MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI,
Wafanyakazi wa NSSF, tunaendelea kuwasilisha malalamiko yetu kwako kuhusu ufisadi na ubaguzi uliopo shirikani ili ufanye uchunguzi wako na uchukue hatua stahiki ili kuliokoa shirika letu.
1. Udanganyifu katika utendaji wa shirika.
Mkurugenzi Mkuu kwa makusudi kabisa aliopoingia shirikani alipunguza malengo yaliyokwisha wekwa na mtangulizi wake ili aonekane 'anaperfom" hivyo taarifa zikawa zinapelekwa wizarani zikionesha anavuka malengo kwa mwaka wa 2018/2019.
Mwaka 2019/2020 kwa ujanja kabisa hakukuwa na ongezeko lolote la malengo bali alichofanya ni kujumlisha michango na wanachama waiohamia NSSF kutoka mifuko mingine kwenye makusanyo ya mwaka uliopita, hivyo inaonekana ameongeza makusanyo kwa asilimia kubwa sana na amekuwa akipita na kujisifu kwa hilo.
2. Ubaguzi kwa wafanyakazi.
Mkurugenzi huyu amekuwa akifanya ubaguzi wa wazi baina ya staff aliotoka nao PPf na sisi wa NSSF, kwa mfano staff wote wa PPF wamewekwa makao makuu tu hawapelekwi mikoani.
Aidha kuna staff ambao PPF hawakuwa na cheo chochote lakini walilopokuja NSSF wamepewa umeneja.
3. Ubaguzi katika mishahara.
Inafahamika wazi kuwa mfanyakazi wa umma anapohamishiwa kwenye taasisi nyingine anahamia na mshahara wake iwapo ni mkubwa.
PPF mishahara yao ilikuwa ni mikubwa kuliko NSSF. Lakini kwa hila kabisa akatumia kipengele cha kodi ya nyumba na kuwqaongezea mishahara staff aloikuja nao kutoka PPF, kisha wakaingia mikataba na mabenk chap chap wakaikopea nyongeza ile yote hii mantiki yake ni kukwepa hoja za CAG iwapo wangekopeshana kupitia mikopo ya shirika na vile vile kujilipa in advance in case of anything. Jamaa ni mjanja sana yeye na watu wake.
4. Dhuluma kwenye makato ya wafanyakazi.
Ndani ya NSSF kuna mpango wa uchangiaji wa wanachama wa NSSF-Hiari kwa wafanyakazi ambapo mwajiri anachangia 10% na mfanyakazi anakatwa 10%.
Mpango huu haupo NSSF peke yake bali mashirika mengi yana mpango kama huu kwa namna tofauti hata PPF walikuwa nao na walilipana mafao mifuko ilipounganishwa.
Mwezi Desemba 2018 mkurugenzi mkuu alisitisha kuchangia 10% yake bila taarifa yoyote huku akiendelea kuwakata wafanyakazi mpaka hivi leo licha ya wafanyakazi wengi kuandika barua kuomba makato hayo yasitishwe.
Mwezi Desemba 2019 mkuu huyu aliitisha baraza la majadiliano na kuwafahamisha kuwa alisitisha makato kutokana na agizo lako ulilotoa ulipokutana na viongozi wa mifuko mwezi Desemba, 2018 hivyo amekuja na mpango mpya ambao itabidi michango yote iliyokokwisha changiwa NSSF kiasi cha bilioni 23 kitolewe na uanzishwe mfuko binafsi wa wafanyakazi utakao kuwa na bodi yake na uongozi wake utakaojumuisha na wafanyakazi waliohamia.
Wawakilishi wa wafanyakazi walijua huu ni mchezo mchafu aina ya DESI, hivyo wakaugomea mpango huo na ikakubaliwa kuwa makato kwa wafanyakazi yasitishwe kuanzia mwezi Desemba, 2019.
Na michango iliyopo iendelee kubaki NSSF, Cha kushangaza makato yanaendelea mpaka sasa na hatujui kimsingi mkuu anahitaji nini hasa.
Mheshiwa Rais, tunaomba uingilie kati, kwani tunakufahamu na wewe ni msema kweli na mtetezi wa wanyonge.
Mungu akubariki!
Mbona watetezi wa Erio wote mmejiunga siku moja ya 8/1/2020?[emoji23][emoji23][emoji23]
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwingine wa 8/1/2020 kaja kwa lengo la kumtetea, nadhani wengi ndo wale wanaosemwa wanapewa upendeleo
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kweli kama yuko hivyo basi hana maana na kikono chake kama cha kuku[emoji85][emoji85]
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kabisa sema kama mwaka sasa mambo yamebadilika sana , kuna ofisi yao nilienda huduma zimekuwa imara sana hakuna majivuno tena kjna kaheshima flan hivi.. hakika Magufuli kapatia sana kumueka jamaa pale, nimependa uwazi kuhusu ulipaji wa vitu, mwendo ni kielektroniki.. kiukweli we are so proud to see proper working style. Aendelee kukaza wanyooke walizoea kurelax
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo kiongozi wenu yuko vizuri, hatukuwahi kusikia kelele wakati yuko PPF, tatizo mlizoeshwa vibaya huko NSSF sasa hamtaki kubadilika, pambaneni na hali zenu. Muheshimiwa Raisi, achana na hawa maboya, jenga taifa.
Pole mtoa post inaonekana nawe ni wale wale ambao mirija ya ulaji imefungiwa sasa muna mu attack Erio. Mulizoea dezo dezo tu kufanya Shirika kama shamba la bibi munakula pesa za wanachama bila huruma shirika linatafunwa kila upande na wafanyakazi wasio waaminifu sasa Erio amekuja ameziba mirija yenu yote ndio mnamu attack poleni sana Hapa ni Kazi tu kashasema Baba vipi sauti inatosha huko nyuma
Unajua Hii kasi ya sasa hivi inaonyesha kabisa watu waliozoea dezo pale mjengon NSSF inawapa watu mchecheto ndo yanazaliwa mambo kama haya... Maana hizi zinaonekana kama ni kelele za watu wachache wa Makao makuu tu... maana mkoan watu wapo busy na kutoa huduma fresh kabisa.. anyway ulaji dezo ukikata kelee hufunguka.. sema jamaa kama anakaza aendelee tu ili shirika lizidii kung'aa.. sisi wananchi tunataka matokeo kama tunayoyaona .. sio humo ndani mjomba ake nanj au nani kabanwa kufanya uhujumu wake. Mwachen Erio apige kazi kama PFF.. yani jamaa nachompendea ni Low Key Goal Getter... matokeo yanaongea zaidi
Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wewe ndo unaemtetea mwizi, erio na wenzake fuatilia historia zao ppf, record zinaonyesha wazi ni wapigaji ndo maana mwenzetu huko nyuma ameeleza jinsi walivyokua wanajilipa mamilioni kila baada ya miaka miwili, hadi mhasibu mkuu akafukuzwa baada ya kutaka kuzuia, pia ukisoma post za nyuma utaona kuwa wamejilipa immediately walivyojua wanakuja nssf na pia walipoingia nssf wakajilipa allowance ya furniture mamilion fasta fasta ila wakazuia mikopo ya furniture kwa staff angali wao walishajilipa kifisadi.
Usitetee ujinga tu soma watu wanacho complain uelewe
Sent using Jamii Forums mobile app
Wachangiaji wote wanaomtetea erio walijiunga JF January 8th, 2020 daaah Erio ana akili fupi sana kama kuku
We unaonekana ni staff uliebanwa mteremko wako.. sikushangai, Wizi haulipi ndugu yangu .. acha jamaa achape kazi.. mwache aendeleeeee kuwanyoosha vizuri kwa maslahi ya umma, wananchi hatutak watu design yako kwa sasa wanaojiangalia wao wenyewe
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kua we ni mfaidika mwenzake mliopiga pamoja huko ppf sikushangai, tetea ugali ndugu
Sent using Jamii Forums mobile app
Hushangai andiko lake Sababu nawe Join date yako ni 08/01/2020Sishangai andiko lako[emoji1787][emoji1787] unahitaji counselling ya kisasa kabisa, You sound low minded. Nenda ujue kufanya reasoning ya comments zako.
Sent using Jamii Forums mobile app
Bora umegundua aisee
Kwanini usijikite kwenye hoja husika ukaijibu moja baada ya ingine kuliko hili jibu la jumla?Pole mtoa post inaonekana nawe ni wale wale ambao mirija ya ulaji imefungiwa sasa muna mu attack Erio. Mulizoea dezo dezo tu kufanya Shirika kama shamba la bibi munakula pesa za wanachama bila huruma shirika linatafunwa kila upande na wafanyakazi wasio waaminifu sasa Erio amekuja ameziba mirija yenu yote ndio mnamu attack poleni sana Hapa ni Kazi tu kashasema Baba vipi sauti inatosha huko nyuma
Kwanini usijikite kwenye hoja husika ukaijibu moja baada ya ingine kuliko hili jibu la jumla?