SEMKIWA3
Senior Member
- Feb 17, 2019
- 103
- 59
Habari zenu wanaJF.
Niende moja kwa moja kwenye mada,ugonjwa wa denguo ni ugonjwa ambao umekuwa tishio sana kwa sasa hapa nchini hususani maeneo ya Dar es salaam na Tanga.
Ugonjwa huu ulikuwepo tangu awali lakini kwa sasa umekuja kwa kasi mpya zaidi kiasi cha kuenea hadi mikoani,kama ambavyo awali tulifahamu kuwa ugonjwa huu ulikuwepo sana ndani ya jiji la Dar es salaam lakini sasa umeanza kuenea mikoani hasa mikoa ya jirani na tanga.
Chini nitaweza attachments za picha zikionyesha taarifa sahihi kuhusu ugonjwa huu wa denguo.
Mimi kama mwanafunzi wa chuo kikuu kishiriki cha elimu cha Dar es salaam yaani DUCE janga hili la gonjwa la denguo limeniathiri sana mimi pamoja na wenzangu tuliopo hapa chuoni.
Wiki iliyopita marafiki zangu kama sita wote walipatwa na ugonjwa huu hadi kupelekea kulazwa katika hospitali za Baracks na Kairuki Victoria,licha ya wote hawa kuumwa na kulazwa kila mara,siku ya jana tumempoteza mwanafunzi mwenzetu wa kike aliyekuwa anasoma mwaka wa pili,kiukweli hili ni pigo kubwa sana kwetu.Sisi kama wanafunzi wa chuo kikuu hili jambo kweli limetufika licha ya kuwa tupo makini sana kupambana nalo lakini ni hatari zaidi.
Chini hapa pia nitaweka attachment ya kitambulisho cha mwanafunzi huyu anayeitwa MARRY KISAKA ili tumfahamu sote wanaJF.
R.I.P dear Marry Kisaka,wengi tulikupenda ila mungu alikupenda daima.
Niende moja kwa moja kwenye mada,ugonjwa wa denguo ni ugonjwa ambao umekuwa tishio sana kwa sasa hapa nchini hususani maeneo ya Dar es salaam na Tanga.
Ugonjwa huu ulikuwepo tangu awali lakini kwa sasa umekuja kwa kasi mpya zaidi kiasi cha kuenea hadi mikoani,kama ambavyo awali tulifahamu kuwa ugonjwa huu ulikuwepo sana ndani ya jiji la Dar es salaam lakini sasa umeanza kuenea mikoani hasa mikoa ya jirani na tanga.
Chini nitaweza attachments za picha zikionyesha taarifa sahihi kuhusu ugonjwa huu wa denguo.
Mimi kama mwanafunzi wa chuo kikuu kishiriki cha elimu cha Dar es salaam yaani DUCE janga hili la gonjwa la denguo limeniathiri sana mimi pamoja na wenzangu tuliopo hapa chuoni.
Wiki iliyopita marafiki zangu kama sita wote walipatwa na ugonjwa huu hadi kupelekea kulazwa katika hospitali za Baracks na Kairuki Victoria,licha ya wote hawa kuumwa na kulazwa kila mara,siku ya jana tumempoteza mwanafunzi mwenzetu wa kike aliyekuwa anasoma mwaka wa pili,kiukweli hili ni pigo kubwa sana kwetu.Sisi kama wanafunzi wa chuo kikuu hili jambo kweli limetufika licha ya kuwa tupo makini sana kupambana nalo lakini ni hatari zaidi.
Chini hapa pia nitaweka attachment ya kitambulisho cha mwanafunzi huyu anayeitwa MARRY KISAKA ili tumfahamu sote wanaJF.
R.I.P dear Marry Kisaka,wengi tulikupenda ila mungu alikupenda daima.

