UKAWA mwisho Nungwi, Zanzibar Wote CUF

UKAWA mwisho Nungwi, Zanzibar Wote CUF

Kamuche

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2010
Posts
368
Reaction score
121
Naomba kuuliza, msinijibu kwa Matusi tafadhali. Hivi Muungano wa UKAWA unaishia kwenye Serikali ya Muungano peke yake? Kule Zanzibar kwa Wawakilisha na Masheikha mbona hatuoni hesabu za Kugawana Majimbo, Masheikha wala Urais? Maana naona Maalim Seif ashapitishwa bila baraka za UKAWA.
 
Naomba wana UKAWA mje mtufafanulie.
 
mbona mbeya yote kapewa chadema ambayo ni sawa na zanzibar husemi ? huko cuf wana nguvu mwenye nguvu shemu ndio anaachiwa jimbo
haha..ni kwamba hajasoma tuu vyema utaratibu wa ukawa...
 
mbona mbeya yote kapewa chadema ambayo ni sawa na zanzibar husemi ? huko cuf wana nguvu mwenye nguvu shemu ndio anaachiwa jimbo

Sijui hawa tutawapa darasa hadi lini, kwa utaratibu waliojiwekea UKAWA. Mgombea atateuliwa kutokana na kujulikana kwake mahali husika. wagombea hawagawani majibo kama chakula cha njaa.
 
Zanzibar nzima ni sawa na jimbo la ubungo, na Cuf kule ndo ina nguvu. Tatizo lako unataka kuilinganisha zanzibar na tanganyika, yaani ni sawa na kulinganisha bahari na kidimbwi. Zanzibar ukipuliza kipyenga nchi nzima wanasikia, zanzibar naweza kuizungukia yote kwa baiskeli- by Kessy
 
Zanzibar nzima ni sawa na jimbo la ubungo, na Cuf kule ndo ina nguvu. Tatizo lako unataka kuilinganisha zanzibar na tanganyika, yaani ni sawa na kulinganisha bahari na kidimbwi. Zanzibar ukipuliza kipyenga nchi nzima wanasikia, zanzibar naweza kuizungukia yote kwa baiskeli- by Kessy

Kwenye Ubunge najua hilo. Kwenye Uwakilisha na Ushekha nako mnapiga Kimya? Unataka kuniambia CDM au NCCR hawana hata uwezo wa Kusimamisha Shekha Zanzibar?
 
Mliosoma, mngenisaidia kuhusu hilo. Je, SMZ ni ya CUF na CCM peke yake?
huwa wanapima majimbo kutokana na uimara wa chama ktk uchaguzi uliopita....km mojawapo ya kigezo.KWa hiyo usitegemee Lema aongolewe, au Sugu, au sehemu NCCR wamekuwa wa kwanza au wa pili toka kwa ccm..
 
Naomba kuuliza, msinijibu kwa Matusi tafadhali. Hivi Muungano wa UKAWA unaishia kwenye Serikali ya Muungano peke yake? Kule Zanzibar kwa Wawakilisha na Masheikha mbona hatuoni hesabu za Kugawana Majimbo, Masheikha wala Urais? Maana naona Maalim Seif ashapitishwa bila baraka za UKAWA.
Anyway usikate tamaa kwa ubunifu wako..ukweli ni kwamba lengo la ukawa si kunyang`anya majimbo ila kuinyang`anya ccm na michepuko yake...
 
Kwenye Ubunge najua hilo. Kwenye Uwakilisha na Ushekha nako mnapiga Kimya? Unataka kuniambia CDM au NCCR hawana hata uwezo wa Kusimamisha Shekha Zanzibar?

Mashekha wanateuliwa na rais
 
Mie naona kwenye UKAWA CUF ndo wanajiamini zaidi, maana wameshatangaza Mgombea Urais Muungano na Mgombea Urais Zanzibar. Washirika wengine naona Kimyaaa!
 
Kwenye Ubunge najua hilo. Kwenye Uwakilisha na Ushekha nako mnapiga Kimya? Unataka kuniambia CDM au NCCR hawana hata uwezo wa Kusimamisha Shekha Zanzibar?

Nafasi ya Sheha huchaguliwa na serikali haigombaniwi na nafasi hii hupewa CCM tu.
CDM Na NCCR hawataki kufanya kama alivyofanya Mrema, Kulisha miezi miwili na kutoambulia kura hata moja
 
Usilolijua ni kama usiku wa giza! Inatosha kujua kuwa CUF ni UKAWA, na wamepewa Visiwa vya unguja na Pemba kwa kuwa ndo wenye nguvu kuliko vyama vingine huko visiwani!
 
Back
Top Bottom