Uingereza na Israel hawana katiba sisi mishipa ya shingo inatutoka

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,487
13,611
Mheshimiwa Waziri wa sheria ameongea mengi wakati akitoa hotuba ya majumuisho ambayo huwa ni majibu na maelezo kwa yale yote yanayokuwa yameulizwa au yanawatatiza wabunge.

Ameongea mengi lakini yaliyonigusa zaidi ni pale aliposema kuwa Israel na Uingereza hawana katiba zilizoandikwa ambazo wanazotumia kama rejea halisi ya uongozi wa mataifa yao.

Mheshimiwa Kabudi akaenda mbali zaidi na kuelezea kuwa Zanzibar kuanzia mwaka 1964 mpaka mwaka 1979 haikuwa na katiba yoyote ile ya maandishi.

Maisha ya kisiasa ya Israel na Uingereza yanakwenda kama kawaida, wao wanazo mila na desturi ambazo kwa umoja wao wamekubaliana ndizo ziwe mwongozo wa kisiasa na kijamii. Hapa Tanzania wajuaji wanajaribu kila kukicha kutuambia kwamba bila ya katiba mpya basi maisha ya taifa yanakuwa na matatizo!.

Gwiji wa sheria labda kasahau kuiongelea Rwanda ambayo tangu Kagame aingie madarakani imekuwa ikizidi kujijengea heshima kimataifa pasipo kuweka msisitizo kwenye masuala ya katiba mpya.

Profesa Kabudi akaieleza jamii yetu kwamba hata huo utungwaji wa katiba yetu uliofanywa kwa mara ya kwanza na Waingereza, ulifanyika katika mtazamo wa dharau ndani yake!. Kwamba tuwaandikie hawa jamaa taratibu za kiutawala kwani wao wenyewe hawawezi kujiandikia.

Maana yake ni kwamba kadri taifa linavyozidi kukua kiumri na kupata watu wenye uwezo wa kuhoji kwa kina juu ya maisha yao ya kila siku, ipo haja ya kuipitia kwa undani hata katiba hii ambayo imejaa chembechembe za ukoloni.

Pia profesa Kabudi kaongelea namna ambavyo mheshimiwa rais asivyofunga safari za nje za mara kwa mara, sawa sawa na maoni ya wananchi wakati wa upatikanaji wa rasimu ya katiba ya Warioba.

Lipo fundisho kubwa kupitia namna ambavyo mheshimiwa waziri wa sheria Prof Kabudi alivyoongea bungeni, nalo ni kwamba wanaharakati wetu wanayo tabia ya kufaidika na jamii pana kutokuwa na taarifa nyingi kuhusu masuala ya katiba. Labda hufanya hivyo kwa nia binafsi lakini watambue kwamba wanachokiongea sio sawa na maneno ya kwenye misahafu.

Israel na Uingereza hawajaweka mkazo kwenye katiba zilizoandikwa lakini maisha yanakwenda kama kawaida.
 
Kukosa kwao katiba hakumaanishi hakuna sheria, lakini pia wenzetu wana displine, anafundisha kua na displine toka huko chini, kuheshimu haki za binadam, kuheshimu misingi ya demokrasia nk, haiwezi kutokea mtu akatokea tu huko alikotoka amevuta bangi akaleta mambo yake nje ya misingi ya taifa.

Kwa nji zetu masikini na tabia yetu ya kutoheshimu sheria na misingi ya taifa ni vigumu kuendelea, hebu fikiri leo Tanzania hatuka katiba ingekuaje, hapa tu mambo yako hovyo watu hawataki kushauriwa wala kupangiwa katiba ipo, je isingekuwepo si ndio ingekua balaa.

Katiba inahitajika kudhibiti watu wasiendeshe nchi kwa matakwa yao na kwa kutumia hisia zao.
 
Kwa hiyo Uingereza ndio reference yetu!? Haya basi Magufuli ndio awe mfalme wetu nadhani itakupendeza ngosha. Badilisheni tu katiba.

Acheni ujinga wenu. Huo upuuzi Wa rais Wa maisha uishie huko sukumaland.

Kuongezea na ushoga Wa uingereza muige pia.
 
Gwiji wa sheria labda kasahau kuiongelea Rwanda ambayo tangu Kagame aingie madarakani imekuwa ikizidi kujijengea heshima kimataifa pasipo kuweka msisitizo kwenye masuala ya katiba mpya.
Hauna uhakika na unachoandika, umesahau kuwa ni mwaka jana tu kagame kafanya mabadiliko ya katiba ili kumruhusu kuongeza term nyingine ya uraisi? Sasa kwa nini asingesubili kugombea bila kufanya mabadiliko ya katiba?
 
Uelewa wa hayo mataifa na sisi ni sawa na Giza nnuru
Wanazo katiba ila ziko kwenye nyaraka tofauti tofauti Uingereza wana ,bill of rights, petiton of rights, Magna carta, habeas corpus, Act of setlement na mengine na mengine na sheria za bunge na maamuzi mengine ya kimahakama. Kama prof kasema hawana katiba hapo naanza kuhisi Mwakiembenization.

Naanza kupata taabu sasa kama na huyu ametugeuka. Akiwa kwenye mdahalo wa katiba wakati ule alitwambia Tanzania na Congo ni nyonga za Africa na kwamba tusipoilinda Tanzania mabeberu wataigawana kama Congo na kwamba njia ya kuilinfa ni kuwapa watanganyika Tanganyika kabla hawajaidai.
 
Hii ni Tanzania siyo Islaeri wala Uingereza.Hatuwezi kufananishwa na hao watu kwa Rangi, Tamaduni, Mira, Destuli,Tabia na hata mazingira.Hapa kwetu tuna mamia ya makabira yenye mila na tamaduni zao.Tukifata ya Islaeli au Uingereza itawezekana kweli?

Huyu professor aache kutuona was Tanzania hatuwezi kufikiri.Afahamu kuwa tulikubaliana kama Taifa kubadili katiba yetu na gharama kubwa tulitumia kufanikisha jambo hilo.

Aache watu wadai kukamilishwa na hatimae katiba ipatikane. Anachopaswa yeye kufanya ni kutimiza wajibu wake kama waziri anayehusika na jambo hili, siyo kutuletea historia na tamaduni za Wayahudi na wazungu wa Uingereza. Siyo kipa umbele chetu, hayana tija kwetu wala hayatuhusu.
 
Mheshimiwa Waziri wa sheria ameongea mengi wakati akitoa hotuba ya majumuisho ambayo huwa ni majibu na maelezo kwa yale yote yanayokuwa yameulizwa au yanawatatiza wabunge...
Nilisema hakuna Professor Tanzania, njaa mwanamalegeza. Ujinga, unaweza linganisha mazingira ya kisiasa yetu na Israel Uingereza? Shame up on him Propesa No.2. Katiba ipo but is not written on paper as a single document kama nchi zilizonyingi. Hapa ni makabila 128, quite diferent, how do you live by mila na desturi. Jinga Propesa! Uingereza kuna akina Ben wanapotezwa, Kunyimwa dhamana miezi mine, Israel inaweza tokea? Shame Propesa No. 2

Britain's unwritten constitution

Unlike most modern states, Britain does not have a codified constitution but an unwritten one formed of Acts of Parliament, court judgments and conventions. Professor Robert Blackburn explains this system, including Magna Carta’s place within it, and asks whether the UK should now have a written constitution.

For most people, especially abroad, the United Kingdom does not have a constitution at all in the sense most commonly used around the world — a document of fundamental importance setting out the structure of government and its relationship with its citizens. All modern states, saving only the UK, New Zealand and Israel, have adopted a documentary constitution of this kind, the first and most complete model being that of the United States of America in 1788. However, in Britain we certainly say that we have a constitution, but it is one that exists in an abstract sense, comprising a host of diverse laws, practices and conventions that have evolved over a long period of time. The key landmark is the Bill of Rights (1689), which established the supremacy of Parliament over the Crown following the forcible replacement of King James II (r.1685–88) by William III (r.1689–1702) and Mary (r.1689–94) in the Glorious Revolution (1688).

From a comparative perspective, we have what is known as an ‘unwritten constitution’, although some prefer to describe it as ‘uncodified’ on the basis that many of our laws of a constitutional nature are in fact written down in Acts of Parliament or law reports of court judgments.
This aspect of the British constitution, its unwritten nature, is its most distinguishing characteristic.

Should the UK have a written constitution?
The question then arises in this 800th anniversary year — should the UK now take steps to codify all its laws, rules and conventions governing the government of the country into one comprehensive document, ‘a new Magna Carta’? The case for a written UK constitution has been debated at our universities and by politicians of all parties for several decades and has been the subject of a House of Commons committee inquiry during the 2010–15 Parliament. If a written constitution for the future is to be prepared, it must be one that engages and involves everyone, especially young people, and not simply legal experts and parliamentarians. Some of the mystique and charm of our ancient constitution might be lost in the process, but a written constitution could bring government and the governed closer together, above all by making the rules by which our political democracy operates more accessible and intelligible to all.
 
Nilisema hakuna Professor Tanzania, njaa mwanamalegeza. Ujinga, unaweza linganisha mazingira ya kisiasa yetu na Israel Uingereza? Shame up on him Propesa No.2. Katiba ipo but is not written on paper. Hapa ni makabila 128, quite diferent, how do you live by mila na desturi. Jinga Propesa! Uingereza kuna akina Ben wanapotezwa, Kunyimwa dhamana miezi mine, Israel inaweza tokea? Shame Propesa No. 2
Karibu kuelewa kabla ya kujibu kwa pupa, Prof. hajapinga uwepo Wa katiba, anajaribu kujenga hoja kwamba sio ya muhimu kuliko kila kitu kama tunavyo aminishwa na Mboye, ambaye naona amefanikiwa kukuaminisha pia na ww
 
Prof Kabudi kaamua kuweka uprof wake pembeni na kuuvaa unazi! Waingereza wamejichagulia mtindo wao wa maisha na sisi watz tumejichagulia mtindo wetu wa maisha. Watanzania wanataka katiba mpya!
 
Kabudi naye kaanza Yale Yale ya akina mwakyembe na akina migiro. Israel na uingereza sio kwamba hawana katiba ila ni kuwa hawa document moja kama hii ya kwetu lakini haimaanishi kuwa hawana katiba. Sisi tu nataka katiba kwa kuwa tumeona umuhimu wake. Mbona kuna nchi nzuri tu zenye katiba bora na zimefanya vizuri mf India, USA, Ghana, nk kwanini asizungumzie huko
 
Wanazo katiba ila ziko kwenye nyaraka tofauti tofauti Uingereza wana ,bill of rights,petiton of rights,Magna carta, habeas corpus,Act of setlement na mengine na mengine na sheria za bunge na maamuzi mengine ya kimahakama...
Umemuelewesha vizuri na aache kupotosha uingereza wana katiba ila hajaandikwa kwenye kitabu kimoja kama zetu yaani inaitwa unwriten constitution.
 
Back
Top Bottom