Ujue uhalali wa siku za maombolezo kitaifa

Ujue uhalali wa siku za maombolezo kitaifa

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
12,212
Reaction score
23,258
Misingi ya kuomboleza siku 21 kitaifa imebebwa kwenye alama na si mioyoni?

Ukirejea sheria zote zilizotungwa na bunge chimbuko lake lilitazama tamaduni na mila!
Kila kabila lililounda taifa lina namna yake ya kuomboleza, kwa mfano;
  • Yapo makabila hunyoa nywele kama alama ya maombolezo.
  • Wapo wanaochinja ng'ombe na kusherekea kama alama ya maombolezo.
  • Wapo wanaohama miji kama Alama ya maombolezo.
  • Wapo wanaolala chini siku kadhaa kama ALAMA ya maombolezo.
Hivyo isingewezekana kulazimishana kuomboleza kwa mitindo hiyo na ndiyo maana katiba ikaona kuliko kufuata mila na tamaduni za kila kabila ni vyema kuwepo na ALAMA moja tu itakayowakilisha MAOMBOLEZO inchi nzima, na ALAMA HIYO ni BENDERA Kupepea nusu mlingoti Full stop!

Haya kukatazana kusherekea ni ujinga wa kutafsiri maono ya katiba!

Katiba ni kama Mila na tamaduni iliowekwa itumike kama destuli kwa watu wote waliostaarabika kitaifa bila buguza!

Na katiba ilitamka wazi kabisa. "Kutakuwa na siku kadhaa za maombolezo AMBAPO BENDERA ITAPEPEA NUSU MLINGOTI!

Kama Kungekuwa na ulazima wa kuzuia sherehe KATIBA Ingesema KUSIFANYIKE SHEREHE!

Kwanini katika siku 21 za maombolezo:
  • Serikali imeruhusu watu wafanye kazi? Si wangelala nyumbani kuomboleza?
  • Je, kama kazi ni lazima ziendelee hawafahamu kuwa miongoni mwa kazi ni pamoja na kuwa MC, mwanamziki au mwanamichezo? Au hizi siyo kazi za watu?
  • Kwanini serikali inaendelea kukusanya kodi siku za maombolezo?
  • Kwanini wanaaipishana ikulu/bungeni kupeana vyeo na kupiga bendi, meza na vigeregere siku za maombolezo?
  • Je, Hivi ndivyo maombolezo yalivyo kupeana ulaji kabla ya siku 21?
Au anaepaswa kuomboleza ni nani kama siyo kitaifa?

Viongozi someni KATIBA iko wazi! Hatutaki Mawazo binafsi kuwa ya KITAIFA!

Maombolezo kitaifa huwakilishwa na BENDERA tu, Imani na shughuli za kidini, kimila na tamaduni iliziacha kama zilivyo!
MSITUPANGIE!
 
We sio mzalendo kwa msiba huu unataka ukapige kwaito? Aah sio kweli. Huu in msiba mkubwa mno umetukuta tuvumilie tu siku rasmi ziishe mtaendelea na myatakayo.
 
We sio mzalendo kwa msiba huu unataka ukapige kwaito ?!!aah sio kweli ..huu in msiba mkubwa mno umetukuta tuvumilie tu siku rasmi ziishe mtaendelea na myatakayo.
Wafuate katiba! Imeelekeza NUSU MLINGOTI! Mambo mengine ya mtu mmoja mmoja hayapaswi kuwa MARUFUKU
 
Katiba imepitwa na wakati ,
Wafuate katiba! Imeelekeza NUSU MLINGOTI! Mambo mengine ya mtu mmoja mmoja hayapaswi kuwa MARUFUKU
Katiba imepitwa na wakati,ndio maana tuna mchakato was kuibadili baadae,mengine ni kufikiri tu kwamba haifai kusherehekea kipindi hiki,vumilienini tu bado tuna majonzi hata kama tamaduni zenu huwa kwenye msiba mnafurahishana kwa hili hapana.
 
Katiba imepitwa na wakati ,

Katiba imepitwa na wakati,ndio maana tuna mchakato was kuibadili baadae,mengine ni kufikiri tu kwamba haifai kusherehekea kipindi hiki,vumilienini tu bado tuna majonzi hata kama tamaduni zenu huwa kwenye msiba mnafurahishana kwa hili hapana.
Inchi inaongozwa na katiba IPI kama hii iliyopo unasema imepitwa na wakati,?
Inamaana katiba kusema BENDERA kupepea NUSU MLINGOTI unaona haikutosha?

Basi rudini kwanza mkabadili katiba
 
We sio mzalendo kwa msiba huu unataka ukapige kwaito ?!!aah sio kweli ..huu in msiba mkubwa mno umetukuta tuvumilie tu siku rasmi ziishe mtaendelea na myatakayo.
Hukuona wabunge walivyoshangilia kwa vifijo na nderemo wakati wa kuapishwa wabunge wapya. Maombolezo hayalihusu bunge? Uzalendo ni nini?
 
Hukuona wabunge walivyoshangilia kwa vifijo na nderemo wakati wa kuapishwa wabunge wapya. Maombolezo hayalihusu bunge? Uzalendo ni nini?
Inashangaza kwakweli, wao walipiga makofi na vigelegele, wakati huo inje BENDERA za ziko NUSU MLINGOTI!

Sasa iweje iwe marufuku wengine kusherekea pasaka wakati katiba ipo wazi?
 
Labda bao la mkono! Lakini la uwanjani lazima kushangilia
Vivyo hivyo kumbukumbu ya kufufuka kwa YESU KRISTO hushangiliwa kwa shangwe kuu kwani ni MWOKOZI. Matrampeti, ngoma , na vyombo vyote vifaavyo kutoa sauti njema vitavurumishwa kwa sauti kuu.

Huyo ni MFALME NA MUUMBA. Kelele za shangwe ni lazima kuonesha ukuu wa tukio. Mtuache tushangilie ukombozi wetu.!! Hatujawazuia wao kuendelea kulia!
 
Hukuona wabunge walivyoshangilia kwa vifijo na nderemo wakati wa kuapishwa wabunge wapya. Maombolezo hayalihusu bunge? Uzalendo ni nini?
Ile sio sherehe Bali ni shughuri,sherehe ndio zenye mushkeli
 
Ile sio sherehe Bali ni shughuri,sherehe ndio zenye mushkeli
Kwahiyo vigeregere vya kwenye shughuli ni tofauti na vigeregere vya sherehe ya kupalizwa YESU Kristo?
 
Ndio,Ila nasikia mama karuhusu
Hakuna cha kuruhusu wala kukataza! Bali Tuangalie KATIBA INASEMAJE!
Hii siyo bonus ni Haki ya wanainchi kuheshimu katiba!

Bila hivyo iko siku kuna tamko litatolewa usilale na wake zetu! Kama tutaendekeza maoni binafsi
 
Hakuna cha kuruhusu wala kukataza! Bali Tuangalie KATIBA INASEMAJE!
Hii siyo bonus ni Haki ya wanainchi kuheshimu katiba!

Bila hivyo iko siku kuna tamko litatolewa usilale na wake zetu! Kama tutaendekeza maoni binafsi
Ha ha haaaa
 
Thread yako ina make sense
Ndo ukweli huo! Hata wakikukamata hawana cha kukushitaki zaidi watumie mahabusu ya polisi kama fimbo lakini kisheria hawana cha kufanya! Vinginevyo wakubambikie kesi!
Na ukitoka unawaroga wote
 
Wafuate katiba! Imeelekeza NUSU MLINGOTI! Mambo mengine ya mtu mmoja mmoja hayapaswi kuwa MARUFUKU
Uko sahihi kwa 100%. Kiukweli polisi wetu wameonesha upeo mdogo sana wa kufikiri! Unaposema maombolezo ya kitaifa ya siku 21, maana yake ni bendera kuendelea kupepea nusu mlingoti, timu zetu za Taifa kuvaa vitambaa vyeusi, na pia kutoa dk 1 kumkumbuka marehemu katika matukio/mikusanyiko yenye ulazima wa kufanya jambo hilo!

Ila huu upuuzi wa kupiga marufuku watu kusherehekea sikukuu zao za kiimani, kwa kisingizio cha kulazimisha kumuomboleza mtu ambaye hana mafungamamo yoyote yale ya kifamilia na watu wengine! haukubaliki. Yaani binadamu mmoja tu awe ni bora sana kuliko Pasaka! Mimi nitasherehekea kama kawaida. Ole wake kenge yeyote yule anisogelee. 😞
 
Uko sahihi kwa 100%. Kiukweli polisi wetu wameonesha upeo mdogo sana wa kufikiri! Unaposema maombolezo ya kitaifa ya siku 21, maana yake ni bendera kuendelea kupepea nusu mlingoti, timu zetu za Taifa kuvaa vitambaa vyeusi, na pia kutoa dk 1 kumkumbuka marehemu katika matukio/mikusanyiko yenye ulazima wa kufanya jambo hilo!...
Mimi nishaandaa mbuzi! Siyumbishwi na kelele za kijinga utazani wanawaambia watoto wao!

Tunaongozwa na katiba!

Katiba iheshimiwe! Tusipangiane vitu vya hovyo hovyo kuwa ndo sheria!
 
Back
Top Bottom