Ujamaa ni njia sahihi ya kutoka kwenye umasikini

mechard Rwizile

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
1,571
873
Jan huko Devos, Switzerland; rais wa China ya Mao alitetea utandawazi wakati Waingereza na wamerakani wanatetea kulinda viwanda vyao. Wamebanwa mbavu, hawana njia nyingine ya kupumua, na kwa bahati mbaya hawataokoka.
Waingereza na Wamarekani wanadhani, kufunga milango ya uchumi wao kama walivyokuwa wamefanya China ya Mao, ndiko kutakowaokoa kumbe sio kweli.

Mambo makubwa mawili nimejifunza, ni kwa vipi kushusha thamani ya fedha yako kunaweza kuchangia kukua kwa uchumi wa nchi yako. jambo la pili; nini thamani ya kuzalisha mali kwa kutumia watu badala ya mashine.

Rais mteule wa Amerika, Mheshimiwa Ronald Trup, anailaumu China kwa kushusha thamani ya fedha zake kwa kiwango cha juu sana. Na dhana hii inasaidia kukua kwa uchumi wa China kwa sababu wanacho cha kuuza nje. Wana vitu vingi vilivyozalishwa kwa gharama ndogo dhidi ya bidhaa ya za Amerika na ulaya ambazo ni aghari sana. Mtu akiwa na $ 10 anaweza kupata vitu vingi kutoka china, ukulinganisha na vile ambavyo vimezalishwa na viwanda vya ulaya na Amerika.

Nimalizie kwa kusema sera za ujamaa zilizolenga mapinduzi ya mila za kichina zimehakisha kuwafikisha hapa walipo, kiasi kwamba sasa wanatetea ambayo yalikuwa yanafanywa na wanyonyaji wa dunia na wele waliokuwa wanayatetea sasa wanayapinga.

Unapotumia watu wako kuzalisha bidhaa, unawawezesha kuuza ujuzi, maarifa na jitihada zao nao wanapata kipato. Tabia hii ina nguvu nyingi China kwa maana watu ni wengi sana na wanashindana kila kukicha. Mashindano hayo ndiyo chachu ya kukua kwa uchumi wa nchi yao.

Trump na May wajue Amerika na Wingereza hazitakuwa zilivyokuwa hapo awali.
 
Ukishasema watu wanashindana hapo hamna ujamaa tena. Katika ujamaa kuna kubweteka na kuridhika na kuleta uvivu wa kufikiri kwa sababu unajua hata kama hufanyi kazi maadam ni umoja utaishi tu.

Ubepari ndo msingi wote wa maendeleo, mnacompete kuwa juu. Ujamaa hakuna ushindani, hakuna ubunifu na mnabweteka kusaidiwa kufukiria. Watanzania itikadi za ujamaa ndo zimetufikisha hapa hatuwezi kufikiria nje ya box maana tulushazoea kusaidiwa kufikiria, kusaidiana so mtu hawazi kesho yake maana ujamaa utamsaidia. Ndo maana tunashika mkia tu kila wakati.

Hata East Africa communities tuingie basi kibiashara bado tunaogopa competition coz hatujui kushindana kisa ujamaa. Dunia ya leo ukiendekeza ujamaa lazima uchumi wako ufe kimoja. Lazima uishi kibepari kama nchi uangalie rasilimali za wengine utafute namna ya kuzichukua kukuza uchumi wa nchi yako.

Ujamaa hauna nafasi kwenye dunia ya leo
 
Ukishasema watu wanashindana hapo hamna ujamaa tena. Katika ujamaa kuna kubweteka na kuridhika na kuleta uvivu wa kufikiri kwa sababu unajua hata kama hufanyi kazi maadam ni umoja utaishi tu.

Ubepari ndo msingi wote wa maendeleo, mnacompete kuwa juu. Ujamaa hakuna ushindani, hakuna ubunifu na mnabweteka kusaidiwa kufukiria. Watanzania itikadi za ujamaa ndo zimetufikisha hapa hatuwezi kufikiria nje ya box maana tulushazoea kusaidiwa kufikiria, kusaidiana so mtu hawazi kesho yake maana ujamaa utamsaidia. Ndo maana tunashika mkia tu kila wakati.

Hata East Africa communities tuingie basi kibiashara bado tunaogopa competition coz hatujui kushindana kisa ujamaa. Dunia ya leo ukiendekeza ujamaa lazima uchumi wako ufe kimoja. Lazima uishi kibepari kama nchi uangalie rasilimali za wengine utafute namna ya kuzichukua kukuza uchumi wa nchi yako.

Ujamaa hauna nafasi kwenye dunia ya leo

Na shukuru kwa mchango wako wa mawazo, sisi hatukuwahi kujenga ujamaa kwa maana ya ujamaa, ila tuliwahi kuwa na nia hiyo na kwa hiyo tulitamka hadharani. Hatua chache tulizozichukua ziliwezesha watu wengi kusoma, kuwa na viwanda vingi ikilinganishwa na sasa.

Hata hivyo nguvu tuliyoitoa kwenye ujamaa, itaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi bora kabisa Africa siku sio nyingi kuanzia sasa. Tanzania imehifadhi rasmali zake vizuri, hasa ardhi na madini, Tanzania ina watu wengi wazalendo, ikilinganishwa na nchi zilizotuzunguka. Na kama tunataka kutoka hapa tulipo tukiamua kutumia raslimali watu tuliyonayo, hatukamatiki.

Hebu angalia shirika la nyumba linavyofanya kazi na nipe mfano wake kwa nchi zilizotuzunguka. Hebu angalisha NHIF inavyopaaa na ilinganishe na nchi nyingine, hebu niambie nani sasa anapeleka watototo wake kusoma Uganda na Kenya?.
Kinachoongelewa hapa ni kwamba hakuna ujamaa unaowezajiendea kivyake vyake ukafanikiwa na wala hakuna ubepari unaoenda kivyake vyake ukafika popote. Ndio maana nimesema walichokuwa wanatetea wajamaa wa china sasa hawakubaliani nacho na walichokuwa wanatetea Wamarekani na waingirenza sasa wanakipinga. Au hauamini kuwa China ni nchi ya kijamaa na inaongozwa na chama cha kikomunisti?
 
Raisi mteule wa Amerika Ronald Trup???? Amerika ni mabara sawa nakubali, kusini na kaskazini sasa sijui huyo ni raisi wa nchi gani katika hayo mabara mawili?
Kiongozi hayo mambo ya ujamaa yalikwisha zikwa na azimio la zanzibar baada ya watu kukaa chini na kuona hayana msaada kwa wananchi wetu.
 
Hivi china ni nchi ya mfano kweli???

Ndiyo. 1950, ilikuwa kati ya nchi zenye uchumi mdogo kabisa duniani, leo hii ni nchi ya pili yenye uchumi mkubwa duniani. China haijaiba raslimali za nchi nyingine kama walivyofanya Amerika na Ulaya. Ni nchi ya mfano.
 
Baki na ujamaa wako.Chna ujamaa upo mdomoni (uongozi) ukapitalist upo kwenye kazi na biashara zao.Mambo ya ujamaa kwa bara la afrika ni ngumu kufanikiwa kama ulivyo jaribiwa ukashindikana.
 
Raisi mteule wa Amerika Ronald Trup???? Amerika ni mabara sawa nakubali, kusini na kaskazini sasa sijui huyo ni raisi wa nchi gani katika hayo mabara mawili?
Kiongozi hayo mambo ya ujamaa yalikwisha zikwa na azimio la zanzibar baada ya watu kukaa chini na kuona hayana msaada kwa wananchi wetu.
Umeongelea sana kichwa cha habari haujaongelea dhana kama kushusha thamani ya fedha, haujaongelea matumizi ya watu dhidi ya teknologia! Haujajadili nguvu ya china katka uchumi wa dunia. Nifundishe ninafundishika,
 
Raisi mteule wa Amerika Ronald Trup???? Amerika ni mabara sawa nakubali, kusini na kaskazini sasa sijui huyo ni raisi wa nchi gani katika hayo mabara mawili?
Kiongozi hayo mambo ya ujamaa yalikwisha zikwa na azimio la zanzibar baada ya watu kukaa chini na kuona hayana msaada kwa wananchi wetu.

Nisamehe nimekosea, niliimanisha Ronald Trump na sio Ronald Trup, America ya kaskazini (USA). Sijasema tujenge ujamaa, nakubaliana na wewe kwamba ukisafiri kwa basi hadi ukafika baharini, chombo kinachohitajika kukuvusha sio gari tena.
 
Watu wakishindana kwenye biashara hapo hakuna tena sera ya ujamaa au sera ya kikomunisti. Watu wakianza kushindana vile wanavyozalisha mali, wanavyouza na hatimaye kupata faida hapo tayari sera za soko huru zinatamalaki.

Hao wachina sasa hivi wanatumia sera za kijamaa zaidi kwenye masuala yanahohusu jamii, utamaduni, wao kama taifa. Lakini kwenye biashara sasa hivi ni cut-throat competition ni kushindana tu.

Wachina wengi wakiingia middle class level wataanza kudai mishahara bora zaidi kama ya wenzao huko Europe. Sera za nchi zitabadilika tu, zitakuja changamoto mpya ambazo watu wa Ulaya tunaona wanapitia leo.

Kujenga uchumi ni hatua.

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Jan huko Devos, Switzerland; rais wa China ya Mao alitetea utandawazi wakati Waingereza na wamerakani wanatetea kulinda viwanda vyao. Wamebanwa mbavu, hawana njia nyingine ya kupumua, na kwa bahati mbaya hawataokoka.
Waingereza na Wamarekani wanadhani, kufunga milango ya uchumi wao kama walivyokuwa wamefanya China ya Mao, ndiko kutakowaokoa kumbe sio kweli.

Mambo makubwa mawili nimejifunza, ni kwa vipi kushusha thamani ya fedha yako kunaweza kuchangia kukua kwa uchumi wa nchi yako. jambo la pili; nini thamani ya kuzalisha mali kwa kutumia watu badala ya mashine.

Rais mteule wa Amerika, Mheshimiwa Ronald Trup, anailaumu China kwa kushusha thamani ya fedha zake kwa kiwango cha juu sana. Na dhana hii inasaidia kukua kwa uchumi wa China kwa sababu wanacho cha kuuza nje. Wana vitu vingi vilivyozalishwa kwa gharama ndogo dhidi ya bidhaa ya za Amerika na ulaya ambazo ni aghari sana. Mtu akiwa na $ 10 anaweza kupata vitu vingi kutoka china, ukulinganisha na vile ambavyo vimezalishwa na viwanda vya ulaya na Amerika.

Nimalizie kwa kusema sera za ujamaa zilizolenga mapinduzi ya mila za kichina zimehakisha kuwafikisha hapa walipo, kiasi kwamba sasa wanatetea ambayo yalikuwa yanafanywa na wanyonyaji wa dunia na wele waliokuwa wanayatetea sasa wanayapinga.

Unapotumia watu wako kuzalisha bidhaa, unawawezesha kuuza ujuzi, maarifa na jitihada zao nao wanapata kipato. Tabia hii ina nguvu nyingi China kwa maana watu ni wengi sana na wanashindana kila kukicha. Mashindano hayo ndiyo chachu ya kukua kwa uchumi wa nchi yao.

Trump na May wajue Amerika na Wingereza hazitakuwa zilivyokuwa hapo awali.
Ni njia sahihi ya kwenda kwenye umasikini sio kutoka kwenye umasikini. Wachina sio wajamaa soma historia na current international affairs. Just remember one thing, theoretically socialism sounds well but practically it has proved fiasco
 
Ndiyo. 1950, ilikuwa kati ya nchi zenye uchumi mdogo kabisa duniani, leo hii ni nchi ya pili yenye uchumi mkubwa duniani. China haijaiba raslimali za nchi nyingine kama walivyofanya Amerika na Ulaya. Ni nchi ya mfano.
We kumbe huijui China!!

Eti hawaibi rasilimali.
 
Na shukuru kwa mchango wako wa mawazo, sisi hatukuwahi kujenga ujamaa kwa maana ya ujamaa, ila tuliwahi kuwa na nia hiyo na kwa hiyo tulitamka hadharani. Hatua chache tulizozichukua ziliwezesha watu wengi kusoma, kuwa na viwanda vingi ikilinganishwa na sasa.

Hata hivyo nguvu tuliyoitoa kwenye ujamaa, itaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi bora kabisa Africa siku sio nyingi kuanzia sasa. Tanzania imehifadhi rasmali zake vizuri, hasa ardhi na madini, Tanzania ina watu wengi wazalendo, ikilinganishwa na nchi zilizotuzunguka. Na kama tunataka kutoka hapa tulipo tukiamua kutumia raslimali watu tuliyonayo, hatukamatiki.

Hebu angalia shirika la nyumba linavyofanya kazi na nipe mfano wake kwa nchi zilizotuzunguka. Hebu angalisha NHIF inavyopaaa na ilinganishe na nchi nyingine, hebu niambie nani sasa anapeleka watototo wake kusoma Uganda na Kenya?.
Kinachoongelewa hapa ni kwamba hakuna ujamaa unaowezajiendea kivyake vyake ukafanikiwa na wala hakuna ubepari unaoenda kivyake vyake ukafika popote. Ndio maana nimesema walichokuwa wanatetea wajamaa wa china sasa hawakubaliani nacho na walichokuwa wanatetea Wamarekani na waingirenza sasa wanakipinga. Au hauamini kuwa China ni nchi ya kijamaa na inaongozwa na chama cha kikomunisti?

Kupeleka watoto kusoma Kenya na Uganda hiyo ni sifa kweli, thumb down broda,,

Na kama wale waliokuwa wanapeleka watoto Kenya sasa hv hawapeleki tena, jiulize kwa nini hawapeleki tena? Ni kwa sababu ya ubepari ulianza kukubaliwa Tanzania au kwa sababu ya ujamaa? Ukishapata jibu hapa utajua msingi wa maendeleo ya kweli upo kwenye ujamaa au ubepari.
 
Kupeleka watoto kusoma Kenya na Uganda hiyo ni sifa kweli, thumb down broda,,

Na kama wale waliokuwa wanapeleka watoto Kenya sasa hv hawapeleki tena, jiulize kwa nini hawapeleki tena? Ni kwa sababu ya ubepari ulianza kukubaliwa Tanzania au kwa sababu ya ujamaa? Ukishapata jibu hapa utajua msingi wa maendeleo ya kweli upo kwenye ujamaa au ubepari.

Ninaamini watu wamepunguza kupeleka watoto Kenya na Uganda kwa sababu walichokuwa wanakifuata kule kinapatikana hapa. Swali ambalo lingekuwa gumu kwangu: "Ni kwa sababu ya ubepari ulianza kukubaliwa Tanzania au kwa sababu ya ujamaa?" Nimetoa mfano huo, kuonyosha Tanzania isivyokuwa nyuma kwa sababu ya ujamaa iliyokuwa inataka kuujenga na kwamba bado inaweza kwenda mwendo wa chura( leap frog) na kuzifikia na hatimaye kuzipita nchi zile zilizotangulia.
Kama umefuatilia Kigoda cha Mwalimu kinachoendeshwa na chuo kikuu cha Dar- utagundua kuwa kwa sasa watu wamegundua uzuri wa mfumo wa kijamaa na mapungufu yake.

Na bado tupo watu, tunaoamini kuwa mfumo huu ukitekelzwa na watu wanoujua vizuri, tunaweza kwenda haraka na kufika pale tunapotaka kufika ndani ya muda mfupi inavyowezekana. Ninajua hakuna mfumo mbao ni imara sehemu zote.
Fikiria kidogo, matumizi ya raslimali na raslimali watu tuliyonayo kama tutazitumia kwa misingi ya kijamaa, taifa litafika wapi katika kipindi kifupi.
 
Ukishasema watu wanashindana hapo hamna ujamaa tena. Katika ujamaa kuna kubweteka na kuridhika na kuleta uvivu wa kufikiri kwa sababu unajua hata kama hufanyi kazi maadam ni umoja utaishi tu.

Ubepari ndo msingi wote wa maendeleo, mnacompete kuwa juu. Ujamaa hakuna ushindani, hakuna ubunifu na mnabweteka kusaidiwa kufukiria. Watanzania itikadi za ujamaa ndo zimetufikisha hapa hatuwezi kufikiria nje ya box maana tulushazoea kusaidiwa kufikiria, kusaidiana so mtu hawazi kesho yake maana ujamaa utamsaidia. Ndo maana tunashika mkia tu kila wakati.

Hata East Africa communities tuingie basi kibiashara bado tunaogopa competition coz hatujui kushindana kisa ujamaa. Dunia ya leo ukiendekeza ujamaa lazima uchumi wako ufe kimoja. Lazima uishi kibepari kama nchi uangalie rasilimali za wengine utafute namna ya kuzichukua kukuza uchumi wa nchi yako.

Ujamaa hauna nafasi kwenye dunia ya leo
wala hujui itikadi ya ujamaa inafanya kazi vipi. umekurupuka tu na kutoa maelezo sterio type. huku ukielezwa jinsi china ilivyofanikiwa kukuza uchumi wake na kiwango cha maisha ya watu wake kwa kufuata sera ya ujamaa unaleta propaganda za wamarekani wakati wa vita baridi...wewe ndio uko ndani ya box.
 
wala hujui itikadi ya ujamaa inafanya kazi vipi. umekurupuka tu na kutoa maelezo sterio type. huku ukielezwa jinsi china ilivyofanikiwa kukuza uchumi wake na kiwango cha maisha ya watu wake kwa kufuata sera ya ujamaa unaleta propaganda za wamarekani wakati wa vita baridi...wewe ndio uko ndani ya box.

Sio kweli naijua sana itikadi ya ujamaa inasimamia vitu gani;
1. Uchumi upangwa na serikali/umma( central planning), uchumi unapngwa kulingana na uhitaji na sio kupata faida kubwa.
2. Njia kuu za uchumi zinamilikiwa na umma(
3. Hakuna mtu anaruhisiwa kumnyonya mwenzie( wanao ruhusiwa kunyonya, ni watoto, wazee sana na wote wasi jiweza), kila mtu afanye kazi sio kulingana na mahitaji yake bali kulingana na uwezo wake.
4. Mgawanyo kulingana na mahitaji na sio kulingana na uwezo wakuzalisha.

- Ni saidie jambo moja, uchumi wa china ni wangapi duniani?
- China ina mfumo gani rasmi wa uchumi( itikadi yake)?
 
Back
Top Bottom