Naombeni kwa anaejua ni kipi bora kati ya ufugaji wa kondoo na ng'ombe wa kienyeji kwa maeneo ya Kahama shinyanga. Yani kipi kinaweza kuwa kinalipa kwa uharaka kuzidi kingine?
Ahsante naomba kuwasilisha
Mkuu, vyote ni vinalipa LAKINI inategemea na factor nying, mfano malengo yako, soko lako mtaji ulionao NK
Ni vizuri ukajiuliza kwa context ya TANZANIA kati ya nyama ya KOndoo, mbuzi na ngombe nini kinalika zaidi? mara nyingi ukitoa mikoa ya Arusha na kwa mbali Singida sijawahi ona NYAMA ya KONDOO buchani, najaribu kusema nini, fuga kitu ambacho hata ukiwa na shida unaweza peleka buchani ukapata pesa, walaji wa kondoo ni wachache saana miongoni mwetu watanzania
UFUGAJI unalipa KAMA utatumia akili,, usifuge kama babu zetu walivyokuwa wanafuga,,, anza na malisho pata malisho ya kutosha, nunua ngombe kipindi cha kiangazi ..wape balanced diet ndani ya miezi mitatu peleka buchani, hiii hata kama unauishi eneo dogo unaweza kufanya==same applied hata kwa mbuzi...hutaingia garama kubwa na wala hutakaa na mifugo muda mrefu
Kidumu chama cha MAPINDUZI