Ufoo Saro na Malumbano ya hoja

Ufoo Saro na Malumbano ya hoja

hunchback

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2014
Posts
658
Reaction score
289
Nimekuwa nikifuatilia kipindi cha malumbano ya hoja kwa muda mrefu sasa. Toka Ufoo Saro awe miongoni mwa waongozaji kipindi kimepwaya.

Mtangazaji huyu amekuwa akiingilia au kukatisha hoja za watu pasipo kuwa na sababu za msingi. Kuna wakati anaonekana ni mwenye jazba sana.

Ushauri wangu: Ufoo ajitahidi kudhibiti hisia au kuondoa uoga ili kipindi kiwe na mantiki nzuri zaidi na kivutie badala ya kupoteza watazamaji.
 
Hiki kipindi kimepoteza umaarufu tangu wamweke Ufoo Saro. Hakina mvuto kwa kuwa Ufoo Saro hana hekima wala busara. Wangemwacha akawa anaripoti tu matukio. She is a total failure ila anabebwa tu.
 
Naona Ufo Saro amewabana sana watoa hoja au wachangiaji kiasi kwamba kipindi kimekuwa ni malumbano na Ufo Saro na sio malumbano ya hoja.

Naona mpaka Juma Kapalatu ameamua kuwa mpole, haongei.

Sijui wenzangu mnaonaje
 
Itv mtoebi huyu dada mara moja anakera sana na anakifanya kipindi kiwe cha ovyo sanaa!anakera mnooo
 
Kipindi kime kosa mvuto siku hizi wala sina mpango nacho siku nyingi bora mzee masaki kesho
 
Nahsi kma vile anafagilia kibarua hv...yan haiwezekani mtu anatoa hoja kisha yeye anamkatisha,unajua mtu anapotoa point zake then wewe ukamkatisha kinachofuatia ni kwmb yule mtoa hoja huwa anachanganyikiwa hv yan unamtibua.Yeye inapofikia mtoa hoja ametoa vielelezo kukazia hoja ikiwa ni pamoja na kutajwa mtu au chama,huyu dada huwa mkali sasa sijui malumbano gani yasiyoruhusu hata kutoa mifano...me naona tumsamehe tu ila uzuri ni kwamba kwa sasa wa kumdanganya hayupo ni mabadiliko tuu japo yeye hayataki..
 
kuna mzee kapaniki hapa anajitahidi kuingiza siasa daaah.. bora uchaguz upite watu wawe "wao" maana sijui tumetekwa na nn
 
Naona Ufo Saro amewabana sana watoa hoja au wachangiaji kiasi kwamba kipindi kimekuwa ni malumbano na Ufo Saro na sio malumbano ya hoja.

Naona mpaka Juma Kapalatu ameamua kuwa mpole, haongei.

Sijui wenzangu mnaonaje

Huyo Dada sijui atajibu nini siku ya hukumu mbele ya PILATO. Kuna siku humu humu nilikuja na UZI wa kumuhusu huyu Dada lakini watu wakaanza kunishambulia ila kesho yake kuna baadhi ya STAFF wenzake wananitumia PM za kutosha kwa kuniambia kuwa nilipoanzisha ule UZI utadhani nilikuwa katika FIKRA zao kwani wanasema ni Dada MJIVUNI, MBABE, MPENDA SIFA KWA UONGOZI, ANAPENDA UKUBWA na ana KIMBELEMBELE sana na taratibu sasa hayo MADHAIFU yake members wengine MNAOJITAMBUA mmeanza kuyaona.

In short KIPINDI kimemvaa ILA hajakivaa. Dada Fatma Almasi Nyangasa aliyehamia AZAM Tv na Dada Magreth Cosmas ambaye bado yupo hapo walikuwa WANAKITENDEA sana haki hiki Kipindi kuanzia MVUTO wao wa KIMWONEKANO na wa kujua KUKICHANGAMSHA Kipindi.

ITV kwa huyu Dada mnacheza style ya wimbo wa Reggae wakati mdundo wa wimbo unaopigwa ni wa Ndombolo.
 
Hata me naona leo ni tofauti zaidi,cha muhimu kila mtz. asikate tamaa tujitokeze kwa wingi oktoba 25 kupiga kura.Tuhamasishane vinginevyo kujikwamua kimaendeleo itakuwa ni ndoto.
 
Naona Ufo Saro amewabana sana watoa hoja au wachangiaji kiasi kwamba kipindi kimekuwa ni malumbano na Ufo Saro na sio malumbano ya hoja.

Naona mpaka Juma Kapalatu ameamua kuwa mpole, haongei.

Sijui wenzangu mnaonaje

Ameharibu totally mi kaniboa kinyama manusura niswitch off tv nikalale sema nilikuwa na hamu ya kujua mawazo ya watu kuhusu amani na uchaguzi nikavumilia.
 
Nikweli kabisa mkuu, nilidhani nimeliona hili mwenyewe kumbe nawe umeiona. Huyu dada kapwaya sana.. Na hafai kuendesha hiki kipindi maana ANAJIONA,MJUAJI, MBISHI na analazimisha wachangiaji wafikiri anavyofikiri yeye. # ITVFUKUZAUFOOSARO
 
Tena nakiswahili chake cha kuchapia basi anazidi kubwa kero kweli.mwenzie J.Kapalatu kakaa kimya nadhani alisoma salama za nyakati wasionekane wote kubwa wajinga.
 
Back
Top Bottom