Ujumbe kwa Ezekiel Maige

Ujumbe kwa Ezekiel Maige

Yakini

Member
Joined
Nov 20, 2012
Posts
75
Reaction score
19
Tunakumbuka jinsi ulivyoingia kwenye siasa na kupata upenyo kwenye jimbo letu la msalala. Ulianza kwa mbwembwe hata watu wakakusifia japo nilipata shida sana kuamini hilo.

Nikukumbushe tu kwamba wakati ukiingia bungeni kwa mara ya uliikuta ISAKA yetu ikivuma kwa kuwa na fulsa nyingi za kiuchumi hasa bandari yetu ilikuwa ikijulikana inchini kote kama bandari ya nchi kavu, Lakini toka umekuwa mbunge hakuna jipya ulilolifanya zaidi ya kuendelea kuipoteza Isaka yetu.

Hata maji tu yamekushinda kuyasogeza kutoka kahama mjini. Hali ilikuwa mbaya zaidi pale kwa hila zako ulipo changia kumuondoa diwani msomi kwa hila na wana ccm wenzio na kupandikiza diwani asiyejua hili wala lile, diwani wa darasa la saba.

Hivi ulikuwa na mpango gani?? au ndo kutuadhibu? Tukupe tu taarifa kuwa tumechoka, na tunakusubiri 2015. Pamoja na kuwa naibu waziri na baadae kuwa waziri umeshindwa kabisa hata kutuondolea kero ya maji, acha shida zingine tulizonazo, bandari imekufa, mashirika yanakufa, wewe ndo kwanza kumekucha na CCM. Hakika utajua tu 2015.

Ni hayo tu.
 
Mmechegua mchumia tumbo.

Next time kuweni makini kabla hamjafanya maamuzi kuchagua wawakilishi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Yeye alikuwa anataka ngazi ya kupandia ili anunue ile nyumba ya "dollar kadhaa, dsm" na kuanzisha kampuni ya uchukuzi wa malori siyo masuala ya maji huko kwao!
 
Huyu Maige ni kiazi sana,namfahamu kwa muda mrefu,hana msaada wowote hata kwa ndugu zake wa karibu.
 
Back
Top Bottom