Ujumbe toka udsm

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
TUAMKE JAMANI TUSILALE, MAPAMBANO BADO........
Napenda kwanza kutoa shukurani zangu za dhati kabisa kwenu ninyi wanachuo
wenzangu kwa mshikamano mliouonyesha kipindi chote cha mapambano dhidi ya
sera kandamizi na dhalimu ya uchangiaji wa elimu ya juu. Hii inadhihirisha
wazi ni jinsi gani tulivyo wazalendo na kuonyesha ukomavu wa kifikra katika
kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya Taifa letu. Nawahakikishieni ndugu zangu
anayedhania mabadiliko ya kweli yatatokea kwa kuibembeleza serikali ajue
anakosea sana. Naimani wengi wetu tumerudi salama chuoni, poleni kwa
matatizo yote yaliyotusibu kwa kipindi chote tulichokuwa uraiani naaimani
kila mmoja wetu amekuwa barozi mzuri katika kuuelimisha uma wa watanzania
kuelewa kiini hasa cha tatizo ni nini. Hatuna sababu yoyote ile ya msingi ya
kujilaumu kwa mgomo wetu, kwani tulikuwa tunapigania mustakabari wa maisha
ya watanzania masikini na mabadiliko kidogo tumeyaona ingawaje hatujafikia
lengo letu. Cha kusikitisha labda ni wenzetu waliopoteza maisha katika ajali
ya basi kule singida, ambapo baadhi yetu pia walipata majeraha. Mwenyezi
mungu awarehemu na zawadi pekee tuliyonayo kwao ni kufanikisha vita hii
tuliyoianza pamoja. Kilicho mbele yetu hivi sasa ni kuendeleza wimbi la
mapambano tena safari hii ajenda zetu za msingi ni kuuondoa utawala wa
kisiasa chuoni, kurejesha wenzetu chuoni, kupigania muhimiri wetu DARUSO
pamoja na kuizika na kuitokomeza kabisa sera ya uchangiaji. Wakati huu ni wa
pekee katika historia ya nchi yetu ambapo vijana hasa wasomi ni nguvu ya
mabadiliko, tukikaa kimya historia hii ndugu zangu itatuhukumu. Najua wengi
wetu sasa hivi tumejawa na roho za uoga wa kinafiki, lakini jua kabisa fika
hiyo siyo sirika ya msomi tena wa chuo kikuu mlimani ambayo ni uwezo wa
kuhoji yanayokubalika na kukataa vitu vya kishenzi vilivyozoeleka na
visivokubalika mbele ya wapigania haki. Kwa sababu tunapokataa tunajenga
hoja ya msingi kuonyesha jinsi gani hatukubaliani na maamuzi yanayofanywa
kisiasa zaidi na kutukandamiza sie wanafunzi. Wote tunakumbuka fedha ya
matibabu iliunganishwa kwenye ada ya mwanafunzi kwa mwaka wa masomo wa jana
(2006/07) na tukatangaziwa na huyo Mkaliandara pale Nkrumah, na hata mwaka
huu wa masomo kabla ya chuo hakijafungwa ilieleweka hivyo, lakini sasa
tumelazimishwa kulipia gharama za ziada shilingi 50,000 eti za matibabu.
Jamani hela zetu hizo ndizo zilikuwa zikitumika kujaza mafuta ya AURORA za
Mkaliandara, kuwalipa wale washenzi FFU na kulipa allowances za kina BUSH
pale getini geti maji. Leo ni wiki ya tatu tangu chuo kifunguliwe mpaka hivi
sasa watu hatuna pesa sababu eti bado wanaendelea kuprocess kutokana na
batch za malipo, tena wengine wanawekewa laki tatu, wengine laki nne na
wengine laki sita au siku hizi kwenye bum kuna grade?. Huo ndiyo wizi
tunaoukataa jamani tukigoma wanatuita wahuni, tusipokuwa makini fedha zetu
hizi zitakuwa zinafisadiwa, kuna umuhimu wa kuipigania DARUSO yetu. Leo hii
tumerudi chuoni mtu ulikuwa na chumba awali na ulikilipia semistor nzima,
lakini sasa hivi unanyang'anywa tena bila kulipwa hata fidia anapewa mtu
mwingine ambaye alikuwa hana chumba kisa umechelewa kulipa, kweli hiyo ni
haki?. Sisemi mliopata mnyang'anywe ila tulipwe tulionyang'anywa. Bei ya
vitu zimepanda maradufu si cafteria wala stationary tena hawana huruma
kabisa wanadai mambo yamebadilika, je hayo mambo mbona hayakubadilika awali
yabadilike leo hii kisa hatuna uongozi wa DARUSO? Tunakatazwa tusibebane
tena kwa kukaguliwa kwa usumbufu mkubwa na wafanyakazi wa ofisi ya dean of
students usiku wa manane, kweli hiyo ndiyo kazi ya mlezi na bila kubebana
tutaweza kuishi ndugu zangu? Tujiulize kwa nini cafteria ya DARUSO
imevunjwa? Eti kwa sababu mapato yake yanaingia DARUSO ndiyo yanatupa kiburi
sie wanafunzi kugoma tena huyo ni proffesor mzima ndiyo anachangia hoja hiyo
kwenye panel badala ya kuainisha kiini cha tatizo. Kweli huku ni kufirisika
kimawazo kwa uongozi wetu wa chuo na kuzidi kutawaliwa na fikra za kisiasa.
Ndugu zangu kisheria udahili wetu haukufutwa sie bado ni wanafunzi halali wa
chuo kiku cha Tanzania, registration number zetu ni zile zile, matokeo yetu
ni yaleyale yanaendelea kutumika, iweje leo sasa uniambie eti viongozi wetu
wamepoteza sifa za kuwa viongozi kisa tumedahiriwa upya. Huu ni wizi mtupu
na propaganda za kisiasa za ndugu yetu Mkaliandara, suala la kutengenezewa
vitambulisho vipya lilikuwa ni la lazima ili kurekebisha expiring date na
ndiyo maana tarehe ya kuexpire ni sawa kwa wanafunzi wote, na mtakaobakia
chuoni mtarudishiwa vitambulisho vyenu vya zamani. Ndugu zangu wasomi haya
yote yanafanyika kwa sababu hatuna chombo chetu cha kututetea, huu tena siyo
wakati wa kuogopa ni kusimama imara na kupigania kuirudisha madarakani
serikali yetu ya DARUSO. Tukulifanikisha hilo wale wenzangu na mimi
tuliyonyang'anywa vyumba tutalipwa peza zetu pamoja na fidia juu kwa sababu
wametusitishia mkataba ghafla bila kupewa notes, fedha za matibabu
zitaeleweka tulizichangia kwa msingi ipi? Na hizo cafteria na stationary
ambao wamiliki wake ni wao wenyewe watatueleza ni kwa nini wamepandisha bei
ya vitu hovyo? Na itawezesha pia wenzetu walioko nje kwa ajili ya umasikini
wetu wanarudi chuoni haraka iwezekanavyo pamoja na mwanaharakati,
mpambanaji, ndugu yetu mpendwa na mtetezi wa haki za masikini raia wa Uganda
Silas Kefar Odong Odwar ambaye alifutiwa kibali cha kuishi nchini kwa
propaganda za kisiasa na kuondolewa nchini mara moja anaungana nasi.
Tusipokaa chini na kubadili mwelekeo wa fikra zetu hivi sasa, tutajikuta
tumepelekwa tusikotaka kwenda na tusijue tumefikaje huko, kwa pamoja
tunaweza "The greatness of our survival here at the hill is not a given we
must fight for it and solidarity will be only our truly mace" Aluta continua
vita bado inaendelea tusiogope tuimarishe ushirikiano wetu tukutane
REVOLUTIONARY SQUARE kwa mikakati zaidi nchi hii ni yetu lazima
tuipiganie.Ni mimi mtoto wa masikini tuwasiliane kupitia
masikin...@yahoo.com
 
Walikubali tshirt za kijani na njano, wakapikiwa pilau na wakapelekewa mabasi wakajiona wajanja sana. Sisi tuliumia sana kwa usaliti wenu wakati ule kuona jamii ya kisomi ikifanya mambo ya kihuni kabisa lakini tulikuwa hatuna cha kufanya uchaguzi ulikuwa wenu. sasa mnaona nyota nyota mnaanza kulialia. Mimi nawaambia na bado usaliti wenu kwa nchi utawatokea puani kwani hili ni part gazeti tu. mafisadi wamehiaribu nchi hata mtakao maliza chuo kwa uchungu ( kama Hawa alivyoambia baada ya dhabi yake kuwa utazaa kwa uchungu) kazi hakuna kwa hiyo mtaendelea kula pilau ya pale diamond na kuvaa Tshirt a kijani na njano nyie watoto wa wakulima na wafanyakazi shame on you!

Na hii ni zawadi yenu wote mliofanya ule usaliti ili muweze kutubu kwa nchi na kwa wote waliowategemea muwatetee Mithali 1: 8-19
8 Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, wala usiache sheria ya mama yako
9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, na mkufu shingoni mwako.
10 Mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi wewe usikubali
11. Wakisema "haya! njoo pamoja nasi na tuvizie ili kumwaga damu tumwotee asiye na hatia, bila sababu
12 tuwameze hai kama kuzimu na wazima , kama wao washukao shimoni
13 Tutapata mali yote ya thamani tutazijaza nyumba zetu mateka
14 Wewe utashirikiana nasi tutakuwa na vitu vyote shirika
15 Mwanangu, usiende njiani pamoja nao uzuie mguu wako usiende katika mapito yao
16 Maana miguu yao huenda mbio maovuni, nao hufanya haraka ili kumwaga damu
17 Kwa kuwa mtego hutegwa bure, mbele ya macho ya ndege yeyote
18 Na hao hujitolea damu yao wenyewe hujinyemelea nafsi zao wenyewe
19 Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali huuondoa uhai wao walio nayo
 
Last edited:
Walikubali tshirt za kijani na njano, wakapikiwa pilau na wakapelekewa mabasi wakajiona wajanjasana. Sisi tuliumia sana kwa usaliti wenu lakini tulikuwa hatuna cha kufanya uchaguzi ulikuwa wenu. sasa mnaona nyota nyota mnaanza kulialia. Mimi nawaambia na bado usaliti wenu kwa nchi utawatokea puani kwani hili ni part gazeti tu. mafisadi wamearuibu nchi hata mtakao maliza chuo kwa uchungu ( kama Hawa alivyoambia baada utazaa kwa uchungu) kazi hakuna kwa hiyo mtaendelea kula pilau ya pale diamond pamoja na Tshirt shame on you!

Ndio hivyo wote utawaona mstari wa mbele kuipigia debe CCM na wache huwepo katika upinzani na sasa nasikia au wameshafungua Tawi la CCM na wamejiunga eti ni wakereketwa wakuu.
 
TUAMKE JAMANI TUSILALE, MAPAMBANO BADO........
Napenda kwanza kutoa shukurani zangu za dhati kabisa kwenu ninyi wanachuo
wenzangu kwa mshikamano mliouonyesha kipindi chote cha mapambano dhidi ya
sera kandamizi na dhalimu ya uchangiaji wa elimu ya juu. Hii inadhihirisha
wazi ni jinsi gani tulivyo wazalendo na kuonyesha ukomavu wa kifikra katika
kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya Taifa letu. Nawahakikishieni ndugu zangu
anayedhania mabadiliko ya kweli yatatokea kwa kuibembeleza serikali ajue
anakosea sana. Naimani wengi wetu tumerudi salama chuoni, poleni kwa
matatizo yote yaliyotusibu kwa kipindi chote tulichokuwa uraiani naaimani
kila mmoja wetu amekuwa barozi mzuri katika kuuelimisha uma wa watanzania
kuelewa kiini hasa cha tatizo ni nini. Hatuna sababu yoyote ile ya msingi ya
kujilaumu kwa mgomo wetu, kwani tulikuwa tunapigania mustakabari wa maisha
ya watanzania masikini na mabadiliko kidogo tumeyaona ingawaje hatujafikia
lengo letu. Cha kusikitisha labda ni wenzetu waliopoteza maisha katika ajali
ya basi kule singida, ambapo baadhi yetu pia walipata majeraha. Mwenyezi
mungu awarehemu na zawadi pekee tuliyonayo kwao ni kufanikisha vita hii
tuliyoianza pamoja. Kilicho mbele yetu hivi sasa ni kuendeleza wimbi la
mapambano tena safari hii ajenda zetu za msingi ni kuuondoa utawala wa
kisiasa chuoni, kurejesha wenzetu chuoni, kupigania muhimiri wetu DARUSO
pamoja na kuizika na kuitokomeza kabisa sera ya uchangiaji. Wakati huu ni wa
pekee katika historia ya nchi yetu ambapo vijana hasa wasomi ni nguvu ya
mabadiliko, tukikaa kimya historia hii ndugu zangu itatuhukumu. Najua wengi
wetu sasa hivi tumejawa na roho za uoga wa kinafiki, lakini jua kabisa fika
hiyo siyo sirika ya msomi tena wa chuo kikuu mlimani ambayo ni uwezo wa
kuhoji yanayokubalika na kukataa vitu vya kishenzi vilivyozoeleka na
visivokubalika mbele ya wapigania haki. Kwa sababu tunapokataa tunajenga
hoja ya msingi kuonyesha jinsi gani hatukubaliani na maamuzi yanayofanywa
kisiasa zaidi na kutukandamiza sie wanafunzi. Wote tunakumbuka fedha ya
matibabu iliunganishwa kwenye ada ya mwanafunzi kwa mwaka wa masomo wa jana
(2006/07) na tukatangaziwa na huyo Mkaliandara pale Nkrumah, na hata mwaka
huu wa masomo kabla ya chuo hakijafungwa ilieleweka hivyo, lakini sasa
tumelazimishwa kulipia gharama za ziada shilingi 50,000 eti za matibabu.
Jamani hela zetu hizo ndizo zilikuwa zikitumika kujaza mafuta ya AURORA za
Mkaliandara, kuwalipa wale washenzi FFU na kulipa allowances za kina BUSH
pale getini geti maji. Leo ni wiki ya tatu tangu chuo kifunguliwe mpaka hivi
sasa watu hatuna pesa sababu eti bado wanaendelea kuprocess kutokana na
batch za malipo, tena wengine wanawekewa laki tatu, wengine laki nne na
wengine laki sita au siku hizi kwenye bum kuna grade?. Huo ndiyo wizi
tunaoukataa jamani tukigoma wanatuita wahuni, tusipokuwa makini fedha zetu
hizi zitakuwa zinafisadiwa, kuna umuhimu wa kuipigania DARUSO yetu. Leo hii
tumerudi chuoni mtu ulikuwa na chumba awali na ulikilipia semistor nzima,
lakini sasa hivi unanyang'anywa tena bila kulipwa hata fidia anapewa mtu
mwingine ambaye alikuwa hana chumba kisa umechelewa kulipa, kweli hiyo ni
haki?. Sisemi mliopata mnyang'anywe ila tulipwe tulionyang'anywa. Bei ya
vitu zimepanda maradufu si cafteria wala stationary tena hawana huruma
kabisa wanadai mambo yamebadilika, je hayo mambo mbona hayakubadilika awali
yabadilike leo hii kisa hatuna uongozi wa DARUSO? Tunakatazwa tusibebane
tena kwa kukaguliwa kwa usumbufu mkubwa na wafanyakazi wa ofisi ya dean of
students usiku wa manane, kweli hiyo ndiyo kazi ya mlezi na bila kubebana
tutaweza kuishi ndugu zangu? Tujiulize kwa nini cafteria ya DARUSO
imevunjwa? Eti kwa sababu mapato yake yanaingia DARUSO ndiyo yanatupa kiburi
sie wanafunzi kugoma tena huyo ni proffesor mzima ndiyo anachangia hoja hiyo
kwenye panel badala ya kuainisha kiini cha tatizo. Kweli huku ni kufirisika
kimawazo kwa uongozi wetu wa chuo na kuzidi kutawaliwa na fikra za kisiasa.
Ndugu zangu kisheria udahili wetu haukufutwa sie bado ni wanafunzi halali wa
chuo kiku cha Tanzania, registration number zetu ni zile zile, matokeo yetu
ni yaleyale yanaendelea kutumika, iweje leo sasa uniambie eti viongozi wetu
wamepoteza sifa za kuwa viongozi kisa tumedahiriwa upya. Huu ni wizi mtupu
na propaganda za kisiasa za ndugu yetu Mkaliandara, suala la kutengenezewa
vitambulisho vipya lilikuwa ni la lazima ili kurekebisha expiring date na
ndiyo maana tarehe ya kuexpire ni sawa kwa wanafunzi wote, na mtakaobakia
chuoni mtarudishiwa vitambulisho vyenu vya zamani. Ndugu zangu wasomi haya
yote yanafanyika kwa sababu hatuna chombo chetu cha kututetea, huu tena siyo
wakati wa kuogopa ni kusimama imara na kupigania kuirudisha madarakani
serikali yetu ya DARUSO. Tukulifanikisha hilo wale wenzangu na mimi
tuliyonyang'anywa vyumba tutalipwa peza zetu pamoja na fidia juu kwa sababu
wametusitishia mkataba ghafla bila kupewa notes, fedha za matibabu
zitaeleweka tulizichangia kwa msingi ipi? Na hizo cafteria na stationary
ambao wamiliki wake ni wao wenyewe watatueleza ni kwa nini wamepandisha bei
ya vitu hovyo? Na itawezesha pia wenzetu walioko nje kwa ajili ya umasikini
wetu wanarudi chuoni haraka iwezekanavyo pamoja na mwanaharakati,
mpambanaji, ndugu yetu mpendwa na mtetezi wa haki za masikini raia wa Uganda
Silas Kefar Odong Odwar ambaye alifutiwa kibali cha kuishi nchini kwa
propaganda za kisiasa na kuondolewa nchini mara moja anaungana nasi.
Tusipokaa chini na kubadili mwelekeo wa fikra zetu hivi sasa, tutajikuta
tumepelekwa tusikotaka kwenda na tusijue tumefikaje huko, kwa pamoja
tunaweza "The greatness of our survival here at the hill is not a given we
must fight for it and solidarity will be only our truly mace" Aluta continua
vita bado inaendelea tusiogope tuimarishe ushirikiano wetu tukutane

REVOLUTIONARY SQUARE kwa mikakati zaidi nchi hii ni yetu lazima
tuipiganie.Ni mimi mtoto wa masikini tuwasiliane kupitia
masikin...@yahoo.com[/
QUOTE]

WE NAWE UNAZUNGUMZIA SOLIDARITY IPI HAPO CHUONI KWENU?? HIYO SOLIDARITY FAKE MLIYONAYO MNAFIKIRIA MNAWEZA MKAKILAZIMISHA CHUO AU SERIKALI IKATII MNACHOTAKA KWA SASA?? HEBU MWAMBIE BABA YAKO AUZE NG'OMBE HUKO KIJIJINI KWENU UMALIZE KUSOMA SIO KUANDIKA MAMBO YASIYO NA MBELE WALA NYUMA, WENZAKO WAMELIPA PESA WANASOMA NA 95% WAMESHAREJEA HAPO CHUONI WEWE UNATAKA KUWAFANYA WAPOTEZE MUDA WAO PASIPO SABABU ZA MSINGI, GROW UP BWANA KOMAA SONGA MBELE SIO KUTAKA KULETA MIGOMO ISIYO NA MSINGI KHA....
 
Back
Top Bottom