Ujuvi wa siri na mapokeo ya imani

Jul 18, 2020
14
12
Na: Norbert Mporoto
28.02.2021

“Allah amefaridhisha mambo ya dini kwa hivyo usiyapuuze. Vilevile kaweka mipaka usiikiuke, amekataza baadhi ya mambo kwa hivyo usiyafanye. Yale aliyoyanyamazia ni kwa ajili ya huruma zake kwako wala hakusahau kwa hiyo usiyadadisi”

Ni maneno mazuri yenye kubeba dhamiri ya imani zetu, ili mioyo yetu itulie tukisubiria kuuona ufalme wa mbingu. Naomba nikiuke kidogo misingi ya imani zisizo asili yetu kwa kuanza kufanya udadisi juu ya uhusiano wetu wa kibinadamu na dini hizi, ambazo zinaongozwa na misahafu kama katiba yake.

Kama ilivyo katika uongozi wa taasisi, jamii, au taifa lazima kuna sheria na taratibu ambazo zinatumika kama mwongozo, na asili yake ikiwa ni katiba ambayo ndiyo mkusanyiko wa sheria hizo. Hivyo, imani zetu kupitia dini huongozwa na misahafu anuai kulingana na muktadha wa dini husika. Kuzungumzia dini ya mtu kwa uzuri au ubaya si jambo la kiungwana hata kidogo, lakini kukiuka misingi ya dini ili kukosoa (kulingana na mienendo husika), kuokoa na kurekebisha hatma za waumini katika imani zao ili kutafuta mwafaka mwema katika jamii zao ni jambo sahihi ambalo makala hii inalenga kujadili kwa kina.

Kiuhalisia dini ni jukwaa linalowakusanya watu wa imani moja chini ya mwamvuli unaosimamia na kuainisha sheria, kanuni, miiko, na taratibu ambazo huakisi utamaduni na asili yao wakati wote wanaposimama kuitetea kwa kuabudu, na kuidhihirisha imani yao. Lakini kwa maana iliyopoteza umaana wake katika mapokeo yaliyofanywa na wengi wetu ni ile inayoakisi dini kuwa imani. Awali kabla ya mapokeo ya imani au dini hizi kulikuwapo na imani zetu asilia (kote barani Afrika). Mapokeo ya imani kiukweli hayakuzingatia muktadha na hatma yetu, ila tu wapokeaji hawa waliweza kuzipokea kama m’badala wa imani zao zilizoitwa za kishenzi na zilizojaa uovu na matendo yanayosadikika kuwa ya kishetani. Labda! Kwa kifupi, walianzisha safari isiyoweka bayana mwelekeo wake, na baadae kukosa ufahamu wa kuona mbali kusawili matokeo ya kinachofanyika kwa kivuli cha imani hizo.

Uwezo hafifu wa kung’amua kilichopo ndani ya mapokeo hayo na matokeo yake unatokana na mfumo uliotumika na waliozileta imani hizo. Mbinu hizo zilimdhoofisha mpokeaji na kumuaminisha kuwa hakuna imani ya kweli zaidi ya hiyo, hivyo msingi huu m’bovu umetujenga kuwa na akili fupi za kutoweza kuamua nini hatma yetu dhidi ya mataifa anzilishi ya imani hizi.

Jambo ambalo ni kosa, ni kushindwa kung’amua kuwa imani ya watu fulani hubeba utamaduni wa watu husika, hivyo hata akipewa mtu mwingine aiendeleze imani hiyo hawezi endana nayo kamwe. Ni shughuli ngumu ya kumpaka rangi punda ili ageuke kuwa pundamilia wakati inafahamika wazi kuwa mvua ikinyesha atairejea asili yake ya kuwa punda. Na hivyo ndivyo ilivyo kwetu sisi tuliopokea imani hii, na tumeshindwa kuendana nayo kiasi kwamba imani hizi zimegeuka kuwa zimwi linalotutafuna kila uchao.Lakini upande wa pili kwa waliotuletea imani hizi kwao ni furaha na shangwe mithili ya ngedere waliovamia shamba la mahindi maana hawana uchungu nayo, wala hawaumii kwani hawajui hata gharama na kiasi cha jasho lilichomwagika kufikia hatua hiyo.

Kitendo cha kuridhia kupokea imani zao, ni kuruhusu mataifa yetu yaenende katika mwongozo wa tamaduni mbili tofauti. Lakini tamaduni hizi mbili haziwezi pikika katika chungu kimoja, hivyo chokochoko na mitafaruku inayoendelea barani Afrika kwa namna moja au nyingine inatokana na ugeni wa tamaduni za kiimani tulizobebeshwa, na kuzivaa haswa kanakwamba ni asili yetu, kiasi cha kushindwa kuimudu mihemko yetu juu yake na hata kutizamana kama maadui wa kiimani.

Leo hii Afrika, dini imekuwa mithili ya dawa za kulevya zenye madhara zaidi ya bangi na mirungi (yapasa itumike fikra ili uweze kutambua ukweli huu, na tuweke kando hisia zetu). Imani za dini tulizopokea zimeathiri watu wetu kifikra, zimejenga hofu na woga na zaidi dini hizi zinatafuna mihimili ya mataifa yetu, yaani aliyeleta ukoloni ndiye aliyeleta dini hivyo shabaha ya mkoloni bado iko palepale kupitia mwamvuli wa dini tulizopokea. Hivyo tunautukuza ukoloni katika namna tusiyoielewa!

Kupitia mikononi mwa waanzilishi wa dini hizi, dini zimekuwa zikichochea mapigano baina ya waafrika. Kwa sababu za kutengenezwa, historia ya bara la Afrika inaonyesha namna ambavyo baadhi ya nchi zimekuwa zikikumbwa na kashfa ya mapigano ya kidini. Japokuwa ukweli wake ni kwamba mapigano hayo yanasababishwa na imani ya uadui ambavyo mizizi yake imetokana na mataifa anzilishi wa dini hizo kwa kutizama watu wa dini moja kuwa na uhasama na watu wa dini nyingine, kitu kinachopelekea kuvunjika kwa umoja baina yao na kushamiri kwa mapigano ya kidini.

Mapigano haya hayakuwepo kipindi babu zetu wakisali chini ya mti ama kipindi tunatambika; kipindi ambacho hizo imani zetu zinazoitwa za kishezi na zenye unasaba na ushetani zikiwa zinatumika. Kamwe hatukuwahi kupigana kisa huyu anatambika chini ya mti au yule anatambika juu ya jiwe. Kwanini leo hii kuwe na mapigano? Tumetoa wapi hizi tabia za kishenzi kwenye dini tulizoaminishwa eti ni za watu safi na werevu? Kwanini dini za sasa hazihubiri upendo katika matendo? Kati ya hao na babu zetu nani ni washenzi? Kitu pekee kinachopelekea tuyanyoshee vidole mataifa hayo ni namna ambavyo yamekuwa yakinufaika na kile tunachokiita ‘faida mgogoro’ mara baada ya pande hasimu walizozichochea kupigana, hatimaye kupata madhara. Kinachoonekana baada ya hapo si kusaidia mapigano hayo yaishe, bali ni kuumia kwa rasilimali za taifa husika.

Mapokeo ya kidini katika bara letu yaliandaliwa kwa kipindi kirefu, hakuna mizania inayopima wema au ubaya, usahihi au upotoshaji, au hata mienendo ya dini hizi huku kwetu. Tumekuwa na woga wa kutotaka hata kuhoji tu kwanini dini hizi nyuma yake kuna vitisho vingi, vinavyotuweka mbali na Mungu kwa kuwa tunamwogopa (maana anaadhibu sana tunapokosa, hapendi tukosee, hapendi twende kinyume na kanuni zake). Lakini anatupenda sana pale tunapomtolea fungu la kumi.

Sitaki mnielewe vibaya mkanibatiza majina ya hovyo, lakini ukweli ni kwamba mnamkosea sana Mungu. Mungu hayuko hivyo, yaani mungu wa sisi waafrika sio mnyonge anayetaka tuwe watu wa kupelekwa kama bendera. Wala si dhaifu kushinda Mungu wa wazungu, wala hataki kila siku tumlilie kwa kueleza shida zetu ambazo tumejitakia wenyewe. Mungu katupa akili, ni lazima tuitumie kutafakari mapokeo ya dini hizi. Na panapobidi basi tusimame kuabudu kwa usahihi, tofauti na hizi imani za kibepari zisizo na kweli ya huko tuendako.


NB: Picha imetumika kufasili Makala hii, haina umiliki.
Screenshot_2019-03-30-12-27-38.jpg
 
Ukweli mchungu ila atuna namna tuishi umu umu.tu nazani nikuto kuoji nako kumechangia kuogopa kwamba ukioji unamkosea.Mungu.
 
Ukweli mchungu ila atuna namna tuishi umu umu.tu nazani nikuto kuoji nako kumechangia kuogopa kwamba ukioji unamkosea.Mungu.
Shida yake ukihoji basi hapo ndipo "dhambi" inachipua, woga unashamiri, na adhabu kwa muumba inaanza. Ni ukweli mchungu, kuna mahali tunakosea sana.

Asante kwa kuisoma Makala hii. Karibu sana.
 
Don Nalimison alianzisha dini yake, sio dhehebu, sijui mpaka sasa ana wafuasi wangapi? Hebu ngosha njoo utujibu
Unajua ujinga bado umekua tatizo sana.

Watu wamekua wakiongelea Imani za mababu zetu sanaaaaaa.
Umefatilia ni Mungu yupi alikua akifanyiwa ibada na mababu zetu.. ?
Alikua anatolewa sadaka kwa njia zipi ??

Mleta mda usikurupuke Rudi kasome chimboko la Imani za mababu zetu na njinsi sadaka zilivyokua zikitolewa. We katafute sijui utatoa wapi, ila tu katafute full details.
Tafuta history ya Nyuma kabisa, Wanyamwezi walitoka wapi, wairaki, nini asili ya wapare na kabila zingine..

Alafu rudi na kauzi kako haka upya.
Utajua ujui.

Alichoanzisha na kukisimamisha Mungu muumba wa mbingu na nchi acha kiendelee kusimama na kusambaa kote duniani, huwezi stop.
 
Ilipaswa utumie akili kufikiria na sio hisia. Umetoka nje kabisa ya kile ambacho Makala hii imejadili. Yamkini wewe ndiye unapaswa kurudi na kusoma chimbuko la Imani za kiafrika, na zaidi ujikite katika tathmini ya Utamaduni wa Mwafrika.

Fanya uhusianishi wa zama zile na zama hizi za mapokeo ya dini ambazo zimeleta mtafaruku katika mataifa mengi. Wangapi wamekufa katika mapigano ya kidini, wangapi wametoweka katika mazingira ambayo imani ya dini za kimapokeo imechagiza vifo.

Zungumza mfumo wa kimaisha ambao kuna taasisi za kidini ambazo zinafanya kazi kama Dola. Nini madhara yake kwa mataifa ambayo wamepokea imani hizi?

Ukimaliza yote hayo weka hisia pembeni, iruhusu akili ifikiri.
Tukizungumzia dini, dini kubwa hapa duniani ni mbili.. Ukristo na Uislamu.

Sasa unaposema mapigano mala vifo. We weka wazi unamuogopa nani ?
Na ukiongelea hayo mambo hebu tuwaulize alshababu/ndugu zetu waislamu tuwaulize kulikoni...

Am a Christianity na sijafungwa fikra na dhehebu lolote lile. kama kuna dini/imani nzuri zaidi ya Ukristo nipo tayar kujiunga.
 
Naomba nitumie mfano wa nchini Nigeria. Ile nchi imegawanywa, kaskazini ikiwa ni ngome ya kiislamu na kusini ikiwa ni ngome wa kikristu.

(Najiuliza, wanaigawa ili iwe nini? Kwa faida ya nani? Ikiwa dini na imani zinaongozwa na upendo kwanini waafrika hawa wahitilafiane kwa sababu ya dini tena baada ya Mapokeo? Mwishowe najijibu, lengo ni kuumia kwa rasilimali za kiafrika)

Baada ya hapo likazuka kundi la Boko Haram, uislamu ukapakwa matope kwa propaganda kwamba wanataka kuanzisha ngome ya uislamu. Mabinti wa kikristu wakatekwa n.k.

Sijawahi sikia ukristu una magaidi bali uislamu. Ni Mungu yupi aliumba Magaidi hawa ikiwa binadamu wote tuko sawa mbele yake? Hizi ni propaganda tu chini ya jua ili watu wanufaike.

Iweje ukristu uwe unamithilika kama Taifa tena wenye uwakilishi (kiti) hadi Umoja wa Mataifa na si uislamu? Ikiwa Mungu aliziumba dini hizi kwa upendo wake kwetu, mbona zinatugawa?

Nchini Zimbabwe, nani anafahamu kuwa kuna makanisa dola yanagombania madaraka kila uchwao. Ni vita vya Anglikani na Roman, kwanini makanisa dola yame ji-attach kwenye siasa za dunia. Lengo ni kunfaidia nani?

Kuna nchi ziko katika mkakati wa kidunia, zinagawika kwa misingi ya dini, zipo zinazogawika kwa misingi ya ukabila, n.k.

Najiuliza nchi ya Nigeria kwa zaidi ya miaka 10 sasa wameshndwa kuwadhibiti Boko Haram, na ikiwa ni nchi ambayo iko kwenye top five ya mataifa yenye jeshi imara Afrika. Ongeza jeshi la Umoja wa nchi za Magharibi, jeshi la U.N lakini bado Boko Haram anatamba tu. Nyuma yake ni kivuli cha maslahi za kidini?

Who is Boko Haram? For whom they serve?
Mifano iko mingi. Nawasilisha.
Makao makuu ya wachawi Duniani nasikia ni Africa katika nchi ya Nigeria.
Tuyaache hayo.

Cha kwanza unatakiwa ujue.. waislamu na wakristo hawana Mungu mmoja,
Waislamu wana mungu wao na wakristo wana mungu wao.

Kutaka hizi dini mbili zifungamane ni haiwezekani.
Tusisahau Shetani yupo.

Unaweza kufatilia nini hasa chimbuko la gasia au machafuko hayo na unaweza pata majibu vizuri tu.

Na pia kitu kingine cha mwisho unatakiwa kujua kila mahali wanapomzungumzia mungu, shetani pia utamkuta kwenye hayo maeneo katoa copy zake.
Namaanisha shetani mbinu yake ni Kuiga siku zote, anatoa product ambazo ni ngumu sana kutofautisha hiki kimefanywa na Mungu au ni shetani, kazi kwako kujua hizo roho zimetokana na nani.

Conclusion :
Tuache kubeza dini au imani zote kwani Mungu wa kweli yupo na ukimtafuta anapatikana.
 
Na: Norbert Mporoto
28.02.2021

“Allah amefaridhisha mambo ya dini kwa hivyo usiyapuuze. Vilevile kaweka mipaka usiikiuke, amekataza baadhi ya mambo kwa hivyo usiyafanye. Yale aliyoyanyamazia ni kwa ajili ya huruma zake kwako wala hakusahau kwa hiyo usiyadadisi”

Ni maneno mazuri yenye kubeba dhamiri ya imani zetu, ili mioyo yetu itulie tukisubiria kuuona ufalme wa mbingu. Naomba nikiuke kidogo misingi ya imani zisizo asili yetu kwa kuanza kufanya udadisi juu ya uhusiano wetu wa kibinadamu na dini hizi, ambazo zinaongozwa na misahafu kama katiba yake.

Kama ilivyo katika uongozi wa taasisi, jamii, au taifa lazima kuna sheria na taratibu ambazo zinatumika kama mwongozo, na asili yake ikiwa ni katiba ambayo ndiyo mkusanyiko wa sheria hizo. Hivyo, imani zetu kupitia dini huongozwa na misahafu anuai kulingana na muktadha wa dini husika. Kuzungumzia dini ya mtu kwa uzuri au ubaya si jambo la kiungwana hata kidogo, lakini kukiuka misingi ya dini ili kukosoa (kulingana na mienendo husika), kuokoa na kurekebisha hatma za waumini katika imani zao ili kutafuta mwafaka mwema katika jamii zao ni jambo sahihi ambalo makala hii inalenga kujadili kwa kina.

Kiuhalisia dini ni jukwaa linalowakusanya watu wa imani moja chini ya mwamvuli unaosimamia na kuainisha sheria, kanuni, miiko, na taratibu ambazo huakisi utamaduni na asili yao wakati wote wanaposimama kuitetea kwa kuabudu, na kuidhihirisha imani yao. Lakini kwa maana iliyopoteza umaana wake katika mapokeo yaliyofanywa na wengi wetu ni ile inayoakisi dini kuwa imani. Awali kabla ya mapokeo ya imani au dini hizi kulikuwapo na imani zetu asilia (kote barani Afrika). Mapokeo ya imani kiukweli hayakuzingatia muktadha na hatma yetu, ila tu wapokeaji hawa waliweza kuzipokea kama m’badala wa imani zao zilizoitwa za kishenzi na zilizojaa uovu na matendo yanayosadikika kuwa ya kishetani. Labda! Kwa kifupi, walianzisha safari isiyoweka bayana mwelekeo wake, na baadae kukosa ufahamu wa kuona mbali kusawili matokeo ya kinachofanyika kwa kivuli cha imani hizo.

Uwezo hafifu wa kung’amua kilichopo ndani ya mapokeo hayo na matokeo yake unatokana na mfumo uliotumika na waliozileta imani hizo. Mbinu hizo zilimdhoofisha mpokeaji na kumuaminisha kuwa hakuna imani ya kweli zaidi ya hiyo, hivyo msingi huu m’bovu umetujenga kuwa na akili fupi za kutoweza kuamua nini hatma yetu dhidi ya mataifa anzilishi ya imani hizi.

Jambo ambalo ni kosa, ni kushindwa kung’amua kuwa imani ya watu fulani hubeba utamaduni wa watu husika, hivyo hata akipewa mtu mwingine aiendeleze imani hiyo hawezi endana nayo kamwe. Ni shughuli ngumu ya kumpaka rangi punda ili ageuke kuwa pundamilia wakati inafahamika wazi kuwa mvua ikinyesha atairejea asili yake ya kuwa punda. Na hivyo ndivyo ilivyo kwetu sisi tuliopokea imani hii, na tumeshindwa kuendana nayo kiasi kwamba imani hizi zimegeuka kuwa zimwi linalotutafuna kila uchao.Lakini upande wa pili kwa waliotuletea imani hizi kwao ni furaha na shangwe mithili ya ngedere waliovamia shamba la mahindi maana hawana uchungu nayo, wala hawaumii kwani hawajui hata gharama na kiasi cha jasho lilichomwagika kufikia hatua hiyo.

Kitendo cha kuridhia kupokea imani zao, ni kuruhusu mataifa yetu yaenende katika mwongozo wa tamaduni mbili tofauti. Lakini tamaduni hizi mbili haziwezi pikika katika chungu kimoja, hivyo chokochoko na mitafaruku inayoendelea barani Afrika kwa namna moja au nyingine inatokana na ugeni wa tamaduni za kiimani tulizobebeshwa, na kuzivaa haswa kanakwamba ni asili yetu, kiasi cha kushindwa kuimudu mihemko yetu juu yake na hata kutizamana kama maadui wa kiimani.

Leo hii Afrika, dini imekuwa mithili ya dawa za kulevya zenye madhara zaidi ya bangi na mirungi (yapasa itumike fikra ili uweze kutambua ukweli huu, na tuweke kando hisia zetu). Imani za dini tulizopokea zimeathiri watu wetu kifikra, zimejenga hofu na woga na zaidi dini hizi zinatafuna mihimili ya mataifa yetu, yaani aliyeleta ukoloni ndiye aliyeleta dini hivyo shabaha ya mkoloni bado iko palepale kupitia mwamvuli wa dini tulizopokea. Hivyo tunautukuza ukoloni katika namna tusiyoielewa!

Kupitia mikononi mwa waanzilishi wa dini hizi, dini zimekuwa zikichochea mapigano baina ya waafrika. Kwa sababu za kutengenezwa, historia ya bara la Afrika inaonyesha namna ambavyo baadhi ya nchi zimekuwa zikikumbwa na kashfa ya mapigano ya kidini. Japokuwa ukweli wake ni kwamba mapigano hayo yanasababishwa na imani ya uadui ambavyo mizizi yake imetokana na mataifa anzilishi wa dini hizo kwa kutizama watu wa dini moja kuwa na uhasama na watu wa dini nyingine, kitu kinachopelekea kuvunjika kwa umoja baina yao na kushamiri kwa mapigano ya kidini.

Mapigano haya hayakuwepo kipindi babu zetu wakisali chini ya mti ama kipindi tunatambika; kipindi ambacho hizo imani zetu zinazoitwa za kishezi na zenye unasaba na ushetani zikiwa zinatumika. Kamwe hatukuwahi kupigana kisa huyu anatambika chini ya mti au yule anatambika juu ya jiwe. Kwanini leo hii kuwe na mapigano? Tumetoa wapi hizi tabia za kishenzi kwenye dini tulizoaminishwa eti ni za watu safi na werevu? Kwanini dini za sasa hazihubiri upendo katika matendo? Kati ya hao na babu zetu nani ni washenzi? Kitu pekee kinachopelekea tuyanyoshee vidole mataifa hayo ni namna ambavyo yamekuwa yakinufaika na kile tunachokiita ‘faida mgogoro’ mara baada ya pande hasimu walizozichochea kupigana, hatimaye kupata madhara. Kinachoonekana baada ya hapo si kusaidia mapigano hayo yaishe, bali ni kuumia kwa rasilimali za taifa husika.

Mapokeo ya kidini katika bara letu yaliandaliwa kwa kipindi kirefu, hakuna mizania inayopima wema au ubaya, usahihi au upotoshaji, au hata mienendo ya dini hizi huku kwetu. Tumekuwa na woga wa kutotaka hata kuhoji tu kwanini dini hizi nyuma yake kuna vitisho vingi, vinavyotuweka mbali na Mungu kwa kuwa tunamwogopa (maana anaadhibu sana tunapokosa, hapendi tukosee, hapendi twende kinyume na kanuni zake). Lakini anatupenda sana pale tunapomtolea fungu la kumi.

Sitaki mnielewe vibaya mkanibatiza majina ya hovyo, lakini ukweli ni kwamba mnamkosea sana Mungu. Mungu hayuko hivyo, yaani mungu wa sisi waafrika sio mnyonge anayetaka tuwe watu wa kupelekwa kama bendera. Wala si dhaifu kushinda Mungu wa wazungu, wala hataki kila siku tumlilie kwa kueleza shida zetu ambazo tumejitakia wenyewe. Mungu katupa akili, ni lazima tuitumie kutafakari mapokeo ya dini hizi. Na panapobidi basi tusimame kuabudu kwa usahihi, tofauti na hizi imani za kibepari zisizo na kweli ya huko tuendako.


NB: Picha imetumika kufasili Makala hii, haina umiliki.View attachment 1714046
Dini ipo moja tu ukristo bas hao wengine ni magenge ya wahalifu na vikundi vya ugaidi km hutaki jinyonge tu
 
Back
Top Bottom