Ujumbe Wa Mama Kwa Mwanawe

Ujumbe Wa Mama Kwa Mwanawe

The Boldly

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2017
Posts
2,377
Reaction score
5,150
*UJUMBE WA MAMA KWA MWANAE KIPENZI*
🤔🤔🤔

*"Mwanangu sikwambii uache kusoma au uache kazi lakini ukikutana na Fursa nzuri usiiache kamwe."*

*"Mwanangu utamaliza Chuo baada ya Miaka 25..."*

Jumla ya ada yako tangu unaanza shule mpaka unamaliza ni *Milion 16,800,000/= Tshs*.

Tanzania itakupa Mshahara wa *Laki 7 (Tshs 700,000/=)* kila mwezi kwa degree yako TU.

Ila.,
Toa asilimia *10% NSSF* (70,000/=)

Toa *Kodi asilimia 9%* (63,000/=)

Toa *Helsb asilimia 15%* (105,000/=)

Toa *NHIF asilimia 3%* (21,000/=)

Utabakiwa na *Tshs. 441,000/=*

Toa *Nauli kwa mwezi* Tsh 90,000/=

Toa *Chakula cha Mchana* Tsh.90,000/=

Toa *Pango* Tsh.100,000/=

Toa *Chakula cha nyumbani* Tsh.90,000/=

Toa *Gharama za kiwi na doby + nguo za ofisi* Tshs. 30,000/=

Utabakiwa na *Tshs 41,000/=*

Toa *bill ya Maji* 10,000/= na *Bill ya umeme* 20,000

Utabaki na *Tshs 11,000/=*

Weka na *Chupa ya Maji ya kunywa* ya 600/= ya bakheresa.

Hapo naona mwanangu kama utakuwa unadaiwa kila mwezi.

Basi komaa tu hivyo hivyo siku ziende.

Ukitaka kupiga simu tuma *Tafadhali Nipigie* maana huna budget ya vocha na pesa imekwisha.

Lakini pia usisahau *kutoa zaka na sadaka*.

Na pia *usiruhusu wageni kuja kukutembelea nyumbani kwako*, maana hutokuwa na pesa ya kuwanunulia hata soda.

Haya jitahidi Mwanangu shule njema angalia usigongwe na Bodaboda kwa mawazo ya maisha.
 
Back
Top Bottom