Suala la kusimamisha mgombea mmoja kwa kile kinachoitwa UKAWA katika majimbo ya uchaguzi katika ngazi za udiwani, ubunge na hata urais ni jambo muafaka. lakini hebu fanyieni kazi jambo hili muhimu saaana.
Utaratibu wa uwakala:
Mawakala wa uchaguzi katika vituo nya kupigia kura wanaruhusiwa wale tu wenye wagombea. Chama kisicho na mgombea hakiruhusiwi kuweka wakala. Hii inamaana UKAWA wakimteua mgombea kutoka NCCR katika udiwani, katika kata husika kila kituo kitakuwa na wakala mmoja tu wa NCCR, na huyu ndiye atakuwa mlinzi wa kura za diwani huyo.
Jinsi ya kuibiwa kura kwa wakala mmoja.
1. Endapo huyo wakala akiwa mbinafsi, au mroho wa pesa anaweza kushawishiwa kirahisi akauza kura.
2. Akitoka tu kwenda haja, atakuta kura za ziada za CCM zimeishajazwa ndani ya box au box limebadilishwa.
3. Mtu mmoja ni rahisi kumbabaisha wakati wa kuhesabu kura na akapoteza kile alichotakiwa kufanya.
Kupoteza jimbo au udiwani kwa mgombea mmoja wa UKAWA na kipa CCM ushindi wa bila kupingwa
Kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza kiti cha udiwani au jimbo la ubunge katika hali ifuatayo:
1. Mgombea akitekwa na wana CCM muda mfupi kabla ya kurudisha na kuachiwa baada ya muda kuisha.
2. Mgombea akiamua kusaliti akala pesa ya CCM akaingia mitini baada yakurushwa form.
3. CCM kuweka pingamizi kwa huyo mgombea mmoja na tume ya uchaguzi ikakubaliana nalo.
Njia ya kutokea.
Kwa maoni yangu napendekeza yafuatayo:
1. Kuhusu uwakala, chama kilicho achiwa jimbo na nafasi ya udiwani kiweke wagombea wasindikizaji kwa tiketi ya vyama vingine. Maana yangu ni kwamba kama jimbo wameachiwa NCCR. mgombea halisi wa NCCR ni A. NCCR iteue wagombea wasindikizaji B ajifanye CHADEMA, C ajifanye CUF, D ajifanye NLD. wachukue form za kugombea na uongozi wa vyama vya CHADEMA, CUF, NLD wawapitishie form zao. Hawana haja ya kupiga kampeni. Watawezesha kituo kimoja cha kupiga kura kuwa na mawakala wanne. Kuwaibia kura mawakala wanne ningumu kidogo. Hii ifanyike kwa ngazi ya kata tu. katika ubunge mawakala hawa ndio watasimamia kura za mbunge.
2. Kuhusu Mgombea mmoja, kuwepo ulinzi madhubuti kwa wagombea siku za kurejesha form. Ikiwezekana awepo mgombea wa ziada wa chama kilichoachiwa jimbo. achukue form kwa ticketi ya chama kingine na apige kampeni ya kuwaomba wananchi wampigie yule mlengwa. endapo ikitokea masuala ya mapingamizi na usaliti, huyu wapili aendeleze mchezo.
​
Toa ushauri zaidi.
Utaratibu wa uwakala:
Mawakala wa uchaguzi katika vituo nya kupigia kura wanaruhusiwa wale tu wenye wagombea. Chama kisicho na mgombea hakiruhusiwi kuweka wakala. Hii inamaana UKAWA wakimteua mgombea kutoka NCCR katika udiwani, katika kata husika kila kituo kitakuwa na wakala mmoja tu wa NCCR, na huyu ndiye atakuwa mlinzi wa kura za diwani huyo.
Jinsi ya kuibiwa kura kwa wakala mmoja.
1. Endapo huyo wakala akiwa mbinafsi, au mroho wa pesa anaweza kushawishiwa kirahisi akauza kura.
2. Akitoka tu kwenda haja, atakuta kura za ziada za CCM zimeishajazwa ndani ya box au box limebadilishwa.
3. Mtu mmoja ni rahisi kumbabaisha wakati wa kuhesabu kura na akapoteza kile alichotakiwa kufanya.
Kupoteza jimbo au udiwani kwa mgombea mmoja wa UKAWA na kipa CCM ushindi wa bila kupingwa
Kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza kiti cha udiwani au jimbo la ubunge katika hali ifuatayo:
1. Mgombea akitekwa na wana CCM muda mfupi kabla ya kurudisha na kuachiwa baada ya muda kuisha.
2. Mgombea akiamua kusaliti akala pesa ya CCM akaingia mitini baada yakurushwa form.
3. CCM kuweka pingamizi kwa huyo mgombea mmoja na tume ya uchaguzi ikakubaliana nalo.
Njia ya kutokea.
Kwa maoni yangu napendekeza yafuatayo:
1. Kuhusu uwakala, chama kilicho achiwa jimbo na nafasi ya udiwani kiweke wagombea wasindikizaji kwa tiketi ya vyama vingine. Maana yangu ni kwamba kama jimbo wameachiwa NCCR. mgombea halisi wa NCCR ni A. NCCR iteue wagombea wasindikizaji B ajifanye CHADEMA, C ajifanye CUF, D ajifanye NLD. wachukue form za kugombea na uongozi wa vyama vya CHADEMA, CUF, NLD wawapitishie form zao. Hawana haja ya kupiga kampeni. Watawezesha kituo kimoja cha kupiga kura kuwa na mawakala wanne. Kuwaibia kura mawakala wanne ningumu kidogo. Hii ifanyike kwa ngazi ya kata tu. katika ubunge mawakala hawa ndio watasimamia kura za mbunge.
2. Kuhusu Mgombea mmoja, kuwepo ulinzi madhubuti kwa wagombea siku za kurejesha form. Ikiwezekana awepo mgombea wa ziada wa chama kilichoachiwa jimbo. achukue form kwa ticketi ya chama kingine na apige kampeni ya kuwaomba wananchi wampigie yule mlengwa. endapo ikitokea masuala ya mapingamizi na usaliti, huyu wapili aendeleze mchezo.
​
Toa ushauri zaidi.