Hbr Ya Asbh Wanajamvi, Leo Napenda Kupata Maelekezo Au Maelezo Kutoka Idara Ya Uhamiaji Tanzania, Swali Na Malalamiko Yangu, Ni Kuhusu Utoaji Wa Hati Za Dharura Za Kusafiria, Ambazo Watumiaji Wengi Ni Madereva Na Wasaidizi Wao, Kutoka Tanzania Kwenda Nchi Za Afrika Mashariki Na Kati, Awali Tulikuwa Tukipata Hati Hizo Kwa Muda Wa Mwaka 1 ,Kwa Gharama Tofauti Vituo Vingi Walichaji Elfu 20 Na Vingine Elfu 15 ,Hakuna Hata Risiti Walau Ile Ya Ticket Ya Bus, Sasa Tokea Mwisho Wa 2017 Utaratibu Umebadilika Kwa Kutoa Toka Muda Mwaka 1 Hadi Ya Safari 1 Tu (Single Journey) Yaani Ukitoka Na Kurudi Imeisha. Hivyo Ikiwa Kwa Mwaka Utasafiri Mara 10 ,Basi Yatupasa Tukate Hati Hizo Mara 10 Pia. Sasa Tatizo Ni Kila Safari Unatakiwa Uende Kwa Wakili Kuapa Kwa Kujaza Form Za Affidavits Na Kulipia Elfu 15 ,Na Hiyo Hati Ya Dharura (Passipot) Elfu 10 ,Passipot Size Elfu 3 ,Photocopy Kuanzia Kadi Za Gari, Leseni Ya Kuendesha Gari Na Kitambulisho Elfu 1.5 .Jumla Elfu 29.5 .Kila Safari. Swali Kwanini Kila Safari Lazima Niende Kwa Wakili Kuapa Tu!!!!?? Kwani Taarifa Za Safari Iiiyopita Zimeenda Wapi, Wkt Naona Anaweka Ktk Kompyuta!!!? Kwanini Mi Nikiwa Naomba Nyingine Nisiihie Kwa Afisa Uhamiaji Tu Kwa Kuchukua Taarifa Zangu Za Mwezi Uliyopita Na Kuthibitisha Kwa Hati Yangu Iliyoisha Ambayo Ninayo!!?!? Haya Kwanini Basi Wasingeiweka Iwe Walau Ya Miezi 6 Tu ,Kama Mwaka 1 Ni Mrefu Na Wao Wanakosa Makusanyo. Hivi Madereva Wana Kipato Kikubwa Kiasi Gani Hadi Kuwabana Na Kuwakamua Hivi Jmn, Sawa Lengo Kukusanya Mapato Mengi, But Hili Si Sawa Jmn, Hili Lipo Pale Uhamiaji Makambako Ndio Nimekumbana Nalo Binafsi. Tunawaomba Wahusika Mlitazame Hili Jmn.
