Mine eyes
JF-Expert Member
- Apr 11, 2016
- 6,434
- 7,094
Mkuu ungezitaja hapa na wengine wafaidikePole ..Mimi huwa natumia za kienyeji ..zinanisaidia tuu
Mkuu ungezitaja hapa na wengine wafaidikePole ..Mimi huwa natumia za kienyeji ..zinanisaidia tuu
Shukurani nasubiria mkuuMkuu pm yako nimeiona, na nimekujibu kaka, ondoa hofu.. hapa nafunga safari ya kwenda kwake nakupigia uongee nae ndugu yangu.
Sikukulenga wewe braza, kwani maelezo yako yalijitosheleza na hongera sana kwa hilo,Mie dawa siijui ntashare nanyi nini sasa.. nilichosema ni kwamba aje nimpe mawasiliano nae, kwani akija pm ndio nitawafanya nini, kama ningehitaji kitu mimi ndio ningewafata huko pm kwanza..
Siwez kuweka namba hapa.. samahanini kwa hilo.
Ukishaona msg ya njoo inbox jua tu huyo ni tapeliNinyi mnao muita inbox kwann msitoe hapa hiyo tiba ili na wengine wanufaike nayo??? huko inbox mnataka kuwafanya nini wenzenu.....
sio vizuri kama unajua kitu flani ukashare kwa wenzio hata baraka zinaongezeka.
Kuna mmoja nilifanya tu kumjaribu nika muinbox hahaha basi akasema aaah tuma laki mbili kwa namba hiyo nikutumie dawa,Ukishaona msg ya njoo inbox jua tu huyo ni tapeli
Sawa dada.Sikukulenga wewe braza, kwani maelezo yako yalijitosheleza na hongera sana kwa hilo,
Ila kuna watu walimuita pm ukisoma comments utaona.
Nakuja kwenu wanajamvi kuomba msaada wa mawazo nifanyeje niweze kuondokana na tatizo hili sugu na lililonitesa kwa miaka 22 sasa.
Tatizo hili liligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1995 hospitalini na nikaanza kutumia dawa na kufuata masharti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuepuka aina fulani za vyakula na madawa na pia kubadili lifestyle.
Nikiri kuwa baada ya muda fulani baada ya kuanza matibabu nilipata nafuu kubwa hadi husahau maumivu ya tatizo hili lakini nilijitahidi kubaki katika masharti yale.
Baadaye tatizo lilianza upya na nikaanza kutumia dawa zile zile nilizotumia awali lakini sikupata nafuu. Nimebadilisha dawa mbalimbali lakini bado tatizo limeng'ang'ania. Baadhi ya dawa ninazokumbuka nilizotumia mpaka sasa ni: CIMETIDINE, RANITIDINE, OMEPRAZOLE, PANTOPRAZOLE, LANSOPRAZOLE na Antiacids za maji kama MILK OF MAGNESIA na RELCER GEL.
Nimewahi pia kutumia dawa za kienyeji kadhaa bila mafanikio. Mfano: Unga wa mbegu ya parachichi, mafuta ya ubuyu, asali mbichi na mdalasini, kuchemsha mmea wa mbigili n.k.
Nimeshawahi pia kupima H.PYLORI TEST mara 2. Mara moja nilikutwa Positive nikapewa HELIGO KIT dozi ya wiki 2 na nikaendelea na lansoprazole kwa wiki 2 zaidi. Nilipopima tena H.PYLORI ikasoma Negative lakini bado nikindelea kuumwa.
Mwaka jana nilifanyiwa kipimo cha OESOPHAGOGASTRODUODENOSCOPY hospitali moja ya rufaa na ripoti ya Daktari ilisomeka: "Multiple wounds found around the duodenum". Nilipewa dawa lakini bado sikuona nafuu kubwa.
Hivi leo nina siku ya 6 natumia TINIDAZOLE, LANSOPRAZOLE NA CLARITHRIMYCIN kwa pamoja na bado sijisikii nafuu yoyote. Maumivu ni makali, tumbo linauma na kutonesha (painful & tender), nikila chakula kidogo tu nasikia tumbo limejaa. Siwezi kulalia ubavu wa kulia tena sababu ya maumivu.
Usiku wa leo tumbo liliniuma sana mpaka jasho likanitoka japo kulikuwa na baridi.
Kwa ufupi nateseka jamani na nimekuja kwenu kama kuna mhanga kama mimi aliyewahi kuugua tatizo hili na kupona au madaktari mliomo humu jamvini mnisaidie jinsi ya kufanya.
Natanguliza shukurani nikiomba radhi pia kwa post ndefu. Nimelazimika kuandika hivi ili tatizo langu lieleweke vema.
ASANTENI!
Mwanajamvi mwenzenu anayeteseka.
Asante sana ndugu kwa mchango wako.Niliupoteza huu Uzi
Kiboko ya Dawa zote hizi ni Juice ya Kabichi au Cabbage wazungu wanaiita.
•Cabbage/Kabichi
•Muwa au Apple
•Maji Safi
Saga mchanganyiko huu kwa Blender hadi upate Juice nzito nzito.
Kaza Moyo maana ladha yake Mhhh Kunywa Juice hii Glass kubwa 2 au 1 kutwa mara tatu. Alafu njoo tupe mrejesho.
Dawa nyingine nzuri pia ni Juice ya mboga za majani na matunda ( Detox )
•Mboga yoyote Ya Majani isiyokuwa na Acid
•Muwa
•Mtindi
•Maji Safi
•Apple
Saga huo Mchanganyiko kwenye blender kunywa utakavyoweza itakusaidia sana.
Katika zote hiyo ya Cabbage ni nzuri zaidi.
Angalizo: Usiweke Sukari hata kidogo. Uwepo wa Muwa na Apple ni kuleta hiyo ladha ya Utamu hata mtindi ni vizuri ukitumia ule wenye ladha za matunda.
Ushauri mzuriAiseee sikutishi ila vidonda vyako vipo stage ya mwisho be careful sana,
Nakupa dawa tatu usidharau kabisa.
Moja, chukua bamia kata kata vipande weka kwenye blender na glass ya maziwa blend kisha kunywa asubuhi kabla hujala chochote na usiku nusu saa baada ya kula.
Najua itakupa shida kumeza ila pambana utanipa mrejesho.
Dawa ya pili, unga wa mbegu za mlonge,
Chukua kijiko kimoja cha unga huo weka kwenye maziwa au uji kunywa, unaweza kuharisha au kutapika au vyote, usijali jikaze endelea kutumia.
Dawa ya tatu ni maziwa mtindi,
ndio glass moja ya maziwa mtindi kila siku asubuhi mchana na jioni, utaleta mrejesho.
Achana na hizo dawa za hospital hakuna tiba bali zinapunguza makali halafu kumbuka unazidi kujaza chemical mwilini.
NB: Kama una kawaida ukisikia maumivu ya tumbo unakunywa maziwa fresh nakushauri acha mara moja, maziwa fresh huzidi kukwangua kwenye vidonda lakini mtindi wale bacteria wake ndio tiba yako.
Pilipili ipi mkuu, maana zpo aina nyingi aiseeeTumia pilipili mzee. Utapona utabaki na historia tu .. Ila mwanzoni utapata shida sana
Sasa nyie wa kutaka pm, aiseeee mnaboa pia maana ya hili jamvi linapungua ubora,, toeni hapa watu wajue dawa, ili wajitibu aiseeePole sana nicheck private nikupe dawa alafu utakuja kutoa ushuhuda