Ukaccm vs ukawa

Serikali mbili au tatu ni kipengele tu ndani ya Katiba Mpya, hakiwezi kuvuruga Mchakato, labda kama Wapinzani wao wanafikri Katiba mpya ni mjadala juu ya aina ya serikali.

hayo ni mawazo yako mgando ya kiCCM. juzi kikwete kaongea hoja ngapi bungeni? hukumsikia akiwatetea wazanzibar kwa kuvunja muungano baada ya kuunda nchi ya Zanzibar kutoka kwenye muungano wa awali?
 
Umeandika vema, nimekuelewa.
 
Mashirika ya kimataifa hayana nafasi katika mstakabali wa Taifa letu.

mashirikaka gani unayoongelea ndugu yangu? na yamekuwaje na mustakabali wa nchi? nahishi elimu ya shule za kata itakuwa imekuathiri ubongo wako, sio bure!
 

mkuu, CCM hawakatazwi kutoa maoni yao, kama ilivyo kwa makundi mengine. tatizo ni pale CCM wanapolazimisha mawazo yao ndiyo iwe katiba mpya. wanakuja na hoja ya serikali 2 ambayo haimo kwenye rasimu ili iweje? kwanini wasitoe maoni jinsi ya kuboresha serikali 3 badala ya kuzipinga? hoja ya serikali 2 haimo kwenye rasimu. kwa nn CCM wanataka kuichomeka kwenye rasimu?
 
Tatizo la CCM ni kupinga kila kitu kilichomo kwenye rasimu. Hayo yaliyomo kwenye rasimu ndiyo maoni ya wananchi. Sasa kama CCM wanayakataa kulikuwa na haja gani kuunda tume kutafuta maoni ya wananchi? Na kuna haja gani ya kuendelea na mchakato wa uundaji wa katiba? Tunapoteza muda na fedha za wananchi bure!
 

UKAWA NAWAAMINI SANA WANALINDWA NA NGUVU YA UMMA WANASEMA NGOJA MJADALA UANZE ,HOJA ZA ------ NI DHAIFU SANA NA ZOTE ZINAJIBIKA KIRAHISI SANA HAZIWEZI KUSHINDANA NA ZA WARIOBA said (UKAWA TEAM)
 
Mimi bado naamini CCM ndiyo itakatupa Katiba zuri, wana nia ya dhati na Muugano wetu.

CCM inawanachama milioni tano tanzania nzima,na tanzania ina kadiliwa kuwa na idadi ya watu milioni 45 so toa milioni 5 ya CCM wanabaki milioni 40 so interest za watu milloni 4 haxiwezi kukandamiza hawa milioni 40
 
serikali tatu haziepukiki kuna mambo mengi hayakuingizwa kwenye rasimu hii kwa kuwa siyo mambo ya muungano na kwa kuwa rasimu hii ni ya serikali tatu

tume imeyaacha makusudi ili yaende kwenye katiba za nchi washirika wa shirikisho, mfano mambo kama aridhi, kodi, elimu maliasili madini,

ukilazimisha serikali mbili inabidi urudi tena ili kujumuisha mambo ya muungano na yasiyo ya muungano kwenye katiba moja,

hii haiwezi kuwa kazi ya bunge maalumu la katiba kisheria inagoma kabisa.

sijui kama CCM hilo wanaliona, maana yake ni kwamba tume irudi tena kwa wananchi mara ya pili, kitu ambacho ni kupoteza muda kwa kutafuta matokeo ambayo hayabdiliki
 
basi tuambie tatizo la muungano lipo kwa kiasi gani na utushawishi kwa hoja mpaka tukuelewe. na hiyo 80% uliyoipachika kwenye maelezo yako ni kitu gani na umeipataje? usikariri kila jambo kama kasuku.

Mkuu naona Hotuba maridadi ya JK imekupiga chenga! Hiyo 80% imeelezwa humo, sina haja ya kurudia rudia! Muungano una matatizo, lakini solution sio kuongezea tena tatizo kwa kuunda nchi mbili zijipachike ndani ya nchi moja! Tukifanya hivyo Historia itatuhukumu milele!!
 
Serikali mbili au tatu ni kipengele tu ndani ya Katiba Mpya, hakiwezi kuvuruga Mchakato, labda kama Wapinzani wao wanafikri Katiba mpya ni mjadala juu ya aina ya serikali.

UKAWA wanafikiri Katiba mpya ndio tiketi ya kwenda Ikulu!
 

mkuu, wananchi wanataka serikali 3. sasa serikali 2 unazongangania ni za nani? hicho kikundi kinachotaka serikali 2 waende wakaziingize kwenye katiba ya kikundi chao. katiba ya wananchi inayojadiliwa bungeni ni ya serikali 3.
 

Solution yake ni nini kumbe?
Z

Una hakika kwamba muungano huu sio wa nchi mbili ndani ya nchi moja? Kwani hujui kwamba Zanzibar ni nchi?
 
Tatizo hapa ni baadhi ya watu kutokufahama mantiki ya hoja zao. Kuna baadhi wanadhani hoja zao ndiyo za wananchi bila kufahamu kuwa CCM ni sehemu ya wananchi.

CCM, kama baraza la katiba, ilishatoa maoni yake tayari na yakaingizwa kwenye rasimu. Sasa wasubiri wajumbe wa bunge la katiba wayafanyie kazi. Kwanini wanataka kulazimisha mambo ambayo hayamo kwenye rasimu inayojadiliwa bungeni yaingie kwenye rasimu. Suala la serikali 2 halimo kwenye rasimu. Kwanini wanataka kuliingizamo kimabavu? Huoni kwamba wanatishia uhai wa bunge la katiba?
 
Na ni kwa nini pia wengine wang'ang'anie kura ya siri... na ule umoja unaitwa Tanzania Kwanza na si ukaccm hii ni yako... mwanauzi usiweke ushabiki weka hoja yenye mantiki na watu wachangie kwa hoja lakini si kutoa hoja elekezi kwa yale tu unayotaka wanauzi huu wajielekeze.
Asante!
 
Tujikite kuhamasisha watu waikatae hiyo katiba ya CCM itakapokuja kura ya maoni
 

Acheni unafiki serikali yenu ndiyo iliyoratibu suala zima la tume ya maoni mwanzo mwisho je hamkuona umuhimu wa kuchukua maoni ya hiyo 80% au yanakuwa na umuhimu kwenu kwa kuwa matakwa yenu hayajatimizwa? je ingekuwa hao mnaodai ni wachache wamependekeza serikali 2 mngetoka kusema 80% hawakusema juu ya muungano, hakika mwisho wenu umefika hamtashinda nguvu ya umma nyamazeni waacheni wananchi watengeneze katiba yao:tape:
 

Matatizo ambayo ccm imeshindwa kuyatatua ndani ya miaka 50 na yanazidi kuongezeka kila uchao wapisheni wananchi wafanye maamuzi magumu juu ya maslahi yao na vizazi vyao vijavyo sio kumfurahisha ------😛eace:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…