Ugonjwa nchi hii si majipu pekee

xaracter

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,026
606
Naanza kupata wasiwasi kuwa baada ya miaka kumi tutakuwa pale pale au vibaya zaidi kwa kuwa nchi hii ina maradhi mengi.

Tukifanya siasa za kutumbua majipu pekee, basi malaria kipindupindu, ngoma nakadhalika hata visipotuua vitatudumaza.

Fikra pevu na pana zinahitajika kuhakikisha tunatoka hapa tulipo ukitaka kujua nchi hii ina maradhi mengi angalia kamati za bunge zilizochaguliwa watu wameondoa wenya macho na kutuwekea vipofu watuongoze.

Afrika itaendelea tu pale tutakapoepukana na utumwa wa kifikra.
 
Lakini najiuliza kWa nini

hawana Ujasiri wa kitumia NENO Ufisadi ambalo ni rasmi kisheria linakubalika?

Majipu ni nini?? Si lughaa tu ya kisanii ???
Toka mwaka 1990,
Kura yangu inaendelea kupanda thamani !!

Sijawahi kuchagua Mafisadi
Mabadiliko hayawezi kutokea kupitia kwa watu wale(chama) wale mfumo uleule

Hata kama ni Malaika
 
Back
Top Bottom