Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Tatizo la Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari limeendelea kuwa sugu siku kwa siku. Serikali imekuwa ikijatahidi kujitetea kwamba tatizo ni ufinyu wa bajeti na hivyo Walimu waendelee kuvumilia mpaka hapo hali ya kifedha itakapokuwa nzuri.
Lakini cha kushangaza bajeti ya kukuarabati Ikulu kila mwaka huwa inapatikana bila matatizo yeoyote kwa kuwa Ikulu ni mahali patakatifu pa patakatifu.
Kwa mfano tangu Serikali ya awamu yanne iingie madarakani takribani bilioni 17 zimetumika katika kukarabati Ikulu.
Kwa mfano,tazama jedwali hili
Mwaka na kiasi cha pesa
2006-2007 - 6,114,562,685
2007-2008 - 5,596,900,000
2008-2009 - 5,712,000,000
Pesa hizi kwa Mwaka zingejengwa Nyumba nzuri za Walimu 611 na chenji inarudi.
Hivyo basi kwa kipindi chote cha miaka mitati jumla ya nyumba 1833 zingejengwa na wala tusingekuwa na tatizo kubwa la nyumba za walimu.
Hoja zangu za msingi:
Lakini cha kushangaza bajeti ya kukuarabati Ikulu kila mwaka huwa inapatikana bila matatizo yeoyote kwa kuwa Ikulu ni mahali patakatifu pa patakatifu.
Kwa mfano tangu Serikali ya awamu yanne iingie madarakani takribani bilioni 17 zimetumika katika kukarabati Ikulu.
Kwa mfano,tazama jedwali hili
Mwaka na kiasi cha pesa
2006-2007 - 6,114,562,685
2007-2008 - 5,596,900,000
2008-2009 - 5,712,000,000
Pesa hizi kwa Mwaka zingejengwa Nyumba nzuri za Walimu 611 na chenji inarudi.
Hivyo basi kwa kipindi chote cha miaka mitati jumla ya nyumba 1833 zingejengwa na wala tusingekuwa na tatizo kubwa la nyumba za walimu.
Hoja zangu za msingi:
- Hivi ni kwanini Ikulu ikarabatiwe kila Mwaka?
- Ni kwanini ikarabatiwe kwa pesa yote hiyo?