Ufisadi umezidi jimbo la Ismani kwa Lukuvi

Manywele.

Member
Nov 25, 2011
25
3
Kadri siku zinavokwenda ndivyo hali inavyokuwa tia maji tia maji katika jimbo la ismani kwa mheshimiwa Lukuvi kuanzia kijijini kwake Idodi na maeneo mengine jimboni humo. Tatizo kubwa linalozidi kuwa sugu kila kukicha ni maji ambapo vyanzo vyake vinazidi kukauka kila kukicha, na miundo mbinu ikiwapo mabomba vikiwa vimechoka taabani hadi kupelekea mabomba yaliyotumika miaka ya 8
0 na 90 leo hii zmebaki alama tu na viongozi wakilifumbia macho hili akiwamo mbunge wetu (mungu mutu) Lukuvi ambae ni mbunge wa pili jimboni humo toka alivyo mpindua MWADUMA. Lkn kinacho nikitisha ni pale ambapo wanakijiji waliamua kuchangia hela sh.4000/= kwa kila mmoja ili kukarabati miundo mbinu ya maji na hela ya kumlipa fundi wakufuatilia ambae kwa kata ya nduli alikuwa akilipwa sh.30000/= kwa mwezi na usafiri wake ukiwa ni baiskel tu. Hakika hela zilichangishwa kwa kila mwanakijiji na aliegoma alikamatwa na kupelekwa jela. Ila chaku skitisha hela hizo hadi leo hazieleweki ziko wapi na zilitumika vipi kwani hakuna htduma yeyote ambayo ili rekebishwa na tukihoji ktk vikao tunaambiwa ziko banki hadi leo na ikiwa ni mwaka wa nne sasa. Lkn kwa habari zakuaminika wale walio husika na michango hiyo i mean viongozi wa maji na wenye viti wa vijiji sasa wamenunua magari ya biashara, wamejenga nyumba za kifahari pamoja na vitega uchumi vingine vikiwemo kufungua bar, maduka, mifugo(ngombe) na mashamba: My take mali zote hizi wamezipata wapi, na kwa kazi gani hapa vijijini wapate utajiri wa haraka haraka hivi kwa kipindi cha miaka minne hii hii kama sio michango yetu ya maji na huduma nyingine kama afya na elimu?
 
Kijiji hicho kina idadi ya watu wangapi mpaka michango hiyo itoshe watu kujenga nyumba za kifahari na kununua magari kwa Tshs 4000@?
 
Back
Top Bottom