UKAWA mnachanganya wapiga kura...

UKAWA mnachanganya wapiga kura...

ICHIMU

Member
Joined
Jul 25, 2015
Posts
58
Reaction score
12
Ukawa wabishi sana,tuliambiwa kwamba migogoro ndani ya ukawa imekwisha,mbona hapa kahama mjini vyama vyote vimesimika wagombea udiwani?ina maana kura tuzitapanye?jamani eeh!sisi wapiga kura mnatuchanganya!!!!!afu upande wa ubunge nashuhudia Chadema wamesimika jimbo la ushetu,jimbo la kahama mjini,jimbo la msalala..nccr wamesimika ushetu.....duh wapiga kura tutapanye kura?sijajua huko majimboni kwenu.....jadili.
 
Imenisikitisha sana CUF kuweka mgombea ubunge Ilala.Mgombea wa CHADEMA ndio aliyepitishwa na UKAWA
 
Mbatia alisema ndani ya muda mchache Baregu atasawazisha sehemu chache ambazo bado zina matatizo
 
Wewe pigia kura mgombea unayeona anakubalika...
 
Hamna tatizo! mpaka ikifika mwezi wa 10, mtakuwa mmeshamjua ni nani mwenye uwezo kati ya wagombea wa ukawa! Mpeni yule ana nguvu! Katika majimbo ambayo kuna tatizo hilo basi wananchi waangalie ni yupi anauwezo zaidi! Lakini hata hivyo ukawa bado wanafanyia kazi majimbo yaliyo na utata kama huu na wao watatoa msimamo wao na wananchama watapashwa kuufuata huo!
 
Hata Bariadi cuf ina mgombea na chadema ina mgombea. Na matokeo yake ugomvi au upinzani ni kati ya chadema na cuf. Ccm wakishangilia
 
Changamoto kama hizo haziwezi kukosekana hasa katika nchi kama yetu ambayo dola inatumikia chama (ccm).wananchi mpigieni kura mgombea mwenye uwezo na mnayemwamini.
 
Kila mtu anatafuta ugali wake. Hivi wewe utakuwa uko tayari kumuachia mwingine tu agombee wakati kwenye ubunge

ukifanya kazi kwa 5 years unakula kama 300mil. Waache watu wapambane kutafuta mlo wao. Ni wanasiasa wachache sana

wenye malengo na wewe mwanachi wa kawaida wengine wengi wako kimaslahi zaidi.
 
Back
Top Bottom