda atabahatisha. Walau arudishe vinisenti alivyotumia mwaka huu
 
Fanya kazi ulishe familia ysko.
Usiwaze uchaguzi muda wote, inaelekea nyie ndo mnaishi kwa ruzuku na kodi za wabanchi bila kujishughulisha na kujipatia kipato halali.

khaa muibe kura halafu mseme tusijadili,
 
Back
Top Bottom