UKAWA chini ya Lowassa, Sumaye, Kingunge kukwamisha Katiba ya Warioba; Mbowe&Maalim Seif Jitumbueni!

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Igwe wanaJF!

Nimewajibika kuandika hii hoja nikiwa na mtanziko kwanini Mbowe na Seif wanakabidhi "chungu" kwa hawa maveterani ambao hawana mbinu mpya za kivita?

Naum,Kingunge kipindi cha bunge maalum la katiba aliibuka bungeni kama "mshauri" wa waganga wa tiba asili na kimkakati akapewa muda mrefu kutoa nasaha za Muungano na kuchinjilia mbali tunu za taifa.Sina shida na idadi ya serikali bali hapa kwenye tunu ilikuwa ni mahsusi kuondoa ili kijana wake akichukua nchi asifatwefatwe..Je huyu ana uhalali wa kuanza kuponda katiba pendekezwa ya bunge la katiba?..Je akiyakana maneno yake ataaminika?...Ieleweke tu Kingunge anashawishiwa awe mlezi wa BAVICHA...Je nia ya Kingunge UKAWA ni Katiba mpya au Lowassa awe Raisi.

Ushiriki wa Lowassa katika mchakato wa kukwamisha tume umeelezewa mara kwa mara na wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Katiba kwani aliamini yeye ni Raisi ajaye..na aliitaka tume Mamlaka ya Raisi wa JMT kuhusu Zanzibar yaongezwe.Je huyu ataaminika?..Je dhumuni lake ndani ya UKAWA ni Uraisi au Katiba mpya?...Ikumbukwe kishajitangaza ndiye Mgombea wa Uraisi wa CHADEMA 2020.

Sumaye,huyu ni mjumbe wa kamati kuu chadema kama Lowassa.Huyu alikuja CHADEMA kumnadi Lowassa na kingine.Msimamo wake juu ya katika mpya ni Serikali 2.Je amebadilisha mtazamo wake kuwa serikali 3?

Kati ya wote watatu hamna hata mmoja anayefanana na maono ya UKAWA ambaye mwenyekiti wake mwasisi ndani ya Bunge la katiba ni Prof.Lipumba na Katibu wake Mtatiro.Je wanaweza kumshawishi nani juu ya katiba?

Mbowe na Maalim Seif na Mbatia ndio mliobaki na UKAWA iliyo na lengo moja tu la kupata madaraka na sio kushawishi upatikanaji wa Katiba mpya yenye maridhiano.Ni kwanini msijitumbue wenyewe?Hivi hamjui mmejidhalilisha kisiasa kwa kukubali vijihela kwa kuuza nafasi za kugombea uraisi na ubunge?

Tutoe hoja kinzani na sio matusi.

Nawasilisha
 
Sijakuelewa labda kama utatumia lugha nyingine nitakuelewa.
 
Kwa nini usieleze kukwama kwa katiba ya mzee warioba ikiwa ni pamoja na ccm wenyewe kuikwamisha, ila umeegemea upande wa wale waliokiama chama hicho?
 
Historia haitawaacha salama.Kingunge aliweka wazi msimamo wake unaoenda kinyume na katiba ya Warioba iliyopendekezwa na wananchi.
Watu wa LHRC walijionea jitihada za Lowassa kukwamisha katiba ya Warioba walipokwenda Monduli.
Bango kitita lina kumbukumbu za maandishi ya hawa wasanii.Ipo siku mwisho wa usanii wao utafika.
 
Siasa za kinafiki zimehamia ukawa. Kabla ya gia kubadilishwa angani, chadema iliaminiwa kwa misimamo thabiti ya maadili na sera. Hivi sasa chadema (ukawa) hakuna tofauti na ccm.
 
Kwa nini usieleze kukwama kwa katiba ya mzee warioba ikiwa ni pamoja na ccm wenyewe kuikwamisha, ila umeegemea upande wa wale waliokiama chama hicho?
Kwa nini usieleze kukwama kwa katiba ya mzee warioba ikiwa ni pamoja na ccm wenyewe kuikwamisha, ila umeegemea upande wa wale waliokiama chama hicho?
Kuwapa usukani kuiwakilisha ukawa ni kurudi hatua 100 nyuma.
 
Nani aliikubali?? Magufuli,Samia Suluhu,Majaliwa,January,Nape??? Shida za hii nchi zinatoka ccm....ulitaka waende kinyume na maagizo ya chama....mbona we unatumwa hapa kila siku kutetea upuuzi wa chama chenu kwa maagizo au ili upate buku saba....na hakuna siku umewahi kwenda kinyume na maagizo ya chama.....KAMA WEWE KIBARAKA TU UMESHINDWA,UNADHANI ALIYEKUWA ANAUTAKA URAIS KWA CHAMA HICHO HICHO ANGEPINGANA NACHO????? THINKING BANGI
 
..Dr.Mwakyembe, waziri wa sheria na katiba alisema katiba mpya siyo kipaumbele cha serikali ya Raisi Dr.Magufuli.

..zaidi Mwakyembe alikuwa kati ya vinara wa kupinga katiba pendekezwa ya Jaji Warioba.

..kwa hiyo utaona kabisa kwamba kwa upande wa Tanganyika suala la katiba mpya ni next to impossible.

..ukiangalia upande wa Znz hali ni mbaya zaidi. Ndani ya baraza la wawakilishi kuna watu wenye misimamo mikali kama Balozi Karume.

..Vilevile hali ya kisiasa Znz siyo nzuri kuwezesha mchakato wa katiba mpya.

..kwa maoni yangu, suala hili lipo nje ya uwezo na ushawishi wa Chadema, pamoja na hao uliowataja.
 
Joka kuu nimekuelewa.Ila picha ilivyo kuwaweka hao watu mbele wanaweza kuzungumzia suala la katiba ya Warioba kwa kuiunga mkono hasa ukizingatia tabia zao siku za nyuma.
 
Hahahahahaha!!! Lowassa umewahi sikia mdomoni anaongelea katiba mpya?? Kila akiongea anaongea urais. Iwe mchana au jioni na usiku anaota urais.

Ndo maana amejiandaa kugombea 2020.
 
Nani aliikubali?? Magufuli,Samia Suluhu,Majaliwa,January,Nape??? Shida za hii nchi zinatoka ccm....ulitaka waende kinyume na maagizo ya chama....mbona we unatumwa hapa kila siku kutetea upuuzi wa chama chenu kwa maagizo au ili upate buku saba....na hakuna siku umewahi kwenda kinyume na maagizo ya chama.....KAMA WEWE KIBARAKA TU UMESHINDWA,UNADHANI ALIYEKUWA ANAUTAKA URAIS KWA CHAMA HICHO HICHO ANGEPINGANA NACHO????? THINKING BANGI
Dogo ninachokwambia sibishi kuwa CCM walipendekeza yao,Je UKAWA chini ya Lowasa&co wataweza kuishinikiza CCM kubadili msimamo?
 
So hapa ni kama unawalaumu UKAWA kukosekana katiba mpya?!! Ni ukilaza tu unakusumbua ama kuna kingine?!!
 
Kwa maoni yangu, sisi watanzania tunahitaji kwanza huduma za jamii zilizo bora na nidhamu katika utumishi wa umma. Huwezi kuzungumzia katiba mpya huku watu hawana maji, umeme, huduma duni za jamii na ufisadi ukiwa umetanda kila kona. Ndiyo maana mimi naunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuanza kwanza kupambana na ufisadi na kuonesha nia ya kuboresha mienendo kadhaa katika nchi yetu.
 
Back
Top Bottom