pinno
JF-Expert Member
- Jan 17, 2013
- 1,213
- 1,233
Heshima kwenu wakuu!
Leo wakati wa taarifa ya habari ya saa moja ITV habari ya kwanza ilikuwa kuhusu kuwasili nchini kwa wanamuziki wa kikundi cha PSquare. Mimi nilishtuka kidogo, kwa kuwa tumezoea kusikia habari muhimu kitaifa zikipewa kipaumbele wakati wa taarifa za habari.
Sasa ujio wa hawa wasanii una umuhimu gani kitaifa? Kwa wananchi wa kule vijijini ambao hawana hata uhakika wa mlo mmoja kwa siku hii taarifa ina umuhimu gani? Hata kwa wananchi walio nje ya Dar es Salaam ambao hawategemei kuhudhuria tamasha la wanamuziki hao hizi habari zina manufaa gani?
Naomba michango yenu kuhusu hili wadau.
Its a big business, kesho hiyo tax, bajaji zitafanya sana biashara, watu watajipatia vipato, Hotel walibookiwa hao jamaa na crew yao zimapata faida, Pombe zitakazouzwa kesho ni balaa. bila kusahau kuwa makampuni ya pombe ni moja kati ya makampuni yanayoongoza kwa ulipaji wa kodi. kodi ambayo inamsaidia huyo mwananchi wa kijijini kwa kumpatia ruzuku ya mbolea.
By the way unashangaa kwamba habari kuwekwa ktk habari za kitaifa?? kwani uwanja wa Julius nyerere international airport upo wapi?? Leaders club ipo wapi?? kama vyote vipo dar, ndani ya tanzania, basi ni halali kwa habari kuwekwa kama habari ya kitaifa. kwani aliesema habari za siasa tu, ndo ziwekwe hapo ni nani??