Ukatili kwa watoto wetu mpaka lini?

Mulhat Mpunga

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
27,263
16,288
Habari wanajamvi,

Vitendo Vya Ukatili Kwa Watoto Vmekuwa Ni Jambo La Kawaida Siku Hizi.

Mtoto John William Wa Miaka 4, Huko Geita,amefariki Dunia Baada Ya kupata Kipigo Kwa Kuchelewa Kumfungulia Mlango Baba yake Aliporudi Usiku
Mtoto Huyo,Alicharazwa Viboko Mwili Mzima,Akapigwa Mangumi Na Mateke.

Akapewa Adhabu Ya Kuzunguka Nyumba Yao Usiku Huo Mara Kadhaa Na Kisha Kupakwa Pilipili Machoni Ambapo Adhabu Hizo Zilipelekea Mtoto Huyo Kupoteza Maisha.

Source: The Citizen 26

My take;

Hivi Katika Hali Ya Kawaida Mtoto Wa Miaka 4 Ni Wa Kumfungulia Mtu Mlango Usiku Wa 8?

Jaman Ifike Mahali Tuwe Walinzi Wa Hawa Watoto Wanaumizwa Na Kuathiriwa Kisaikolojia Na Hawa Wazazi Wapuuzi,mda Huo Unakuta Hilo Zee Limelewa Anakuja Kumtesa Mtoto Kiasi Hichi!

Ukiona Mtoto Wa Jirani Yako Anapata Mateso Kama Haya Ni Bora Kumshtaki,mi Wakwangua Akiwa Na 4 Years Nadhani Bado Atakuwa Anabebwa Mgongoni.

Hainiingii Akilini Ndo Mfungua Mlango Usiku Huo Ambapo Watoto Wenzake Wanakuwa Usingzini Wanaota Ndoto Jamani Inauma Sana Kuwakatisha Watoto Maisha.
=====================================





Chanzo: http://www.fikrapevu.com/ukatili-ba...oni-amchapa-viboko-ngumi-na-mateke-hadi-kufa/
 
Jamani wandugu tukumbuke kwamba kuna sababu kubwa inayosababisha ukatili huu kutesa watoto kutokea.
1.Kufunjika kwa ndoa(hii hupelekea mtoto kupata malezi yasio na uhakika wa upendo toka kwa mzazi mmoja tu.

2.Kufariki kwa wazazi(hii hupelekea mtoto kulelewa na ndugu au jamaa wengi wao wasio na huruma na mapenzi kwa mtoto.

#Tujitahidi kuzitunza na tudumu ktk ndoa zetu na pale penye dosari ni vyema tujirekebisha kwa faida ya malezi kwa watoto wetu.
#Pia tuwe na mioyo ya upendo kwa watoto tunaowalea waliotokana na kufariki kwa wazazi wao.
 
Nadhani watu tunatofautiana sana tena sana kama vile mbingu zinavyotofautiana na dunia maana haya mambo nikiyasikia najiuliza sana kama hawa wanaofanya haya ni watu wa kawaida, majuzi yule mama wa Morogoro na mume wake walivyomtesa mtoto wa dada yake(mwenye umri wa miaka minne) kwa kumfungia ndani mpaka mtoto akadhoofika kiasi kile sasa linakuja hili la huyu wa Geita dah! Nasikitika sana kuona ukatili kama huu ukifanyika kwa watoto ambao wanahitaji kuonyeshwa upendo mkubwa sana kweli nasikitika sana na huzuni kunijaa sana moyoni kwa matukio kama haya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…