Uitishwe uhakiki wa vyeti kwa wateule wa Mheshimiwa Rais wote

Say no to actors

JF-Expert Member
Aug 9, 2016
637
640
Habari za mchana wadau,

Mimi "say no to actors" baada ya kusikiliza mjadala unaoendelea katika mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, makanisani, misikitini pamoja na mitaani juu ya tuhuma za baadhi ya wateule wa Mheshimiwa Rais kutumia vyeti vya taaluma visivyokuwa vya kwao mmojawapo akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ndugu Paul Makonda, napendekeza uhakiki wa vyeti ufanyike kwa wateule wa huyu mheshimiwa.

Hii inatokana na serikali kupitia wizara ya elimu na wizara ya utumishi kuutangazia umma kuwa kunafanyika uhakiki wa vyeti kwa watumishi WA umma zoezi ambalo limepelekea watu kuachishwa/ kuacha kazi, kushushwa vyeo, watumishi kutolipwa stahiki zao, na hata kusitisha ajira.

Ni matumaini yangu kama mtanzania ambaye nami naguswa na hili jambo kuona haki inatendeka kwa wateule wote wa Mheshimiwa Rais kufanyiwa uhakiki na ikishabainika kuwa Kuna mtu/watu wanaotumia vyeti vya watu basi hatua Kali zichukuliwe dhidi ya:

1: mhusika anayetumia vyeti/ cheti kisichokuwa cha kwake.

2: usalama wa taifa uwajibishwe kwa kutokuwa makini katika hili mpaka kupelekea taifa kupata aibu ya kuongozwa na viongozi vilaza na wanaostahili kumtumikia kifungo magereza.

3: Mheshimiwa Rais kujitokeza hadharani kuomba wananchi msamaha kwa kuwadanganya kuwa alitumia muda WA kutosha WA kuwafuatilia watu wanaofaa kuteuliwa na mbele ya vyombo vya habari kasema amejiridhisha VYA kutosha na elimu zao na pia amekagua na vyeti.

4: Wizara zinazohusika kuhakiki vyeti zichukuliwe hatua dhidi ya ubabaishaji WA makusudi walioufanya mpaka kupelekea hawa watu ambao mbali na kuteuliwa na Rais kwa mjibu wa sheria Ni watumishi wa umma ambao tungetegemea hizi wizara ndizo ziibue madudu Haya kabla ya wananchi wa kawaida.

Pia katika kuhakiki vyeti vya hawa watu hizi wizara zisihusike na badala yake liundwe jopo la wataalam wasiofungamana na upande wowote ili tupate majibu sahii na kwa wakati. Narudia kuwa natilia shaka serikali kuhusika kwenye uhakiki huu kwani kutskuwepo na uwezekano mkubwa wa kufanya kitu "Funika kombe mwanaharamu apite".

By Kamanda wa KIRIBA kwa sasa ARUSHA kuhakikisha LISSU anakuwa Rais wa TLS.
 
NdNdichakoo kimya gafla.....akiwagusa wale aliyozoea kuwapelekesha.....ataulizwa vp Mbn unamuacha bashite!

Ova
 
yaaani hv hakuna kweli mwenye ushahidi wa vyeti vya daudi.... vingetupiwamo humu jamani tumalize mzizi wa fitna maana tushachoka sasa.....

miss tz alibwaga manyanga baada ya usahidi kutupiwamo humu... sasa bila hilo kelele zote hizi zitakua ni bure kabisa....

fanyeni fanyeni basi tuhamie kwenye ishu mpya!!! woooiii
 
Mbona Mbowe unamuacha pembeni, kama nia ni kuondoa vihiyo mwambie Mbowe na yeye aweke cheti chake hadharani.
 
Ukitaka mkosana na sizonje wew sena uhakiki wa vyeti kwa wateule wake
 
Vile Makonda anaiangalia hii post
download-9.jpg
 
Una utani wewe!
Madudu yatakayo kutwa humo sijui nani atayaziba!

Nilicho jifunza kwenye hii kadhia ya bashite.....aisee hakuna kitu kizuri kama kukazana darasani!
Nimepata vivid example ya kuwaasa wanangu hapo baadae
 
yaaani hv hakuna kweli mwenye ushahidi wa vyeti vya daudi.... vingetupiwamo humu jamani tumalize mzizi wa fitna maana tushachoka sasa.....

miss tz alibwaga manyanga baada ya usahidi kutupiwamo humu... sasa bila hilo kelele zote hizi zitakua ni bure kabisa....

fanyeni fanyeni basi tuhamie kwenye ishu mpya!!! woooiii
Sasa kama mtu ana 0 cheti kinatoka wapi?

Ndio maana watu wanaomba aoneshe cheti chake cha form four kilichomfanya aendelee na elimu yake hadi kufikia kupata degree pale MUCCoBS kwa Prof F.Bee.
 
Sasa kama mtu ana 0 cheti kinatoka wapi?

Ndio maana watu wanaomba aoneshe cheti chake cha form four kilichomfanya aendelee na elimu yake hadi kufikia kupata degree pale MUCCoBS kwa Prof F.Bee.

namaanisha hata hvyo ambavyo vinasemekana vipo... vya kubadli majina.. vya chuo ama vyovyote japo tuanze na kaushahidi kamojawapo... hata basi matokeo kwa ujumla jamani... yaaani nakwambia lasivyo hizi zitakua kelele tu.

hlf kumbuka watu ndo tunamtuhumu ... hata tukienda mahakamani jaji atatuuliza huo ushahidi wa hizo tuhuma mnazozitoa uko wapi.. as much as tunataka this person awe guilty kutokana na mienendo na maneno yake ya karaha .. lkn bila kuthibitisha hizi tuhuma tutafeli kwa kweli
 
yaaani hv hakuna kweli mwenye ushahidi wa vyeti vya daudi.... vingetupiwamo humu jamani tumalize mzizi wa fitna maana tushachoka sasa.....

miss tz alibwaga manyanga baada ya usahidi kutupiwamo humu... sasa bila hilo kelele zote hizi zitakua ni bure kabisa....

fanyeni fanyeni basi tuhamie kwenye ishu mpya!!! woooiii

yote hayo ya nini dadangu, suala hapa ni Daudi Bashite atoe cheti chake cha form 4!
 
yote hayo ya nini dadangu, suala hapa ni Daudi Bashite atoe cheti chake cha form 4!

maana yangu midhali tunamtuhumu... tutoe ushahidi wa kitu tunachomtuhumu... hlf yeye aje akanushe ushahidi kwa kutoa wa kwake... unadhani kwanini kapata jeuri ya kusema hajibu tuhuma za mtandaoni?? unadhani tungekua tumeweka japo vyeti vyake vya chuo angenyamaza??? angekuja tu hapa ila kwa kuwa tunaongea bila matendo ndo anatupotezea

ni kama vile tulivyomtuhumu yeye kutaja majina ya watu hadharani bila kuwa na ushahidi ... em tumtoe hyo jeuri yake kwa kuonyesha ukweli wa tuhuma

hata wewe nikikuuliza kwanini unaamini tuhuma hizi utajibuje???
 
Sasa aitishe nani huo uhakiki. Kikatiba suala la teuzi la Rais ni ridhaa yake halina ubia na mtu. Huo ndio ukweli mchungu.
 
Hata Mheshimiwa Mpendwa Rais wetu vyeti vyake vihakikiwe pia. Nimepoteza imani na uongozi mzima.
 
Sasa kama mtu ana 0 cheti kinatoka wapi?

Ndio maana watu wanaomba aoneshe cheti chake cha form four kilichomfanya aendelee na elimu yake hadi kufikia kupata degree pale MUCCoBS kwa Prof F.Bee.
Na ikidhibitika alitumia jina au cheti cha mwingine hiyo degree inatakiwa ifutwe na yeye ashitakiwe na kurudisha pesa zote alizopokea kama mshahara baada ya kuajiriwa.
 
Back
Top Bottom