Uingizaji sukari vs uingizaji mayai, tuache unafiki

Uingizaji sukari vs uingizaji mayai, tuache unafiki

Technology

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
769
Reaction score
284
Mara kadhaa wafugaji wa kuku tumekua tunalalamikia serikali kutodhibiti uingizaji wa mayai toka Kenya kwani unakaribia soko la ndani na mayai kufikiri kuoza kwa kukosa soko, kwakua wafugaji wakubwa, Kati na wadogo tuko zaidi ya 20000 na wengi wana madeni makubwa ktk taasisi za mikopo/fedha.

Members wengi wa jamii forums ni wanafiki, wamekua wanapinga uingizaji wa sukari toka nje eti unaharibu ajira za ndani na soko pamoja na kuua viwanda, jibuni haya maswali

1. Idadi ya wafugaji wa kuku na idadi yawauajiriwa wa viwanda Vya sukari ili kubwa (sitetei hao waingizaje ieleweke)
2. Wenye viwanda wanaweza kwenda kuuza hata Congo, je mayai utapelekea Congo kwa mitaji ya mikopo
3. Si unafiki kutembea kundi dogo la wenye viwanda na kukaa kimya kwa bias hata za wafugaji ambapo wengi ni wayang na wastaafu
4. Clouds radio waliweka muda Maalumu kuisemea issue ya sukari kwakua walihongwa na wenye viwanda, sisa wajasiriamali hatuna cha kuongea hivyo ni Sawa kuonewa?
 
Mara kadhaa wafugaji wa kuku tumekua tunalalamikia serikali kutodhibiti uingizaji wa mayai toka Kenya kwani unakaribia soko la ndani na mayai kufikiri kuoza kwa kukosa soko, kwakua wafugaji wakubwa, Kati na wadogo tuko zaidi ya 20000 na wengi wana madeni makubwa ktk taasisi za mikopo/fedha.

Members wengi wa jamii forums ni wanafiki, wamekua wanapinga uingizaji wa sukari toka nje eti unaharibu ajira za ndani na soko pamoja na kuua viwanda, jibuni haya maswali

1. Idadi ya wafugaji wa kuku na idadi yawauajiriwa wa viwanda Vya sukari ili kubwa (sitetei hao waingizaje ieleweke)
2. Wenye viwanda wanaweza kwenda kuuza hata Congo, je mayai utapelekea Congo kwa mitaji ya mikopo
3. Si unafiki kutembea kundi dogo la wenye viwanda na kukaa kimya kwa bias hata za wafugaji ambapo wengi ni wayang na wastaafu
4. Clouds radio waliweka muda Maalumu kuisemea issue ya sukari kwakua walihongwa na wenye viwanda, sisa wajasiriamali hatuna cha kuongea hivyo ni Sawa kuonewa?
inaonekana huelewi unachokisema kuhusu kile kinachoitwa 'uingizaji hovyo wa sukari'. iko hivi: ukisoma East Africa Customs Management Act, 2004 na East Africa Common External Taiff, 2012 utaona sukari ipo kwenye kundi la sensitive items (SI). ikimaanisha uingizaji wake ni wa uangalizi, hairuhusiwi kuingizwa hovyo na ndio maana import duty hufika mpaka 100% ili kulinda uzalishaji wa ndani (hii inafanyika popote pale duniani kwenye uzalishaji wa bidhaa itakayohitaji ulinzi wa kibiahara ili kukuza uchumi). endapo kuna upungufu wa sukari nchini serikali inatoa vibali vya muda maalum kwa wafanyabiashara kuingiza sukari (import duty inapunguzwa mpaka 25% ama 0% kabisa kutegemea na uhitaji). vibali hivyo vinaonesha kiasi cha sukari inayohitajika, na kiasi kikitimia hairuhusiwi kuingiza tena. kinachotokea sasa kwenye soko la sukari ni kwamba kuna baadhi wa wafanyabiashara wanatumia 'vibali vya muda maalum' vilivyotolewa na ofisi za serikali kinyume cha utaratibu (the scandal will soon erupt, just wait). hawa 'wafanyabiashara wakubwa' walio na urafiki wa karibu na 'mamlaka' husika za kutoa vibali wanaingiza kinyume na utaratibu na mbaya zaidi kuna wanaopaki kwenye packages zenye nembo za sukari ya hapa nchini. hii ndio sababu kubwa ya wazalishaji wa ndani kulalamikia 'uingizwaji hovyo wa sukari'!
 
Kwani wafugaji hamna chama chenu cha kuongea kwa niaba yenu??
 
inaonekana huelewi unachokisema kuhusu kile kinachoitwa 'uingizaji hovyo wa sukari'. iko hivi: ukisoma East Africa Customs Management Act, 2004 na East Africa Common External Taiff, 2012 utaona sukari ipo kwenye kundi la sensitive items (SI). ikimaanisha uingizaji wake ni wa uangalizi, hairuhusiwi kuingizwa hovyo na ndio maana import duty hufika mpaka 100% ili kulinda uzalishaji wa ndani (hii inafanyika popote pale duniani kwenye uzalishaji wa bidhaa itakayohitaji ulinzi wa kibiahara ili kukuza uchumi). endapo kuna upungufu wa sukari nchini serikali inatoa vibali vya muda maalum kwa wafanyabiashara kuingiza sukari (import duty inapunguzwa mpaka 25% ama 0% kabisa kutegemea na uhitaji). vibali hivyo vinaonesha kiasi cha sukari inayohitajika, na kiasi kikitimia hairuhusiwi kuingiza tena. kinachotokea sasa kwenye soko la sukari ni kwamba kuna baadhi wa wafanyabiashara wanatumia 'vibali vya muda maalum' vilivyotolewa na ofisi za serikali kinyume cha utaratibu (the scandal will soon erupt, just wait). hawa 'wafanyabiashara wakubwa' walio na urafiki wa karibu na 'mamlaka' husika za kutoa vibali wanaingiza kinyume na utaratibu na mbaya zaidi kuna wanaopaki kwenye packages zenye nembo za sukari ya hapa nchini. hii ndio sababu kubwa ya wazalishaji wa ndani kulalamikia 'uingizwaji hovyo wa sukari'!
idoyo, it seems you are those kind of people who believes on employment, we are not! Umeandika pumba Tupu.. Ninachozungumzia Mimi ni impact ya uingizaji wa fast moving products Kama mayai na impact yake kwa maelfu ya wajasiriamali. Serikali inawasaidiaje hawa? You make yourself look stupid
 
Kwani wafugaji hamna chama chenu cha kuongea kwa niaba yenu??
Mkuu tumejaribu kukutana Mara kadhaa pale UDSM, however the turnout was more than dis pointing . Yet we can't negotiate prices za vyakula Vya kuku ilihali eggs price inakwenda chin daily
 
Wafugaji chama chao hakina nguvu. Msaada wao ni pale kunapokuwa na risk analysis from exporting countries ndiyo Director of veterinary services anapiga marufuku. Mfano kwa sasa kama kuna outbreak ya magonjwa kama bird flu (avian influenza) katika nchi fulani basi linatolewa tangazo kuwa hatutaingiza kuku na mazao yake toka ile nchi. Kama wangekuwa na chama kizuri basi kingefanya analysis na kuishauri serikali isiingize mayai toka nje ili kulinda soko la ndani
 
Sukari Tanzania inatumika kama silaha. Wiki jana kwa mfano Mwanza Sukari 50kg ilikuwa Tsh 70,000/= leo 80, 000/= kisa sukari ya nje imepigwa mkwara. Kabla ya hapo walidai ni heri wafunge viwanda kwani sukari zimejaa stooni iweje leo bei ipande kwa kiasi hiki!! Nadhani kuna haja ya kuangalia vema hii sera kwani kuna watu wanaumiza wenzao kwa kumonopolize biashara ya sukari hasa Mwanza.
 
idoyo, it seems you are those kind of people who believes on employment, we are not! Umeandika pumba Tupu.. Ninachozungumzia Mimi ni impact ya uingizaji wa fast moving products Kama mayai na impact yake kwa maelfu ya wajasiriamali. Serikali inawasaidiaje hawa? You make yourself look stupid
mayai ≠ sukari. jipange!
 
mayai ¡Ù sukari. jipange!

kitunda baada ya nyumba 2 kuna mfugaji, kwetu hoja ya mayai = hoja ya sukari.
Labda hoja ya mayai ikawa ya muhimu zaidi kwetu.
 
Wafugaji chama chao hakina nguvu. Msaada wao ni pale kunapokuwa na risk analysis from exporting countries ndiyo Director of veterinary services anapiga marufuku. Mfano kwa sasa kama kuna outbreak ya magonjwa kama bird flu (avian influenza) katika nchi fulani basi linatolewa tangazo kuwa hatutaingiza kuku na mazao yake toka ile nchi. Kama wangekuwa na chama kizuri basi kingefanya analysis na kuishauri serikali isiingize mayai toka nje ili kulinda soko la ndani
Mkuu tumekwenda wizara ya mifugoi several times na jibu wanalotoa ni Kwamba kazi Yao si kulinda mipaka. Iniumiza sana
 
idoyo, it seems you are those kind of people who believes on employment, we are not! Umeandika pumba Tupu.. Ninachozungumzia Mimi ni impact ya uingizaji wa fast moving products Kama mayai na impact yake kwa maelfu ya wajasiriamali. Serikali inawasaidiaje hawa? You make yourself look stupid

Sasa mbona badala ya kueleza kutetea unachomaanisha unashutumu na kutukana watu,!!!!tafuta nama nzuri ya
kuungwa mkono si kwa njia ya kumlazimisha kila mtu aamini kile unachoamini wewe!!!
 
Sasa mbona badala ya kueleza kutetea unachomaanisha unashutumu na kutukana watu,!!!!tafuta nama nzuri ya
kuungwa mkono si kwa njia ya kumlazimisha kila mtu aamini kile unachoamini wewe!!!

Nitetetee nini! ! Huo ni wajibu wa serikali Yenu ya kidhalimu. Kama hawawezi wasubiri 2015
 
baada ya kuona mleta mada anamuandikia mwenzake "umeandika pumba" nimesita hata kuandika maana duh! jamaa anaonekana kua aggressive sana
 
Serikali ina calm the market kwa kuongeza supply... Nyie c mlitakamtupige na kutajirikia kupitia sukari na mayai? Sasa imekula kwenu...
 
I am all for free movement of goods and services in EAC kwakweli wakulima na wazalishaji watanzania mmezidi kutulanguwa. Wacha saruji iletwe, sukari, mpaka miswaki ikibidi.

Bora tuletewe imports tu at cheaper prices kuliko kuangaika na nyinyi mpaka mtakapo jifunza amuwezi kukamua damu maiti. Mayai yatakuozea vipi unless labda umeshaweka bei yako kichwani mwako, kama bei zako zinaendana na majukumu ya uzalishaji na mikopo unatakiwa uwaambie serikari kuangalia riba za mikopo lakini sisi wateja tushachoka mayai yawe chakula cha kina nanilii tu na sisi je.

Waje tu wajenzi wa nyumba wanaotoka na capital nchi za nje na wengine wengi tu kila kona watanzania hakuna kitu wanachoweza zaidi ya ulanguzi i am beginning to think ata wakenya wenye malengo ya kuuza soko la ndani kwetu kwenye kilimo wapewe ardhi tumezidi kuzubaa na kukosa ubunifu, bei ya kifuko cha korosho dar kitakuwa vipi sawa na london. Wakati korosho inatoka mtwara tu something is not right, wakati ya london imetoka mbali na imepitia industrial porecesses. Hapana kwakeli mmezidi kupenda utajiri wa haraka na sio wabunifu kabisa.
 
Mayai mnayotulisha ni yepi hayo

Yale ya jogoo kumpanda kuku au

Yale tusiyojua uzazi wake
 
inaonekana huelewi unachokisema kuhusu kile kinachoitwa 'uingizaji hovyo wa sukari'. iko hivi: ukisoma East Africa Customs Management Act, 2004 na East Africa Common External Taiff, 2012 utaona sukari ipo kwenye kundi la sensitive items (SI). ikimaanisha uingizaji wake ni wa uangalizi, hairuhusiwi kuingizwa hovyo na ndio maana import duty hufika mpaka 100% ili kulinda uzalishaji wa ndani (hii inafanyika popote pale duniani kwenye uzalishaji wa bidhaa itakayohitaji ulinzi wa kibiahara ili kukuza uchumi). endapo kuna upungufu wa sukari nchini serikali inatoa vibali vya muda maalum kwa wafanyabiashara kuingiza sukari (import duty inapunguzwa mpaka 25% ama 0% kabisa kutegemea na uhitaji). vibali hivyo vinaonesha kiasi cha sukari inayohitajika, na kiasi kikitimia hairuhusiwi kuingiza tena. kinachotokea sasa kwenye soko la sukari ni kwamba kuna baadhi wa wafanyabiashara wanatumia 'vibali vya muda maalum' vilivyotolewa na ofisi za serikali kinyume cha utaratibu (the scandal will soon erupt, just wait). hawa 'wafanyabiashara wakubwa' walio na urafiki wa karibu na 'mamlaka' husika za kutoa vibali wanaingiza kinyume na utaratibu na mbaya zaidi kuna wanaopaki kwenye packages zenye nembo za sukari ya hapa nchini. hii ndio sababu kubwa ya wazalishaji wa ndani kulalamikia 'uingizwaji hovyo wa sukari'!
Kwa tasfiri yangu (sijui kama ipo sahihi) ni kuwa unasema import ban kwenye sukari ni muhimu na inaongezewa nguvu na sheria lakini kwenye mayai sio muhimu. Kama una maanisha hivi unakosea sana. Japo tupo kwenye soko huria serikali ina role ya kulinda growth ya domestic industries iwe ni manufacturing, poultry or whatever. Kama imports ya mayai ni kubwa mpaka inatishia uhai wa poultry industry ya ndani, ni mtu na serikali ya ”wehu" pekee ndo wataruhusu hivyo. Ni jukumu la serikali kuweka sera na miongozo ya kulinda industries hizi maana zina mchango wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja kwenye uchumi wa nchi na kupunguza umaskini.
 
Back
Top Bottom