Ukawa Kurudi Bungeni?

Ukawa Kurudi Bungeni?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,051
Reaction score
34,788
10351660_540608599379192_1913927804198506778_n.jpg
 
Akizungumzia mustakabali wa Ukawa kwenye Bunge la Katiba baada ya kuwepo wito wa watu mbalimbali, wakiwamo za viongozi wa dini, Mbowe alisema kuwa watu wanatafsiri vibaya kuwa wajumbe wa umoja huo wanagoma kurejea kwenye Bunge la Katiba, kinachotakiwa ni kuangalia sababu gani zinawafanya kushikilia msimamo huo.

<!--Ads and Related Buttons--> <!-- Ads minus related Buttons --> Alifafanua kuwa wakati wanagomea Bunge la Katiba walikuwa na sababu za msingi na bado zipo, hazijatatuliwa wala hazijafanyiwa kazi. Kwa maana hiyo, kwa kuwa hazijafanyiwa kazi na hazijatatuliwa, wataendelea kubaki nje ya Bunge.

<!--Ads and Related Buttons--> <!-- Ads minus related Buttons --> Hata hivyo, Mbowe alisema kuwa msimamo wao kugomea Bunge la Katiba siyo wa kudumu kwani unasababishwa na mazingira.

<!--Ads and Related Buttons--> <!-- Ads minus related Buttons --> "Watu wakae chini, watathmini, waangalie matatizo yako wapi na tutatue matatizo mapema na yakikamilika, watu watarejea bungeni. Lakini hatuwezi kurudi pale kwenda kutukanana, kunyanyasana na kuvunjiana heshima. Haileti maana kabisa, kitu ambacho si malengo ya Bunge la Katiba.

Mbowe amshangaa Pinda kuhusu Ukawa - Kitaifa - mwananchi.co.tz

 
Nina uhakika watarudi tu

Sioni kama watakomaa muda mrefu sana
 
Nawaunga mkono UKAWA wasirudi mpaka mada itakayo jadiliwa iwe ni mswaada kutoka kwa WANANCHI na sio kutoka kwa MAGAMBA!
 
Ni lazima wakubaliane kwanza nini kitajadiliwa iwapo watarudi bungeni ama sivyo ile sinema ya awali itajirudia!!
 
Wanaosema UKAWA warudi bungeni hawaelewi nini mantiki yao. Kwa kifupi sana, angalia Bunge la Bajeti linavyopitisha mambo yake. Kwa vile ukiisha saini kuwa umehudhuria, basi utake usitake hata kama ukatae kwa sauti ya kupasua spika "HAPANA", bado utaburuzwa na sauti za wanafiki wanaosema "NDIYO". Na hapo utakuwa umebariki kupishwa huko kwa suala husika.

Hivyo ili UKAWA wajisafishe na kuonekana hawakushiriki kubariki ukoloni, ni bora waendelee kubaki nje ya BMK na ccM wapitishe ajenda zao peke yao. VIVA UKAWA VIVA!
 
Mkuu Bulldog, bila malalamiko yao kushughulikiwa basi kurudi kwao itakuwa ni kupoteza muda tu na MACCM ndiyo yatapata nguvu ya kutoa matusi ya nguoni, kashfa, kejeli na kuzomea kwa nguvu zote ili kukwamisha upatikanaji wa katiba ambayo Watanzania wengi tunaitaka.

Nina uhakika watarudi tu

Sioni kama watakomaa muda mrefu sana
 
Mkuu Bulldog, bila malalamiko yao kushughulikiwa basi kurudi kwao itakuwa ni kupoteza muda tu na MACCM ndiyo yatapata nguvu ya kutoa matusi ya nguoni, kashfa, kejeli na kuzomea kwa nguvu zote ili kukwamisha upatikanaji wa katiba ambayo Watanzania wengi tunaitaka.

Shida kubwa ya watanzania ni kukosa msimamo.

Angalia maandamano mengi wanayoitisha mwisho wa siku wanaishia ku-surrender
 
je,Umoja wa katiba ya wananchi(UKAWA) watarudi bungeni tena kutetea katiba ya wananchi au bado mgomo uko palepale?
wapendwa mna jua katiba bila ukawa(chadema,cuf,nccr mageuzi) haitakuwa katiba bora?
Yaani cjuhi nchi ye2 inako elekea maana yawezekana kuna khali ya hatari apo mbeleni ya2 pasa kumwomba mungu atuepushe na majanga haya(mvutano katika siasa)
 
Ukawa wakirudi bungeni bila makubaliano maalumu namna ya kuheshimu maoni ya wananchi watakuwa wamejivunjia heshima yao dhidi ya umma wa kitanzania!
 
CCM waende KIZOTA kuandika katiba mpya. Maana haya ni maigizo, kama walikuwa wanakatiba yao mpya kwa nini waliunda kamati ya Warioba na bunge la katiba? Wanafuja pesa bure. Kama ni maoni ya Chama si tayari walishayapeleka kny kamati? Mbona hata sisi maoni yetu hayapo kny rasimu? Lkn kamati haikuyaandika? Kama kuwafuta wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa. Lkn tumeridhika kwa sababu tupo wachache wenye wazo hilo. Nao CCM wakubali matokeo lkn si kuibadili Rasimu.
 
Back
Top Bottom